Friday, September 30, 2016



Jamaa wakilangua kadi za selcom kwa ajili ya mchezo wa Simba na Yanga nje ya Uwanja wa Taifa leo



Hapa anarudisha pesa kwa watu baada ya wandishi wa habari kukisanua na kusaidiwa na askari mmoja wa JWTZ ambaye akutaka kupigwa picha wala kutaja jina lake.


Saturday, September 24, 2016



Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akikatiza katika Mtaa wa Hamugembe mjini Bukoba alipokwenda kuwafariji waathirika wa tetemeko la ardhi liliua watu 17 na kujeruhi wengine 252 hivi karibuni. Picha na Phinias Bashaya

Bukoba.
Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa amewasili mjini Bukoba mkoani Kagera kuwafariji waathirika wa tetemeko la ardhi lililoukumba mkoa huo na kuua watu 17 na kujeruhi wengine 253.

Baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bukoba, Lowassa alilakiwa na mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare na kwenda moja kwa moja katika mitaa ya Hamugembe na Kashai kuwasalimia wananchi.

Akizungumza na wananchi hao, amesema amekwenda kuwafariji na kuwaunga mkono na kwamba anataka haki itendeke kwa waathirika hao. Lowassa aliyeambatana na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na kada wa chama hicho, Khamis Mgeja amesema atawasilisha msaada aliokwenda nao kwa mkuu wa mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu, Salum Kijuu.MWANANCHI


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama samaki aina ya pweza wakati alipotembelea kiwanda cha samaki cha TANIPESCA eneo la Kilindoni wilayani Mfia Septemba 24, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Mhandisi Methew Mtigumwe akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey D.J Mwanri (Kulia)
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Mhandisi Methew Mtigumwe akisoma Risala wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru
Baadhi ya wakuu wa Wilaya za mkoa wa Tabora wakiulaki mwenge wa Uhuru mara baada ya kuwasili Mkoani humo.

Kipa wa Timu ya Maji Maji ya Songea "Wana Lizombe", Amani Simba akiruka bila mafanikio wakati akijaribu kuudaka mpira uliopigwa kwa umaridadi mkubwa na Mshambuliaji wa Simba, Jamal Mnyate na kuiandikia timu hiyo bao la kuongoza, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeweza kuibuka kidedea kwa kuicharaza timu ya Maji Maji mabao 4-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya Maji Maji, Enyima Darlington akiruka sambamba na Beki wa Simba kuwania mpira wa juu katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeweza kuibuka kidedea kwa kuicharaza timu ya Maji Maji mabao 4-0.
 Mshambuliaji machachari wa Timu ya Simba, Laudit Mavugo akiondoka na mpira baada ya kumtoka Beki wa Maji Maji, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeweza kuibuka kidedea kwa kuicharaza timu ya Maji Maji mabao 4-0.
 Mshambuliaji wa Timu ya Maji Maji, Enyima Darlington akitoa pasi nzuri ya kichwa kwa Mchezaji Mwenzake, Alex Kondo, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeweza kuibuka kidedea kwa kuicharaza timu ya Maji Maji mabao 4-0.
 Ibrahim Ajib wa Simba akimpiga chenda maridadi, Luhanga Mapunda wa Maji Maji, katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa jioni hii katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Simba imeweza kuibuka kidedea kwa kuicharaza timu ya Maji Maji mabao 4-0.



