Wednesday, July 16, 2014

1951Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
KOCHA wa Simba sc, Mcroatia, Dravko Logarusic ameanza kazi kukinoa kikosi chake kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara katika uwanja wa Chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM).
Loga ameamua kuanza kambi mapema kwa lengo la kurejesha heshima ya Simba iliyopotoea kwa miaka mitatu mfululizo.
Katika mazoezi hayo, wachezaji wa zamani ambao hawapo katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania,  Taifa Stars kinachojiandaa na mechi ya Julai 20 dhidi ya Msumbiji wanahudhuria pamoja na wachezaji wapya.
Mshambiliaji wa zamani wa Supersport United ya Afrika kusini, Dani van Wyk amekuwa akihudhuria mazoezi hayo kama sehemu ya kujaribiwa na Loga kabla ya kufanya maamuzi ya kumsaininisha mkataba.
Mchezaji huyo amekuwa akijitahidi kuonesha uwezo wake, lakini Loga anasema anahitaji muda kumtazama kabla ya kufikia makubaliano.
Mlinda mlango bora wa ligi kuu soka Tanzania bara msimu uliopita, Hussein Sharrif `Iker Casillas` amesharipoti kuanza mazoezi na Simba baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili akitokea Kagera Sugar.
Wachezaji wengine wapya walioanza mazoezi ni pamoja na Michael Mgimwa kutoka Thailand, Mohammed Hussein maarufu kama Tshabalala kutoka kwa `wanankulukumbi`, Kagera Sugar.
1
Wakati Simba wakiendelea na mazoezi hayo, nao watani wao wa jadi, Yanga sc wanaendelea kunoa makali katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola chini ya kocha mkuu, Mbrazil Marcio Maximo akisaidiwa na Leonardo Neiva.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog