Wednesday, April 8, 2015

obin van Persie yupo FIT kwa derby  dhidi ya majirani zao Man city
  • Mshambuliaji Robin van persie amepona kabisa kwa mchezo wa jumapili
  • Alikosekana tangu tarehe 21 mwezi wa pili
  • Si rahisi kwa van Persie kuanza kikosi cha kwanza dhidi ya city.
van p
Na Anwar binde,
Robin van Persie amejitangaza kuwa yupo vizuri kwa mchezo wa jumapili dhidi ya wapinzani wao wa jadi Manchester city.
Van Persie amekosekana michezo sita ya Manchester united kutokana na kuumia enka wakati man utd walipooteza kwa 2-1 dhidi ya Swansea tarehe 21 mwezi wa pili.
Kocha Louis van Gaal wiki iliyopita alisema hakutegemea van Persie kupona kwa haraka hivyo na kua vizuri kupambana na city jumapili ijayo pale Old Traffod,lakini Van Persie mwenyewe alijitangaza kwa mashabiki na kuwaambia yupo vizuri.
Hata kama van Gaal akifikiria kumpa nafasi katika mechi yao ya upinzani wa jadi dhidi ya city bado ni ngumu sana kuona jinsi gani ataendana na kasi na mfumo wa sasa ya kitika kikosi cha kwanza
Pengo la mholanzi ambae amefunga magoli 10 tu msimu huu halikuonekana kabisa pale alipoumia,na tangu alipoumia man united imepoteza mchezo mmoja tu tena dhidi ya mabosi wake wa zamani Arsenal kombe la FA.

United walipata ushindi katika ratiba ngumu dhidi ya Tottenham na Liverpool na jumamosi iliyopita ushindi wa 3-1 dhidi ya Aston Villa ushindi uliofanya kuwa juu ya city kwa pointi moja.

Wyne Rooney alifunga goli moja matata kwa mkwaju wa haja,kapteni huyo wa united amekua na kiwango bora kabisa pale mbele katika mfumo wa 4-3-3 akisaidiana na Ashley Young na Juan Mata ambae aliingia nyavuni mara mbili katika ushindi wa 2-1 pale Anfield wiki mbili na nusu zilizopita.
Marouane Fellaini pia anatoa mchango mkubwa katika majukumu ya kiungo na ushambuliaji sehemu ambayo kwa sasa imetulia sana kwenye kikosi hicho cha Manchester united.
Ushindi dhidi ya city iliyopoteza mwelekeo na kuwa chini ya kiwango utaongeza wigo wa pointi kufikia nne na kuongeza matumaini ya Van Gaal kucheza ligi ya mabingwa msimu ujao.

Philippe Coutinho akishangilia bao lake dakika ya 71 huko Ugenini Ewood Park Kipindi cha pili dakika ya 71 Philippe Coutinho aliwafungia bao la kuongoza Liverpool kwa kufanya 1-0 dhidi ya Blackburn Rovers.Mapumziko hakuna Timu iliyoliona lango la mwenzake, Si Blackburn Rovers wala Liverpool.Raheem Sterring kaanza kipindi cha kwanza katika kipute hiki cha marudiano kati ya Blackburn Rovers vs Liverpool.

    MSANII EMMA BOY TOKEA KAHAMA   TZ
UMEFANYIKA CHINI YA PRODUCEI MR T TOUCHEZ STUDIO FREE NATION SOUND


MUDA mfupi uliopita kumefanyika mkutano wa waandishi wa habari na uongozi wa African Stars wana Twanga Pepeta. Mkutano huo uliofanyika Nemax Hotel, Kinondoni, Dar es Salaam, mwanamuziki wa siku nyingi aliyekuwa akiendesha bendi yake ya Extra Bongo ametangaza kuwa anarudi kwenye bendi yake ya zamani ya African Stars maarufu kwa Twanga Pepeta. Pamoja na Ally Chocky waliokuweko katika mkutano huo ni Mkurugenzi wa Twanga Bi Asha Baraka, kiongozi wa bendi Luiza Mbutu, na mcheza shoo mkongwe Nyamwela ambaye pia ndie Mwenyekiti wa chama cha wacheza show Tanzania. Onyesho la kwanza la Chocky katika bendi hiyo litakuwa tarehe 18 mwezi huu wanne, japo ukumbi utakuwa upi haijatajwa lakini Chocky alisema kuwa tayari ana tungo tatu atakazoanza nanzo nazo ni Usiyaogope maisha, Kichwa chini, na No discussion.