Mwenyekiti wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club), Mhe. William Ngeleja akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam leo kuhusu mechi kati ya wabunge ambao ni wapenzi wa timu ya Simba na wapenzi wa timu ya Yanga yenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wahanga wa Tetemeko la Ardhi, lililoukumba Mkoa wa Kagera hivi karibuni. Mchezo huo utafanyika kesho kwenye Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es salaam. Kabla ya Mchezo huo, kutakuwa na michezo ya Utangulizi ambapo Timu ya Bunge ya Mchezo wa Pete (Netball) inakutana na Timu ya TBC huku Mchezo mwingine ukiwa ni ni kati ya Wasanii wa Bongo Movie na Bongo Fleva. Mh. Ngeleja amewataka Watanzania kutoka maeneo yote nchini kujitokeza kwa wingi ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwasaidia wahanga wa Tetemeko la Ardhi Mkoani Kagera.
Mkurugenzi wa Michezo wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Alex Nkeyenge akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam leo kuhusu mechi kati ya wabunge ambao ni wapenzi wa timu ya Simba na wapenzi wa timu ya Yanga yenye lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia wahanga wa Tetemeko la Ardhi, lililoukumba Mkoa wa Kagera hivi karibuni. Nkeyenge amewataka wale wote watakaojitokeza kwenda kuangalia mchezo huo, wanatakiwa kuwa na tiketi za Kielekroniki ambazo zitaanza kutumika rasmi kuanzia hiyo kesho, Pia amezungumzia hali ya usalama katika Uwanja huo kuwa itaimarishwa vizuri kwani Jeshi la Polisi limejipanga vyema kuhakikisha hatuna tukio lolote la uvunjifu wa amani litakalojitokeza uwanjani hapo.
Mwenyekiti wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club), Mhe. William Ngeleja akionyesha moja ya vikombe vitakavyokabidhiwa kwa timu zitakazoshinda katika michezo hiyo ya kesho.
Mwenyekiti wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club), Mhe. William Ngeleja akipokea mfano wa Hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 10, kutoka kwa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mwananchi Communication LTD, Francis Nanai ikiwa ni sehemu ya Mchango wao katika kufanikisha zoezi hilo.
Mwenyekiti wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club), Mhe. William Ngeleja akipokea mfano wa Hundi yenye thamani ya shilingi Milioni tano, kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Tathmini ya Uhai Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Baraka Maduhu ikiwa ni sehemu ya Mchango wao katika kufanikisha zoezi hilo.
Mwenyekiti wa Timu ya Bunge (Bunge Sports Club), Mhe. William Ngeleja akipokea mfano wa Hundi yenye thamani ya shilingi Milioni tano, kutoka kwa mwakilishi wa Kampuni ya Jubilee Insurance.
Mwenyekiti wa Bunge, Mh. Mussa Azzan Zungu akitoa shukrani kwa niaba ya Bunge kwa wale wote waliojitoa kufanikisha zoezi hilo.
WAKATI tiketi za elekroniki zitaanza kujaribio welo, Makampuni mbali mbali wamechangia jumla ya Sh milioni 20 kwa ajili ya kudhamini mchezo wa wabunge mashabiki wa Yanga na wale wa Simba utakaofanyika leo kwenye uwanja wa Taifa ambapo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi.

Makampuni hayo ni Mwananchi Communication iliyotoa Sh milioni 20, mfuko wa bima ya afya NHIF na Jubilee Insurance ambazo zote zimetoa Sh milioni 5 kila mmoja.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo, Mwenyekiti wa Klabu ya Michezo ya Bunge William Ngeleja ambaye pia ni mnazi wa Simba alisema matokeo ya mchezo wa kesho ni hishara ya matokeo ya mchezo wa Oktoba Mosi.

Nae Meneja Miradi wa Kampuni ya Selcom ambayo ndiyo iliyopewa jukumu la kusimamia mfumo huo, Gallus Runyeta amesema kadi  hizo zitatolewa bure katika mchezo wa leo ikiwa ni  majaribio na kuangalia dosari ambazo zitajitokeza kabla ya kuanza kuzitumia rasmi. 

Akizungumzia jinsi ya kuitumia kadi hiyo, Runyeta alisema “Utajisajili kwa kupiga *150*50# halafu ni lazima uiwekee pesa kwa Airtel au M-Pesa. Kiwango cha chini cha kuongeza salio ni Sh 1,000….: “ “Unaweza ukanunua mechi moja kwa kuandika tarehe na mchezo husika au ukachagua baadhi ya mechi au ukanunua mechi zote za msimu za timu unayoipenda.
“Unapokwenda kuingia uwanjani, utaweka kadi yako kwenye alama husika na mlango utafunguka wenyewe. Ukishaangalia mechi uliyoinunua, hauwezi kesho yake ukaenda kutazama mechi nyingine ambayo hujailipia. Kadi itasoma kwenye mechi zilizolipiwa tu. Ukiingia uwanjani hauwezi ukatoka halafu ukarudi kwa tiketi ileile. 

Viingilio vya mchezo huo utakuwa ni shilingi 3000 kwa mzunguko kijani na bluu, 10000 na 15000  kwa  viti vya machungwa, VIP A 200,000, VIP B 100,000 na VIP C ni 50,000 huku kutakuwa na viti 50 vilivyotengwa ambapo kwa yoyote atakayekaa hapo atalipia 1,000,000.

