Wednesday, July 8, 2015

.

Mwimbaji kutokea muziki wa dansi, Christian Bella ameongea kwenye AMPLIFAYA ya Clouds FM July 8, 2015 na kuthibitisha kwamba kukosa tuzo sehemu yoyote au kwenye tuzo zozote haitampelekea yeye kujiondoa kushirikishwa kwenye tuzo.
.
Anaamini kuna vitu vingine vinatokea kwa binadamu..’Cha muhimu nini unafanya na jamii inapokea kazi yako vipi waliopata tunawapa hongera ukiangalia vizuri kuna mapungufu ambayo yalionekana live kwangu mimi nachukulia powa kwasababu sio mara yangu ya kwanza mimi katika mambo ya tuzo sinanga hiyo sifa kwamba mimi wananipanga tuzo hapana lakini najitahidi sana kufanya muziki mzuri aina muziki ninayoufanya ni kufurahisha watu wote’- Christian Bella
.
‘Wao wakijaji kwamba labda kuna vitu gani ili msanii apate kwasababu huwezi kumpa msanii tuzo eti mwandishi bora wakati hajaandika nyimbo yoyote au huwezi kuwa mwimbaji bila kuwa na hits haujafanya chochote umetoa nyimbo haijakubali no mwimbaji bora au mtumbuizaji bora inategemea alichokifanya mwaka uliopita umezunguka wapi na wapi ili upate hiyo tuzo unavyoniambia mimi ni dancer bora itabidi nioneshe mwaka jana nilifanya vitu vya maajabu hata wewe ni dancer bora lakini kama haujafanya kitu una tuzo siwezi kuwaingilia kitu kabisa’- Christian Bella
.
.
‘Siwezi kuwainglia mambo ya tuzo waendele tu na idea zao wanachokifanya mimi bella sio lazima tuzo lakini mashabiki wanavyokubali kazi zangu ndio napata furaha sana wakitoa tuzo na wasipotoa siwezi kujitangaza mara ooh bella sijui hivi na hivi kuhusu tuzo hapana naomba tu makampuni yaongezeke ili yawe yanatoa tuzo’- Christian Bella.

.


waliotembelea blog