Tuesday, December 6, 2016



Msanii wa Bongofleva Darassa ambaye kwa sasa anafanya vizuri na hit single ya wimbo wake mpya unaoitwa ‘Muziki’ ameamua kuweka wazi mtazamo wake kuhusu ile video iliyosambaa ikionesha vijana wakicheza wimbo wake  huku dereva akiacha  gari likienda.

Vijana hao wamekamatwa na polisi na Darassa ameamua kutoa mawazo yake kuhusiana na kitendo hicho ambacho kimewafanya vijana hao kukamatwa na polisi Itigi Singida, Darassa ametuamia account yake ya instagram kuandika ujumbe kuoneshwa kuguswa na

“Hawa ndugu zetu nimepata taarifa wamekamatwa kwa kosa la kutaka kusababisha ajali na unaweza kuona Kama mchezo ulielekea kubaya, ingeweza kua Tatizo kwao Au kumu sababishia mwingine, Naskia watakua mahakamani Leo I’m not so sure naendelea kufatilia”

“Nawaombea Tatizo hili Mungu awafanyie wepesi I’m sure wamejifunza Hawawezi kufanya tena mistake Kama Hii itokee, mizuka feelings mtu anaweza kufanya kitu njee ya mipango yake sometimes, Mungu awasaidie 🙏🏽 LENGO NI KUJENGA DUNIA KUA SEHEMU NZURI NA SALAMA KUISHI #Muziki“


Lucas Pérez (8', na dakika ya 16')



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema ndoto ya mama mmoja kitanda kimoja itatimia endapo ujenzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto inayojengwa Chanika kwa ushirikiano wa Shirika la Maendeleo la Korea Kusini na Mkoa wa Dar es Salaam utakamilika.

Makonda alisema ujenzi wa hospitali hiyo ni muda mwafaka kwa wanawake na watoto kuwa na uhakika wa kupata huduma ya afya.

Alisema hospitali hiyo inayojengwa itahudumia watu 1000 wa nje huku vitanda katika hospitali hiyo ni 160 kwa ajili ya akina mama na watoto.

Aidha alisema wananchi waendelelee kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli ya ulipaji kodi ili nchi iwe na uwezo hata kusaidia nchi nyingine kama wanavyofanya wa Korea.

Makonda alisema madaktari watakao kwenda katika hospitali hiyo watakuwa na makazi humo ili kuondoa usumbufu wa kusafiri kila siku.

Alisema serikali inawapenda wananchi wake kuhakikisha wanapata huduma ya afya bora hususani wanawake na watoto.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati mwenye miiwani) akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Mama na Mtoto ya Chanika leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mradi ujenzi huo, Bing Hunan leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akitembelea ujenzi wa hospitali hiyo leo jijini Dar es Salaam.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.


k1
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akizungumza na wamiliki wa Bloggers Tanzania kabla ya kufunga mafunzo kwa mablooger hao yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
k2
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu akifafanua jambo kwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakati wa ufungaji wa wa mafunzo kwa mablooger Tanzania yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
k3
Mwenyekiti wa Muda wa Tanzania Bloggers network Bw. Joachim Mushi akizungumza na wamiliki wa Bloggers Tanzania kabla ya kumkaribisha Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye kufunga mafunzo kwa Bloggers Tanzania yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
k4
k5 k6 k7 k8
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiwakabidhi baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo kadi za uwanachama za mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSPF katika hafla ya ufungaji wa mafunzo kwa Bloggers Tanzania yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
k9 k10 k11
Baadhi ya wamiuliki wa Bloggers Tanzania wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye wakati wa ufungaji wa mafunzo kwa Bloggers Tanzania yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.




Baada ya kufariki uwanjani kwa mshambuliaji wa timu ya Mbao FC Ismail Khalfan siku ya Jumapili ya December 4, leo December 6 2016 imetoka ripoti ya kilichosababisha kifo cha mchezaji huyo wakati wa mchezo kati ya Mbao FC dhidi ya Mwadui FC.

Ripoti iliyotolewa na hospitali ya mkoa wa Kagera kuhusiana na kifo cha mchezaji huyo, kupitia kwa jeshi la Polisi, Ismail alifariki uwanjani kutokana na kumpata tatizo la kusimama ghafla kwa moyo (sudden Cardiac Arrest-SCA).

Kamishina Msaidizi wa Kagera, Augustin Ollomi ametoa taarifa baada ya uchunguzi wa madaktari kuhusu kifo cha mchezaji huyo ambaye hakuwa na jeraha lolote walibaini kusimama ghafla kwa moyo (sudden cardiac arrest) kulisababisha kifo

SUDDEN CARDIAC ARREST-SCA
Kwa faida yako msomaji:
Kawaida moyo una mfumo wa umeme (heart electrical system), ambao unadhibiti mapigo ya moyo, mfumo huu ukisimama basi moyo unashindwa kusukuma damu sehemu muhimu kama ubongo na ogani kuu.

Moyo ukisimama bila kurudi katika hali yake unasababisha kifo ndani ya sekunde chache na njia pekee ya msaada ni kupita electrical shock ili kushtua mfumo wa umeme wa moyo, na hii inapaswa kufanyika ndani ya sekunde chache mno.
CHANZO: salehjembe


Rais wa Tanzania John Magufuli ametangaza kwamba taifa hilo litanunua ndege zaidi katika juhudi za kufufua shirika la ndege la taifa hilo.

Amesema serikali yake imedhamiria kununua ndege nne zikiwemo ndege kubwa tatu ambazo zitasaidia kuinua "uchumi wa nchi kwa kuwezesha watalii kuja hapa nchini moja kwa moja kutoka nchi zao."

Dkt Magufuli alisema hayo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Masoko ya Afrika wa Kampuni ya utengenezaji wa ndege ya Boeing yenye makao yake nchini Marekani, Jim Deboo katika ikulu jijini Dar es Salaam.
Amesema Tanzania inapanga kununua ndege aina ya Boeing 787 Dash 8 Dreamliner yenye uwezo wa kuchukua abiria 262 ambayo inatarajiwa kuwasili nchini humo Juni 2018.

Ndege nyingine ambazo Tanzania itazinunua ni ndege moja aina Bombardier Q400 Dash 8 NextGen inayotarajiwa kuwasili Mwezi Juni 2017, ndege 2 aina ya Bombardier CS300 zenye uwezo wa kuchukua kati ya abiria 137 na 150 na zinazotarajiwa kuwasili nchini kati ya Mei na Juni, 2018.

Malipo ya awali kwa ndege hizi yameshafanyika.
"Tumeleta ndege aina ya Bombardier hapa, zimepunguza gharama za safari mfano kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, sasa wanalipa kati ya 160,000/ hadi 200,000/- wakati nauli ilishafika Shilingi laki 8 na kitu, lakini watu wengine utakuta wanazungumzazungumza wee maneno ya hovyo kwa kutumiwa, tumeshaamua na tutafanya hivyo" amesema Rais Magufuli.

"Sisi hapa tunazungumza kuwa watalii hawajafika hata milioni 2 kwa mwaka, lakini nchi kama Morocco inapata watalii zaidi ya milioni 12 kwa mwaka, hii yote ni kwa sababu hatuna mashirika ya ndege ya kwetu."

"Kwa hiyo niwaombe tu Watanzania wapende mali zao, kwa sababu wakati mwingine nikiangalia mitandao na magazeti ni ajabu huwezi kuamini kama hao ni Watanzania, unakuta wanasifia tu ndege za watu wengine na wanazibeza za kwao."

waliotembelea blog