Tuesday, December 8, 2015


Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi ni tuzo ambayo Ligi nyingi duniani huwa wanayo hata katika Ligi Kuu soka Tanzania bara huwa ipo, December 8 ndio siku ambayo Ligi Kuu Hispania ilitangaza tuzo ya mchezaji bora wa mwezi, Neymar anayekipiga katika klabu ya FC Barcelona ndio mchezaji aliyefanikiwa kutwaa tuzo hiyo kwa mwezi November.
Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi ya Neymar inaingia katika rekodi za staa huyo, kwani stori kutoka fcbarcelona.com zinaeleza kuwa Neymar ameweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa FC Barcelona kuwahi kutwaa tuzo hiyo, rekodi ya Neymar sio tu ya kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya kwanza kwa upande wake ila ni mchezaji wa kwanza wa FC Barcelona kuwahi kutwaa tuzo hiyo rekodi ambayo haiwezi kuvunjwa.
hi-res-d2eea00c88e563ae6491c4ad75d141f5_crop_exact
Tuzo hiyo ya mchezaji bora wa mwezi ya Laliga imeanza kutolewa toka msimu wa 2013/2014, hivyo huu ni msimu wake wa tatu toka ianze kutolewa na imetolewa mara 21 hadi sasa, kwa maana hiyo Neymar ambaye ana magoli 14 katika msimamo wa wafungaji wa Ligi Kuu Hispania, ameweka rekodi ambayo haiwezi kuvunjwa kamwe na mchezaji wa FC Barcelona kwani hata mchezaji mwingine wa FC Barcelona akishinda tuzo hiyo Neymar ataendelea kuwa na rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa FC Barcelona kushinda tuzo hiyo.

Raheem Sterling alifunga bao mbili na kutengeneza mabao mengine Manchester City walipoichabanga bao 4 kwa 2 Borussia Monchengladbach_ 4-2 na kukaa kileleni kwenye Group D.Raheem Sterling akishangilia moja ya bao lake
Kolarov kwenye patashika baada ya kutupwa nje ya Uwanja na kuangukia kwa waandishi wa HabariHatari tupu!!!Chupuchupu!! Borussia Monchengladbach nao wakishangilia bao lao moja wapo
Silva akishangilia bao lake la kwanzaKikosi cha Man City


Manchester United imefungwa 3-2 na Wolfsburg Bao 3-2 kwenye Mechi ya Kundi B la UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL na kutupwa nje na sasa kucheza Raundi ya Mtoano ya EUROPA LIGI.3-2Kipigo hicho, na ushindi wa PSV Eindhoven wa Bao 2-1 dhidi ya CSKA Moscow, kumezifanya Wolfsburg na PSV kufuzu kwenda Raundi ya Mtoano ya UCL na Man united kumaliza Nafasi ya 3.
Hii ni mara ya kwanza kabisa kwa Wolfsburg kucheza Raundi ya Mtoano ya UCL. 
Naldo akipeta...
Huko Santiago Bernabeu, Cristiano Ronaldo alifunga Bao 4, Karim Benzema kupiga 3 na moja la Mateo Kovacic na kuwapa ushindi Real wa Bao 8-0 toka Kundi A.
Real, na PSG, ambao wameshinda 2-0 walipocheza na Shakhtar Donetsk zote zimesonga na Shakhtar itakwenda EUROPA LIGI.

Man City, ambao walikuwa washafuzu toka Kundi D, Leo wameichapa Borussia Mönchengladbach 4-2 na kumaliza kileleni mwa Kundi hilo na kufuatiwa na Juventus ambao Leo walifungwa 1-0 na Sevilla ambao wamemaliza Nafasi ya 3 na hivyo kwenda EUROPA LIGI.
Van Gaal akipagawa baada ya kutupwa njeNaldo ndiye aliyepeleka kilio baada ya kufunga bao la tatu kwa WolfsburgNaldo akitupia kwa kichwa mpira wa konaAkitupia bao la piliMata akishangilia baoMan United wakipongezana...Akishangilia bao1-1Raha ya kufunga bao!Kikosi cha Man United Van Gaal Mwenyekiti!Sir Alex Ferguson Sir BobbyMapema kabla ya Mechi walipokuwa wanapasha


DROO ya Raundi ya 3 ya Kombe kongwe Duniani, FA CUP, ambalo sasa linaitwa Emirates FA Cup kwa sababu za kiudhamini, imefanyika Usiku huu ikihusisha Timu zote za Ligi Kuu England na Daraja la Championship ambazo huanzia hapa.
Droo hii, ambayo imeibua Mechi 5 za Timu za Ligi Kuu England kuvaana wenyewe kwa wenyewe, imefanyika huko Sport Wales National Centre Mjini Cardiff, na kuhusisha Timu 64 na Mechi zake zitachezwa kati ya Ijumaa Januari 8 na Jumatatu Januari 11.

Arsenal, ambao ndio Mabingwa Watetezi baada ya kulitwaa Kombe hili kwa mara ya pili mfululizo Mwezi Mei Mwaka huu, watakuwa kwao Emirates kucheza na Sunderland wakati Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, Chelsea, wapo kwao Stamford Bridge kucheza na Mshindi kati ya Timu za Madaraja ya chini Leyton Orient v Scunthorpe United.
Manchester United wapo kwao Old Trafford kucheza na Sheffield United wakati Man City wako Ugenini kucheza na Norwich City.
Liverpool wako Ugenini kuivaa Exeter City huku Mechi tamu iko White Hart Lane ambako Tottenhma watavaa Vinara wa Ligi Kuu England Leicester City. 

Droo ya Raundi ya Tatu:
Watford v Newcastle
West Brom v Bristol City
West Ham v Wolves
Salford/Hartlepool v Derby
Exeter City v Liverpool
Northampton Town v MK Dons
Peterborough v Preston
Colchester v Charlton
Tottenham v Leicester
Arsenal v Sunderland
Ipswich Town v Portsmouth
Newport County v Blackburn Rovers
Sheffield Wednesday v Fulham
Wycombe Wanderers v Aston Villa
Birmingham City v AFC Bournemouth
Oxford United v Swansea City
Brentford v Chesterfield or Walsall
Bury v Bradford City
Manchester United v Sheffield United
Everton v Dagenham and Redbridge/Whitehawk
Southampton v Crystal Palace
Carlisle United v Yeovil Town
Nottingham Forest v QPR
Eastleigh v Bolton Wanderers
Chelsea v Leyton Orient/Scunthorpe United


MENEJA wa Manchester United Louis van Gaal Leo amesafiri kwenda Germany na Wachezaji 19 kwa ajili ya Mechi yao ya mwisho ya Kundi B la UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL, ambayo itaamua kama watasonga Raundi ya Mtoano au watatupwa EUROPA LIGI.
Man United hawawezi kutupwa nje kabisa ya Ulaya kwani matokeo ya aina yeyote ama yatwabakisha UCL au kupelekwa EUROPA LIGI wakimaliza katika Nafasi ya 3 ya Kundi B.
Katika Kikosi hicho cha Wachezaji 19 hayupo Kepteni Wayne Rooney na Kiungo Morgan Schneiderlin ambao ni Majeruhi na wanaungana na Majeruhi wengine Marcos Rojo, Ander Herrera, Phil Jones, Luke Shaw na Antonio Valencia.

UEFA CHAMPIONS LIGI
KUNDI: B:

PSV Eindhoven (Pointi 7) v CSKA Moskva (4)
Wolfsburg (9) v Manchester United (8)
-Wolfsburg watafuzu wakipata Sare na watachukua Nafasi ya Kwanza wakishinda.
-Man United watasonga wakishinda na kuwa Washindi wa Kundi.
-PSV watafuzu wakishinda au wakidroo ikiwa Man United itafungwa
-CSKA watatwaa Nafasi ya 3 wakiifunga PSV.
Miongoni mwa Kikosi hicho wapo Chipukizi kadhaa akiwemo Paddy McNair ambae alitolewa Haftaimu kwenye Droo na West Ham Majuzi na nafasi yake kuchukuliwa na Chipukizi wa Uruguay Guillermo Varela ambae nae yupo safarini.

Chipukizi wengine Kikosini ni Nick Powell, ambae muda mrefu hajajumuika katika Kikosi cha Kwanza na pia wapo Kiungo Sean Goss na Beki Cameron Borthwick-Jackson.

Kikosi kamili: David De Gea, Sergio Romero; Paddy McNair, Chris Smalling, Guillermo Varela, Cameron Borthwick-Jackson, Daley Blind, Matteo Darmian; Bastian Schweinsteiger, Michael Carrick, Sean Goss, Nick Powell, Ashley Young, Jesse Lingard, Andreas Pereira, Juan Mata; Memphis Depay, Marouane Fellaini, Anthony Martial.

Memphis Depay kwenye mazoezi huko Volkswagen Arena akijiweka tayari kupambana leo hii usku kwenye hatua ya mwisho

Van Gaal akiwacheki Vijana wake kwenye mazoezi kujiweka sawa dhidi ya Wolfsburg 


Mechi pekee ya Ligi Kuu England huko Goodison Park, Merseyside, Jijini Liverpool, Wenyeji Everton walijinasua toka kwenye kipigo na kutoka Sare ya 1-1 na Crystal Palace.
Bao za Mechi hii zilifungwa na Scott Dann Dakika ya 76 kwa Palace na Romelu Lukaku kurudisha Dakika ya 81.

Kabla ya Lukaku, mwenye Miaka 22, kusawazisha, Everton walipiga Posti mara 3 na hatimaye Lukaku kufunga likiwa ni Bao lake la 50 katika Mechi 100 za Everton.
Matokeo haya yamewaweka Palace Nafasi ya 6, wakiwa na Pointi 23, na Everton wakiwa Nafasi ya 9 wakiwa na Pointi 22 huku Vinara ni Leicester City wenye Pointi 32 baada ya Mechi 15 kwa Timu zote.
Scott Dann akishangilia bao lake Scott Dann akitupia kwa kichwaJason akiendesha mpira huku akinyemelewa na mchezaji wa Everton BrendanYohan Cabaye akituliza kwa uzuri
Meneja wa Everton Martinez Everton v Crystal Palace
Meneja wa Crystal Palace Alan PardewWayne Rooney nae alikuwepo na Mtoto wake KaiArouna akipenya!

waliotembelea blog