Wednesday, July 16, 2014


Straika wa Atletico Madrid Diego Costa amekamilisha Uhamisho wake kwenda Chelsea na kusaini Mkataba wa Miaka Mitano.
Inaaminika Dau la Uhamisho la Straika huyo Mzaliwa wa Brazil lakini anachezea Spain ni Pauni Milioni 32.
Costa anakuwa Mchezaji wa 3 kuchukuliwa na Chelsea kwa ajili ya Msimu mpya na wengine ni Cesc Fabregas na Mario Pasalic.

Msimu uliopita akiwa na Atletico Madrid, Diego Costa alipachika Bao 36 katika Mechi 52 na kuisaidia Klabu yake kutwaa Ubingwa wa La Liga na kufika Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI waliyodundwa 4-1 na Real Madrid.
Costa

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog