Tuesday, August 11, 2015



sterling 5
Winga wa Manchester City, Raheem Sterling ambaye amejiunga na timu hiyo baada ya kununuliwa toka Liverpool ameonekana kuanza kuwavutia mashabiki wa klabu yake mpya baada ya kitendo chake cha kugawa jezi kwa shabiki mdogo baada ya mchezo wake wa kwanza kwenye ligi kuu ya England.
Sterling ambaye alinunuliwa katika dili la paundi milioni 49 alivua jezi yake baada ya mchezo dhidi ya Westbromwich Albion na kwenda moja kwa moja jukwaani ambapo aliikabidhi jezi hiyo kwa shabiki mmoja ambaye alionekana kufurahia kitendo hicho.
Sterling akiruka uzio kwenda kutoa jezi kwa shabiki wa Man City.
Sterling akiruka uzio kwenda kutoa jezi kwa shabiki wa Man City.
Sterling alifanya kitendo hicho kwenye mchezo ambao Man City ilishinda kwa matokeo ya 3-0 matokeo ambayo yamewafanya waongoze ligi katika wiki yake ya kwanza huku mabingwa watetezi wa ligi hiyo Chelsea wakibanwa mbavu.
Sterling alivua jezi yake na kwenda kuigawa kwa shabiki wa Man City.
Sterling na jezi yake mkononi akiipeleka kwa shabiki wa Man City.
Shabiki aliyepewa jezi na Raheem Sterling akionyesha furaha yake.
Shabiki aliyepewa jezi na Raheem Sterling akiionesha huku akifurahia.
sterling 6



Pedro
Huku Manchester United wakionekana kujiandaa kutangaza usajili wa kiungo mshambuliaji Pedro Rodriguez, mahasimu wao toka Jijini Manchester, Man City wameingilia kati usajili huo na kutishia nafasi ya United.
City kupitia kwa mkurugenzi wake mtendaji Txiki Bergistan wanajiandaa kupeleka ofa ya euro milioni 30 kwa ajili ya mchezaji huyo ambapo inaelezwa kuwa ofa yao inazidi ofa ya United kwa euro milioni 4 ambapo United wametoa ofa  ya euro milioni 26.
United kwa siku za hivi karibuni wamekuwa wakitajwa kuwa karibu kumsajili mchezaji huyu ambaye ni dhahiri hana nafasi ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza cha Barcelona na ameweka wazi azma yake ya kutaka kuondoka.
Pedro Rodriguez Wallpapers Barcelona6
Pedro Rodriguez, Winga Mshambuliaji wa Barca kwa sasa ambaye Man City na Man United zinamuwinda.
Manchester City wanaonekana kutumia faida ya ukaribu ulioko kati ya  wakurugenzi wake wawili Txiki Bergistan na Feran Soriano na klabu ya Barcelona ambapo wawili hao waliwahi kufanya kufanya kazi kwa miaka mingi kwenye klabu hii ya huko Catalunya.
Hata hivyo bado ofa ya Manchester City haijawasilishwa rasmi kwa Barcelona na hadi sasa mazungumzo rasmi ambayo yamefanyika ni kati ya Barca na United na inaweza kufikia hatua ya mchezaji mwenyewe kuchagua mahali anakotaka kwenda.


WWW.BUKOBASPORTS.COM Shindano la kuibua na Kusaka Vipaji vya Kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT) ambalo limedumu kwa takribani Miezi Minne hatimaye shindano hilo linakaribia kufika tamati mnamo tarehe 22 August 2015 huku Mshindi Mmoja Akiondoka Na Kitita Cha Shilingi Milioni Hamsini Za Kitanzania.

Na Washiriki waliofanikiwa kuingia Hatua ya Kumi bora watapata kifuta jasho huku wakiwa na mkataba mnono wa kufanya kazi na Kampuni namba moja ya Kutengeneza na Kusambaza filamu za Kitanzania ambao pia ndio waratibu wa Shindano Hilo la Tanzania Movie Talents (TMT) ya Proin Promotions Ltd.

