Thursday, April 9, 2015

FIFA Leo hii imetoa Listi ya Ubora Duniani kwa Nchi na Mabingwa wa Dunia Germany wameendelea kuwa juu wakifuatiwa na Argentina huku Tanzania ikishuka Nafasi 7 na kushika Nafasi ya 107.
Nchi ya juu kabisa kwa Afrika bado ni Algeria lakini imeporomoka Nafasi 3 na sasa ipo ya 21 ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo pia imeshuka Nafasi 3 na ipo ya 23.
Nchi mpya kwenye 10 Bora ni Switzerland na Spain wakati France na Italy zimetoka huko.

Nayo Belgium imepanda Nafasi 1 na ni wa 3 baada ya kuchukua nafasi ya Colombia huku Brazil wakipanda moja wakiwa Nafasi ya 5.
England nao wanaisogelea 10 Bora baada kupanda Nafasi 3 na kushika Nafasi ya 14.
Listi nyingine ya Ubora itatolewa hapo Mei 7

LISTI YA UBORA DUNIANI:
20 BORA:

1. Germany
2. Argentina
3. Belgium
4 Colombia
5. Brazil
6. Netherlands
7. Portugal
8. Uruguay
9. Switzerland
10. Spain
11. France
12. Romania
13. Italy
14. England
15. Costa Rica
16. Chile
17. Croatia
18. Mexico
19. Czech Republic
20. Slovakia

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog