Wednesday, July 16, 2014


On the move: Chelsea midfielder John Obi Mikel has been linked with a transfer to an Italian club
Anatimka zake: Kiungo wa Chelsea, John Obi Mikel anahusishwa kuhamia klabu za Italia.

Imechapishwa Julai 16, 2014, saa 12:08 asubuhi

KLABU ya Chelsea wanatarajia kumuuza kiungo wao raia wa Nigeria, John Obi Mikel, huku kukiwa na taarifa kuwa klabu za Italia zimekubali kutoa ofa ya paundi milioni 5.
Mikel alianza katika mechi 11 tu za ligi kuu msimu uliopita   na alipata upinzani mkubwa kutoka kwa Nemanja Matic, Willian na Ramires.
Kitendo cha kiungo Cesc Fabregas kujiunga na klabu hiyo kutokea katika klabu ya Barcelona kwa dau la paundi milioni 30 kunazidi kufinya nafasi ya Mikel msimu ujao.
New boy: Cesc Fabregas has joined Chelsea from Barcelona in a £30million move this summer
Kijana mpya: Cesc Fabregas amejiunga na Chelsea majira haya ya kiangazi kutokea klabu ya Barcelona.

Mikel, aliyecheza katika mechi zote za Nigeria katika fainali za kombe la dunia za mwaka 2014 nchini Brazil na kufika hatua ya pili na kupigwa na Ufaransa, amesema kuondoka kwake si kwasababu ya kuwasili kwa Fabregas.
Alisema: "Sina tatizo na kusajiliwa kwa Fabregas," alisema. "Tulikutana mara kwa mara. Hata hivyo hatuchezi nafasi moja".
Wakatai huo huo, beki wa Chelsea, Patrick van Aanholt amethibitisha kuondoka klabuni hapo na anaweza kurithi nafasi ya mchezaji aliyesajiliwa na Newcastle Daryl Janmaat katika klabu ya Feyenoord.
Mholanzi huyo mwenye miaka 23 alijiunga na akademi ya Chelsea mwaka 2009 akitokea PSV Eindhoven, lakini amecheza mechi mbili tu na alitumia msimu uliopita kucheza kwa mkopo katika klabu ya Vitesse.
Van Aanholt ameichezea Uholanzi katika mechi mbili na ameiwakilisha nchi hiyo katika ngazi zote kuanzia miaka 16.
On his way: Patrick van Aanholt has been linked with a move to Feyenoord in Holland +
Anasepa zake: Patrick van Aanholt  anahusishwa kujiungga na  Feyenoord ya nchini Uholanzi.

1951Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
KOCHA wa Simba sc, Mcroatia, Dravko Logarusic ameanza kazi kukinoa kikosi chake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara katika uwanja wa Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Loga ameamua kuanza kambi mapema kwa lengo la kurejesha heshima ya Simba iliyopotoea kwa miaka mitatu mfululizo.
Katika mazoezi hayo, wachezaji wa zamani ambao hawapo katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania,  Taifa Stars kinachojiandaa na mechi ya Julai 20 dhidi ya Msumbiji wanahudhuria pamoja na wachezaji wapya.
Mshambiliaji wa zamani wa Supersport United ya Afrika kusini, Dani van Wyk amekuwa akihudhuria mazoezi hayo kama sehemu ya kujaribiwa na Loga kabla ya kufanya maamuzi ya kumsaininisha mkataba.
Mchezaji huyo amekuwa akijitahidi kuonesha uwezo wake, lakini Loga anasema anahitaji muda kumtazama kabla ya kufikia makubaliano.
Mlinda mlango bora wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita, Hussein Sharrif `Iker Casillas` amesharipoti kuanza mazoezi na Simba baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili akitokea Kagera Sugar.
Wachezaji wengine wapya walioanza mazoezi ni pamoja na Michael Mgimwa kutoka Thailand, Mohammed Hussein maarufu kama Tshabalala kutoka kwa `wanankulukumbi`, Kagera Sugar.
1
Wakati Simba wakiendelea na mazoezi hayo, nao watani wao wa jadi, Yanga sc wanaendelea kunoa makali katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola chini ya kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo akisaidiwa na Leonardo Neiva.


Straika wa Atletico Madrid Diego Costa amekamilisha Uhamisho wake kwenda Chelsea na kusaini Mkataba wa Miaka Mitano.
Inaaminika Dau la Uhamisho la Straika huyo Mzaliwa wa Brazil lakini anachezea Spain ni Pauni Milioni 32.
Costa anakuwa Mchezaji wa 3 kuchukuliwa na Chelsea kwa ajili ya Msimu mpya na wengine ni Cesc Fabregas na Mario Pasalic.