Aslay Isihaka maarufu kwa jina la ‘Dogo Aslay’ na  Bakari Abdul katuti ‘Beka’ wakiimba Moja ya Wimbo wao kwenye Ukumbi wa "Rest House" ukumbi wa Jeshi  Wilayani Biharamulo Mkoa wa Kagera kwenye Shoo yao iliyoweza kushuhudiwa na Mashabiki  wengi wa Muziki huo wa Bongo Flava katika Ukumbi huo Biharamulo. Shoo hiyo ilifanyika Usiku wa tarehe 07.04.2015 katika Siku maalum ya Hitma ya kumkumbuka Hayati, Muasisi wa Mapinduzi Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume ambayo ilipewa jina la "Karume Day".
Nyimbo kibao ikiwemo NITAJUTA, NISEME, WAMBEA, NITAKUPWELEPWETA ziliimbwa katika Ukumbi huo wa Rest House ambao ni Ukumbi wa Jeshi katika Mji huo.
Yamoto Band unakuwa umegusa majina ya Vijana Machachari wanne ambao ni Waimbaji wenye Sauti Tamu na Vipaji vya hali ya juu  kutoka Mikoa tofauti hapa Nchini Tanzania. Kundi hilo ambalo lilianza kuunguruma katika Mji wa Mwanza, Geita, Bukoba Mjini na pia kumalizia Burudani zake hapa Wilayani Biharamulo Mkoani Kagera na Vinaja hao kufanya vyema katika Miji hiyo.

Aslay na mwenzake wakiwajibika vilivyo jukwaani
Kundi hilo linaundwa na Aslay Isihaka maarufu kwa jina la ‘Dogo Aslay’, Mbwana Yusuph Kilungi ‘Maromboso’, Enock Deogratius ‘Enock Bella’ pamoja na Bakari Abdul katuti ‘Beka’.
Hakika ilikuwa Burudani
Nyomi ya kutosha usiku huo

‘Dogo Aslay’, Mbwana Yusuph Kilungi ‘Maromboso’ wakiwajibika Jukwaani

Maromboso akifanya yake kwa Mashabiki wao
Jerry kwenye picha akitokelezea na mashabiki
Kiongozi Mnec (kulia) Bw. Yusuph A. Khatry akiwa na Mama
Sunday(kulia) katikati ni Jonathan Mwanga --Waandaaji wa Shoo hiyo wakiwa na Rafiki yao kikazi Bw. Willy Kiroyera ambaye walikutana nae usiku huo wa shoo akitokea Nchi jirani ya Rwanda mjini Bujumbura kwenye shughuli za kitalii.


Wadau..wakifuatilia Muziki huo kwa makini..

Willy O. Rutta akipeana neno na Mtangazaji wa Radio Kasibante Fm Bw. Abdulrazak Majid(kulia) wakati wa Shoo hiyo ya Yamoto Band Biharamulo.



Wadau

Machote yote kwa Waimbaji wa Kundi la Yamoto Band.

Nani zaidi!!




Mashabiki wakiyarudi mangoma ya Live kutoka kwa Yamoto Band

Shabiki wa Yamoto Band nae akijinafasi mbele ya Mashabiki wenzake
Mambo ya Yamoto Band



Hatari sana! Burudani ikiendelea..
Bw. Jonathan Mwanga akipata ukodak na Shabiki wake Biharamulo usiku huu.

Dada moja wa waimbaji Chipukizi wa Said Fella Getrude akiwajibika jukwaani kwa kufokafoka Rap
Baadhi ya Mashabiki waliohudhuria katika shoo ya bendi ya YAMOTO  katika ukumbi wa Rest House jana usiku wakionekana kumkubali Dada huyo mkali wa Kurap .
Chiba akifanya yake huku akiwa kasimama kwa mguu mmoja  pekee
Kipaji ni kipaji

Waimbaji wanaounda kundi la “Yamoto Band”Aslay, Becka, Bella na Maromboso wakitoa burudani sambamba na Kijana wao mwenye mguu mmoja Chiba"



waliotembelea blog