Shindano la TMT lilianza mapema mwezi wa Nne kwa kutafuta vipaji katika Kanda ya Ziwa ambapo usaili ulifanyika Mkoani Mwanza na kuhitimishwa Kanda ya Pwani Mkoani Dar Es Salaam kwa kupatikana Jumla ya Washindi 20 kutoka Kanda sita za Tanzania
Washindi wa kanda sita walipata fursa ya kuingia ndani ya mjengo wa TMT huku wakipatiwa mafunzo ya sanaa kutoka kwa Walimu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam huku mchujo ukiendelea na kupelekea kila wiki Washiriki wawili kuaga shindano, takribani wiki tano jumla ya washiriki 10 waliweza kuaga shindano hili ambalo limefikia hatua ya kuwapata washiriki 10 waliofanikiwa kuingia hatua ya Kumi bora huku wakingojea fainali itakayotoa mshindi wa kitita cha shilingi milioni hamsini za kitanzania
Mpaka sasa washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya Kumi bora wanaendelea na kujifua Kwaajili ya fainali ambayo imebaki wiki moja tu kwa fainali hiyo kuliteka jiji la Dar huku hofu na presha zikiwapata Washiriki hao.
Fainali ya TMT itafanyika Siku ya Jumamosi ya tarehe 22 August 2015 katika ukumbi wa makumbusho ya taifa karibu na Chuo cha IFM kwa viingilio vya shilingi Elfu 50 kwa VIP na Elfu 30 kwa viti vya kawaida.
TMT 2015 inapigwa tafu na Precious Air, Cam gas, ITV na Radio One, Global Publishers, I-View Studio, Paisha na Hussein Pamba Kali



Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za tume ya Taifa ya Uchaguzi kkugombea nafasi hiyo, kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, mwaka huu.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mkurugenzi wa tume ya Taifa ya Uchaguzi, Kailima Ramadhan Kombwey, baada ya kukabidhiwa fomu za tume hiyo za kugombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Agosti 10, 2015. Kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF na Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif.
MGOMBEA wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa amechukua fomu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ya kuwania nafasi hiyo leo Jumatatu Agosti 10, 2015.

Msafara wa Mgombea huyo ulioanzia kwenye Ofisi za Chama cha Wananchi CUF Buguruni na kuishia kwenye Ofisi za CHADEMA Kinondoni Jijini Dar es salaam na kupelekea msongamano mkubwa wa watu ambao wengi wao ni wafuasi wakuu wa vyama vinavyounda UKAWA, na kufanya shughuli mbali mbali kusimama kwa muda wa takribani saa saba.

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Maafisa wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wakati alipofika kuchukua Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25, mwaka huu.


Umati wa watu wakiwemo wafuasi wa vyama vya Siasa vinavyounda UKAWA ukiwa Umefurika kwa wingi kwenye Barabara ya Uhuru, Jijini Dar es salaam kumsindikiza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mwenza wake, Dkt. Juma Haji Duni, walipokuwa wakielekea Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25, mwaka huu. PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mwenza wake, Dkt. Juma Haji Duni wakiwapingua maelfu ya wafuasi wa vyama vya Siasa vinavyounda UKAWA, jijini Dar es salaam, Augusti 10, 2015, walipokuwa wakielekea Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25, mwaka huu.

Mh. Lowassa na Mh. Duni wakiwapungia maelfu ya wafuasi wa vyama vya Siasa vinavyounda UKAWA nje ya Makao Makuu ya Chama cha CUF, Buguruni jijini Dar.









Sehemu ya Wapenzi wa vyama vinavyounda UKAWA wakiushangilia Msafara wa MGOMBEA wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa wakati akielekea Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25, mwaka huu.


Buhuruni Rozana.

MGOMBEA wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akisalimiana na
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF na Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif mara baada ya kuwasili kwenye Makao Makuu ya Chama cha CUF, Buguruni Jijini Dar es salaam.

MGOMBEA wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mwenyekiti wa Chama hicho, Mh. Freeman Mbowe, huku Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF na Mgombea Urais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif akishuhudia.








Mh. Freeman Mbowe, Mh. Tundu Lissu na Mh. James Mbatia wakiwa kwenye magari yao wakati wakimsindikiza Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa na Mgombea Mwenza wake, Dkt. Juma Haji Duni, walipokuwa wakielekea Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuchukua Fomu ya kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Octoba 25, mwaka huu.



Barabara ya Uhuru, Jijini Dar.





Soma Zaidi Hapa »

waliotembelea blog