Sunday, July 13, 2014




Msanii mkongwe kwenye game la Bongo Fleva anajulikana kwa jina la Prof Jay leo mchana alikuwa akishoot video yake mpya aliyomshirikisha Diamond inaitwa KIPI SIJASIKIA. Video hiyo iliyokuwa ikishutiwa pale Sinza Makaburini ilipo Mahakama. Video imesimamiwa wa Dir Adam Juma kutoka Next Level

Prof Jay akiwa na Prod P Funk Majani,

DJ Choka akiingia mahakamani

Uholanzi yaibana Brazil 3-0 na kutwaa nafasi ya tatu katika kombe la dunia.
Uholanzi ilimaliza katika nafasi ya tatu katika kombe la dunia huko Brazil baada ya kuchomeka msumari wa moto ndani ya kidonda cha wenyeji walipowalaza mabao 3-0 mjini Brasilia siku ya jumamosi.
Mashabi wa Brazil waliwazomea wachezaji wao akiwemo kocha Luiz felipe Scolari kwa utendakazi duni katika mechi hizi mbili za mwisho Brazil ilipofungwa mabao 10 nayo ikifunga moja.
Brazil ilifungua mechi hii kwa kasi lakini ikafungwa bao la kwanza kunako dakika ya pili ya mechi hiyo kupitia kwa mkwaju wa penalti uliopigwa na Robin va Persie.
Scolari atakuwa na wakati mgumu kuandikisha kandarasi mpya
Nahodha Thiago Silva alimtega Arjen Robben nje ya eneo lakini refarii kutoka Algerian Djamel Haimoudi akaamua kumwadhibu kwa kadi ya njano na penalti dakika mbili tu baada ya mechi hiyo kuanza badala ya kumwonesha kadi nyekundu .
Mashambulizi ya Uholanzi yalizaa matunda kunako dakika ya 15 ya mechi hiyo David Luiz alipookoa mkwaju uliokuwa unaelkea wavuni kwa kichwa lakini ukamwangukia Daley Blind naye akaurejesha humohumo .
Brazil imefungwa mabao 10 katika mechi mbili
Kila mtu uwanjani alifurahia Brazil walipofanya mashambulizi kwenye lango la Uholanzi lakini kila mara walipofika katika eneo walikosa makali na kushindwa kupenyeza safu ya ulinzi ya Uholanzi.
Uholanzi walisalia kulinda ngome yao na kila walipopata fursa walitekeleza mashambulizi kwa lango la Selecao ambao walionekana imara tofauti kabisa na timu iliyodenguliwa 7-1 na Ujerumani juma lililopita huko Belo Horizonte.
Hata hivyo Georginio Wijnaldum aliifungia Uholanzi bao la tatu kwa nunge na kumpa kocha Louis va Gaal kwaheri na nishani ya shaba kutoka kwa fifa.
David Luiz alisababisha Brazil kufungwa tena
Kwa upande wake Scolari alisalia na maswali mengi bila majibu baada ya safu yake ya ulinzi kuvuja mabao 10 katika mechi mbili.
Bila shaka atakuwa na kibarua kigumu akijaribu kuiokoa kibarua chake kisiote nyasi punde baada ya kipenga cha mwisho cha kombe la dunia huko Maracana jumapili julai tarehe 13 .
Wachezaji wanaotarajiwa kufunga mabao katika fainali
Jumapili ya tarehe 13 Julai mwaka wa 2014 hatimaye imewadia .
Macho yote duniani yatakuwa yanaelekea katika uwanja wa Maracana ulioko Rio Brazil ambapo mechi ya fainali ya kombe la dunia itakuwa ikichezwa.
Mahasaimu wa Jadi Argentina watakuwa wakichuana na Ujerumani katika fainali yao ya tatu katika historia ya kombe la dunia.
Mechi hiyo ndiyo itakayokuwa kilele cha majuma manne ya kipute hicho kilichojumisha timu 32 kutoka mabara yote 5 zikichuana miongoni mwao katika miji 12 ya Brazil kuanzia juni tarehe 12 .
Hayo yote ni kenda timu hizo zote zilikuwa zikiwania kuandikisha majina yao kwenye tuzo la kipekee la dhahabu yaani kombe la dunia.
Katika mechi hii ya leo Mahasimu hawa wanafahamiana sana.
Mashabiki wakijiandaa kwa fainali ya kombe la Dunia
tayari wamechuana mara saba tatu zikiwa ni katika fainali za kombe la dunia mwaka wa 1986 na 1990.
Ujerumani ilishinda mara moja nayo Argentina ikaibuka mshindi mara moja kwa hivyo hii leo itakuwa mechi ya kukata na shoka .
Wajermani wakiandikisha rekodi kwa kuinyeshea wenyeji Brazil jumla ya mabao 7-1 katika nusu fainali huku Argentina nayo ikihitaji muda wa ziada na hata mikwaju ya penalti kuibandua Uholanzi na kufuzu.
Ujerumani itakuwa timu ya kwanza kutoka bara Ulaya kutwaa kombe la dunia katika Marekani ya kusini iwapo itaipiku Argentina.
Timu ya Argentina itakayochuana na Ujerumani katika fainali ya kombe la duniahuko Brazil.
Argentina nayo inakumbuka vyema matukio ya miaka 28 iliyopita ilipoilaza Ujerumani Magharibi wakati huo na kutwaa kombe lao la mwisho la dunia je Historia itajirudia ?
Kama ilivyokuwa katika mech za awali Argentina itakuwa inamtegemea Lionel messi kwa ufungaji mabao kwani hata sasa Di maria bado ni shaka iwapo atacheza au la kutokana na jeraha la paja.
Iwapo atafaulu katika Fainali ,Messi atakuwa bila shaka katika mizani sawa na aliyekuwa nyota wa Argentina Diego Maradona na hata kumpiku kocha huyo wa zamani.
Kwa Upande wao Ujerumani imesifiwa kwa kuwa na uwezo wa kipekee wa kucheza kama kikosi wala sio kumtegemea nyota mmoja kwa ufungaji mabao.
Timu ya Ujerumani itakayochuana na Argentina katika fainali ya kombe la dunia huko Brazil.
Vijana wa Joachim Loew wanamtarajia mfungaji wao nyota Miroslav Klose akisaidiana na Thomas Muller kuwapa mabao na hatimaye ushindi dhidi ya Argentina .
Takriban tiketi elfu 75.000. zimeuzwa na hadi sasa kinachosubiriwa ni kujua iwapo mashabiki wa Brazil watawashabikia majirani wao lakini hasimu wa jadi Argentina, ama timu iliyoandikisha rekodi ya kuifunga Brazil mabao mengi zaidi katika historia Ujerumani.
Dakika tisini zijazo ndizo zitakazoamua mbivu na mbichi

waliotembelea blog