Thursday, April 9, 2015


MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho ameusapoti msimamo wa Arsene Wenger kwamba Ballon d'Or ifutiliwe mbali
Mwezi Januari, Wenger, ambae ni Meneja wa Arsenal, aliiponda Tuzo hiyo ya FIFA anaetunukiwa Mchezaji Bora Duniani wa Mwaka na kusisitiza kuwa angepewa nafasi ya kupiga Kura asingekubali.

Hata hivyo, Wenger hana nafasi ya kumpigia Kura Mgombea wa Tuzo hiyo kwa vile Washiriki wake ni Makocha wa Timu za Taifa na Manahodha wake pamoja na Jopo maalum la Wanahabari.
Cristiano Ronaldo, ambae aliwahi kucheza chini ya Mourinho alipokuwa Real Madrid, ndie anaeshikilia Tuzo hiyo kwa sasa baada ya kuitwaa kwa mara ya 3 Mwezi Januari.

Akiongea hapo jana, Mourinho alisema Tuzo hiyo inavuruga Soka kwa kuweka msisitizo kwa Mtu binafsi badala ya Timu.
Mourinho alisema: "Nadhani Wenger alisema kitu cha maana, anapinga Ballon d’Or, na nadhani yuko sahihi kwa sababu kwa sasa Soka linapoteza mvuto wa Kitimu na kutilia mkazo Mtu binafsi!"
Mourinho alinena: "Sasa tunatizama ubinafsi. Fulani na takwimu zake kwamba alikimbia umbali mrefu. Kwa sababu kwenye Gemu umekimbia Kilomita 11 na mie nimekimbia 9 wewe ndio umefanya kazi nzuri? Pengine siyo! Labda Kilomita zangu 9 ni muhimu kuliko zako 11! Kwangu mie Soka ni Kitimu. Mtu binafsi anakaribishwa ikiwa anataka kufanya Timu yetu iwe bora!''
Aliongeza: "Mchezaji mkubwa akiwasili anaikuta Timu ipo. Si yeye anaeigundua Timu kama vile Columbus alivyoivumbua Amerika. Wewe unakuja kutusaidia tuwe bora zaidi. Kama Meneja kila Siku inabidi utoe ujumbe huu!"

FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani kwa Nchi na Mabingwa wa Dunia Germany wameendelea kuwa juu wakifuatiwa na Argentina huku Tanzania ikishuka Nafasi 7 na kushika Nafasi ya 107.
Nchi ya juu kabisa kwa Afrika bado ni Algeria lakini imeporomoka Nafasi 3 na sasa ipo ya 21 ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo pia imeshuka Nafasi 3 na ipo ya 23.
Nchi mpya kwenye 10 Bora ni Switzerland na Spain wakati France na Italy zimetoka huko.

Nayo Belgium imepanda Nafasi 1 na ni wa 3 baada ya kuchukua nafasi ya Colombia huku Brazil wakipanda moja wakiwa Nafasi ya 5.
England nao wanaisogelea 10 Bora baada kupanda Nafasi 3 na kushika Nafasi ya 14.
Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Mei 7

LISTI YA UBORA DUNIANI:
20 BORA:

1. Germany
2. Argentina
3. Belgium
4 Colombia
5. Brazil
6. Netherlands
7. Portugal
8. Uruguay
9. Switzerland
10. Spain
11. France
12. Romania
13. Italy
14. England
15. Costa Rica
16. Chile
17. Croatia
18. Mexico
19. Czech Republic
20. Slovakia


Real Madrid inazidi kuipumulia Barcelona katika mbio za La Liga baada ya kuichapa Rayo Vallecano 2-0 Kwa ushindi huo, Real Madrid inaendelea kutofautishwa kwa pointi kati yake na Barcelona ambayo hapo awali iliifumua Almeria 4-0. Ronaldo akishangilia bao lake la 300Mabao ya Real Madrid yamefungwa na Cristiano Ronaldo aliyetupia katika dakika ya 68 muda mfupi baada ya kulimwa kadi ya njano kwa kujirusha huku bao la pili likifungwa na James Rodriguez dakika ya 74.
DSC_0377 


  DSC_0338 DSC_0379 
  DSC_0387 DSC_0404 
  DSC_0301 DSC_0406 
  DSC_0386 DSC_0368
DSC_0219 


DSC_0226 

DSC_0235
DSC_0274

waliotembelea blog