Sunday, February 23, 2014

Kocha David Moyes alivyokuwa anaonekana kabla ya mtanange kuanza!!
Mabingwa Watetezi wa England, Manchester United, walishinda Bao 2-0 na kujikongoja Nafasi moja juu na sasa kukamata Nafasi ya 6.
Hadi Mapumziko Mabao yalikuwa 0-0.
Kipindi cha Pili, katika Dakika ya 62, Robin van Persie aliipatia Man United Bao la Kwanza kwa Penati iliyotolewa na Refa Michael Oliver baada Patrice Evra kuangushwa ndani ya Boksi na Marouanne Chamakh.
Bao la Pili lilifungwa Dakika ya 68 kifundi na Wayne Rooney baada ya kupokea pasi safi toka kwa Evra.
Mechi inayofuata kwa Man United ni huko Ugiriki hapo Jumanne Usiku watakapocheza na Olympiacos katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONS.
Van Persie akishangilia...
Wakati Rooney anataka kupiga kona alirushiwa shilingi na hapa akimpatia Mwamuzi wa mchezo huoR


Rasmi: Rooney amethibitisha kusaini kwake Mkataba mpya United kwa kuandika kwenye ukurasa wake wa Facebook akisema 'furaha sana'
Na Mahmoud Zubeiry
MSHAMBULIAJI Wayne Rooney amemshukuru kocha David Moyes jana usiku baada ya kujihakikishia mustakabali wake katika klabu ya Manchester United, kufuatia kusaini Mkataba mpya wa miaka mitano ambao utamfanya apate mshahara wa Pauni 300,000 kwa wiki.
Rooney aliwaambia United alitaka kuondoka mwishoni mwa msimu uliopita baada ya kutofautiana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Sir Alex Ferguson na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England walilazimika kupambana na ofa ya dau la Pauni Milioni 30 kutoka Chelsea.

Sorted: Rooney (centre) with executive vice chairman Ed Woodward and manager David Moyes
Wa hapa hapa: Rooney (katikati) akiwa na Makamu Mwenyekiti wa klabu, Ed Woodward na kocha David Moyes jana baada ya kusaini Mkataba mpya
Moyes alisema jana namna ambavyo alimshawishi mshambuliaji huyo wa kimataifa wa England kubaki Old Trafforf alipokutana naye katika kikao chake cha siri kilichofanyika Juni mwaka jana.
MALIPO MAPYA YA ROONEY
Pauni 15,600,000 kwa mwaka
Pauni 300,000 kwa wiki
Pauni 43,000 kwa siku
Pauni 1,800 kwa saa
Pauni 30 kwa dakika
50p kwa sekunde
Na Rooney ametoa shukrani zake kwa kocha wake huyo aliyemuibua Everton baada ya kusaini Mkataba ambao utamalizika Juni mwaka 2019 ambao unamfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani.
Alisema: "Kulikuwa kuna tetesi kibao wakati wa majira ya joto, lakini nilitulia wakati David Moyes alipokuja kwenye klabu.
"Nimekuwa na uhusiano mzuri naye na anaonyesha imani kubwa kwangu. Mazungumzo yamekuwa yakiendelea kwa muda mrefu – Nina furaha kusaini sasa.
"Hii ni moja ya klabu kubwa duniani na fahamu kwamba nitacheza hapa kwa sehemu kubwa ya maisha yangu ya soka, ni kitu ambacho nasonga mbele kwa ajili hiyo. Nina furaha kwamba kila kitu sasa kimemalizwa na ninaweza kuelekeza fikra zangu kwenye soka yangu,"alisema. 

waliotembelea blog