Katika mchezo huo mbali na wabunge pia kutakuwa na mechi ya bongo movie na bongo fleva ambapo kikosi cha bongo movie kitaongozwa na King Majuto, Dr Cheni, Check Budi, Muhogo Mchungu na Ray Kigosi wakati kwa upande wa Bongo Fleva kitaongozwa na Rich One, Kalla Pina, Ally Kiba, Stamina, KR Muller na H baba.

Baada ya upembuzi Msajili wa Vyama vya siasa Jaji Mutungi alitoa mwongozo kuwa Prof. Lipumba bado ni mwenyekiti halali wa chama hicho aidha baadhi ya viongozi na wanachama waliokuwa wamesimamishwa na wengine kufukuzwa, Jaji mutungi amesema ni wanachama halali.
Baada ya tamko hilo la Jaji Mutungi Leo September 24 2016, baadhi ya wanachama wamemsindikiza Prof. Lipumba mpaka makao makuu ya chama hicho yaliyopo buguruni jijini Dar es salaam kwa ajili ya kumkabidhi ofisi kama mwenyekiti wa halali wa chama hicho.
Baada ya wanachama kufika eneo zilipo ofisi hizo geti lilikuwa limefungwa na walinzi hivyo iliwabidi kuruka ili kulifungua kwa ndani na baada ya kuingia ofisini Prof Lipumba ameyazungumza haya.

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk Beatrice Byalugaba kufanya uchunguzi na kubaini madaktari wa hospitali ya wilaya ya Mafia wanaomiliki maduka ya dawa nje ya hospitali hiyo na kuwachukulia hatua.

Amesema ameshangazwa kukuta maduka ya dawa yanayomilikiwa na madaktari nje ya hospitali hiyo kwani tayari Serikali ilishaagiza kuondolewa kwa maduka ya madaktari karibu na hospitali wanazofanyia kazi.

Waziri mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Septemba 24, 2016) wakati alipotembelea hospitali ya wilaya ya Mafia katika siku ya pili ya ziara yake wilayani mafia. 

Kuhusu tatizo la upungufu wa dawa hospitalini hapo amemuagiza Dk. Beatrice kufanya utafiti wa aina ya magonjwa yanayowasumbua wananchi wa wilaya hiyo ili wanapoagiza waagize dawa nyingi za kutibu magonjwa hayo.Pia aliwataka watumishi wa hospitali hiyo wajitahidi kuwahudumia vizuri wagonjwa licha ya uchache wao. Lengo ni kuhakikisha wanapunguza malalamiko kutoka kwa wananchi.

Wakati huo huo Waziri Mkuu amewahamasisha wananchi kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili waweze kuwa na uhakika wa kupatiwa matibabu bure kwa kipindi cha mwaka mzima.

Awali Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Dk. Joseph Mziba alisema mwamko wa wananchi kujiunga na mfuko wa CHF ni mdogo jambo linalokwamisha upatikanaji wa huduma za afya wilayani Mafia. Jumla ya wananchi waliojiunga na CHF ni  watu 6,000 kati ya watu 50,000.



Kwa upande wake Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo Bw. Eric Mapunda ameiomba Serikali kutoa kibali kwa halmashauri kununua dawa ambazo zinakosekana MSD kwenye soko moja kwa moja bila ya kupitia utaratibu wa manunuzi.

"Kuna wakati tunakosa dawa MSD na kulazimika kununua kwa mawakala kwa kufuata taratibu ya manunuzi. Tunalazimika kununua boksi moja la ambapo boksi moja la panadol linauzwa sh. 20,000 na tukinunua moja kwa moja sokoni bila ya kufuata utaratibu huo boksi hilo hilo tunalipata kwa sh. 8,000,”alisema


Baadhi ya wananchi waliokuwepo hospitalini hapo walieleza malalamiko yao kuhusu lugha chafu na dharau inayotolewa na baadhi ya madaktari na wauguzi.
                                                                              

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

JUMAMOSI, SEPTEMBA 24, 2016
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Spika wa Bunge Job Ndugai, wakati Spika alipofika kumsalimia, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. Kushoto ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka. (Picha na Bashir Nkoromo).

waliotembelea blog