Msimu uliopita akiwa na Atletico Madrid, Diego Costa alipachika Bao 36 katika Mechi 52 na kuisaidia Klabu yake kutwaa Ubingwa wa La Liga na kufika Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI waliyodundwa 4-1 na Real Madrid.
Costa


MCHEZAJI wa zamani wa Arsenal na Chelsea Ashley Cole amesema Wachezaji wa England ni waoga kwenda kucheza Klabu za Kigeni.Cole, mwenye Miaka 33, amejiunga na AS Roma ya Italy baada kuondoka Chelsea kufuatia kumalizika kwa Mkataba wake ambao haukuongezwa.
Akiongea na Wanahabari kwa mara ya kwanza kama Mchezaji wa AS Roma, Cole alitamka: “Wachezaji wa Kiingereza pengine wanaogopa kwenda nje ya Nchi, wanajisikia vyema kubaki Nyumbani.”
Kwenye Kikosi cha England kilichokwenda huko Brazil kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia ni Kipa Fraser Forster pekee ndie alikuwa hachezei Klabu ya England lakini nae hakwenda mbali kwani alikuwa Scotland akichezea Celtic.


Akiongea kuhusu kuhamia AS Roma, Cole amesema: “Hii ni nafasi kwangu kujaribu lugha nyingine, utamaduni na maisha mapya.”

Aliongeza: “Siogopi presha. Nimeona ari ya Mashabiki na mapenzi yao nilipotua tu. Nitasikia raha hapa!”
Ingawa Chelsea walikataa kumpa Mkataba mpya, Cole amesisitiza bado anao uhusiano mzuri na Meneja wa Klabu hiyo, Jose Mourinho.
Cole amesaini Mkataba wa Miaka Miwili na AS Roma na Msimu ujao watashiriki UEFA CHAMPIONS LIGI baada ya kumaliza Ligi ya Serie A wakiwa Nafasi ya Pili nyuma ya Mabingwa Juventus.


Fans greet the Germany teamGermany wamerudi Nyumbani kwao Berlin wakiwa na Kombe la Dunia mkononi baada kuwafunga Argentina 1-0 Juzi na kupokewa kwa shangwe kubwa na maelfu ya Wajerumani.That went well! Philipp Lahm and Thomas Muller pulled off a stunt on stage in Germany on Tuesday
Nahodha Philipp Lahm, akifuatiwa na Bastian Schweinsteiger, aliwaongoza Wachezaji wenzake kushuka toka kwenye Ndege.
Maelfu ya Wajerumani walikuwa wakiisubiri Timu yao katikati ya Jiji la Berlin, huko Brandenburg Gate, kwenye eneo linaloitwa Fan Mile, na Kikosi hicho kikiongozwa na Kocha Joachim Low kilikuwa kikizungushwa Mitaa ya Berlin wakiwa juu ya Basi la wazi na kuishia hapo Brandenburg Gate.
Having a ball: Christoph Kramer pretends to play the guitar as they entertain the huge crowd
Huku Mashabiki wakiimba: "Deutschland, Deutschland, Deutschland!", Kocha Low na Wachezaji wake walipokezana kuinua Kombe la Dunia juu na Basi kupita popole likilakiwa na kusindikizwa na Mashabiki kibao.
Boy band material? (from left) Hummels, Lahm, Durm, Kramer and Muller all get in on the guitar act
Huku wakiwa kwenye msafara huo, Wachezaji kadhaa wa Germany walichukua picha kwenye Simu zao na kuziposti moja kwa moja kwenye Twitter huku wakitoa maneno ya furaha.
Hii ni mara ya 4 kwa Germany kutwaa Kombe la Dunia na mara nyingine zilikuwa Miaka ya 1954, 1974 na 1990.
Pleased: Bastian Schweinsteiger and Lukas Podolski pose with the World Cup trophy in Berlin
Mbali ya sherehe hizo za Mjini Berlin, Kikosi hicho cha Germany kina Wachezaji wengi kutoka Bayern Munich na Klabu hiyo imeandaa sherehe maalum kwenye Mji wao Munich ili kuwapokea Wachezaji wao wa Kikosi hicho.

 Lahm akicheza pembeni mwa Thomas Mullerambaye kabeba kombe la Dunia  2014 waliloshinda huko Brazil siku ya Jumapili kwa kuwatungua Argentina bao 1-0, akiwa amelibeba mbele ya mamia ya mashabiki huko kwao Ujerumani leo hii.

 Podolski, Per Mertesacker, Mesut Ozil, Ron-Robert Zieler, Jerome Boateng na Sami Khedira
Mamia ya Mashabiki leo asubuhi huko Ujerumani wakiwasubiri Mabingwa wao Dunia


Wachezaji wakishusha mizigo yao

Wakipunga mikono kwa Mashabiki!!! Mesut Ozil, Ron-Robert Zieler, Erik Durm, Mats Hummels na Shkodran Mustafi

 Ozil, Benedikt Hoewedes na Per Mertesacker kwenye gari ya wazi na kombe lao.

waliotembelea blog