Thursday, August 28, 2014

Screen Shot 2014-08-28 at 8.27.35 AM 
Toka nimeanza kuandika na kufatilia habari sijawahi kusikia jeshi la nchi limechukua hatamu kuendesha mashindano ya urembo tena mashindano yanayokutanisha warembo kutoka sehemu mbalimbali za taifa ili kumtafuta mshindi.
Stori hii ya kipekee inatokea Uganda ambapo jeshi la nchi hiyo limeamua hivyo baada ya kuona ubabaishaji unaofanywa na Waandaaji wa Miss Uganda shindano ambalo halikufanyika kwa miaka kadhaa kutokana na ubabaishaji.
Ripota wa TZA Kampala Bill the African, ameripoti kwamba mmoja kati ya wenye vyeo vyao jeshini ambae pia ni mdogo wake Rais Museven amesema jeshi limeamua kuchukua usimamizi wa mashindano haya kwa madai kwamba ni njia ya kuwavutia vijana wapende kilimo kitakachotangazwa kupitia haya mashindano ikiwa tayari pia jeshi hilo limechukua Wizara ya kilimo kwa ajili ya kuiongoza.
Screen Shot 2014-08-28 at 8.11.06 AM 
Bill alipozunguka mtaani kuwauliza watu maoni yao imekua 30 kwa 70 yani kuna ambao wanaona hakuna shida Wagumu hawa kuongoza mashindano hayo lakini wengine wengi wanapinga wakisema Jeshi hili linajulikana kabisa huwa halicheki na mtu wala halina urafiki na Raia sasa ndio wataweza kuendesha mashindano ya Urembo? ni vitu viwili tofauti kabisa.


frank-lampard-volley
Siku kadhaa baada ya Frank Lampard kutangaza kustaafu soka la kimataifa – jana ilikuwa siku nyingine kwa wanasoka wawili wa kimataifa barani nao walitangaza uamuzi wa kuachana na soka la kimataifa.
140823111329_etoo512
Samuel Eto’o na Xabi Alonso kwa wakati tofauti jana walitumia mitandao ya kijamii kutangaza uamuzi wao wa kuachana na soka la kimataifa.
Alianza Xabi Alonso kupitia mtandao wa Twitter kutangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Spain.
Kiungo huyo wa Real Madrid ameshaitumikia Spain kwa muda wa miaka 11 na ameifungia nchi hiyo magoli 16 katika mechi 114.
Wakati huo huo mfungaji mabao mengi zaidi wa timu ya taifa ya Cameroon Samuel Eto’o ametangaza kustaafu soka la kimataifa.
Mshambuliaji huyo ambaye ameifungia Cameroon mabao 56 amejiunga na Everton ya Uingereza juzi .
Kufuatia kauli hiyo mshambuliaji huyo sasa hatakuwepo katika kipindi chote cha cha kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwezi Januari mwakani.


IMG_6809.JPG

Wiki kadhaa baada ya kuteuliwa kuwa nahodha mpya wa Manchester United, mshambuliaji Wayne Rooney leo amepata uongozi mpya kwenye medani za soka.
Rooney ameteuliwa na kocha Roy Hodgson amemteua mshambuliaji huyo kuwa nahodha mpya wa timu hiyo ya taifa.
Rooney mwenye miaka 28 amechukua mikoba iliyoachwa na kiungo wa Liverpool, Steven Gerrard aliyestaafu.
Rooney aliwahi kuvaa kitambaa cha unahodha akiiongoza England kwenye mechi ya kufuzu kucheza Kombe la Dunia dhidi ya San Marino, Oktoba 2012.

Staa huyo amewapiku wachezaji wenzake kipa Joe Hart na beki Gary Cahill ambao nao walikuwa wakitajwa kuchukua uongozi huo.


DSCN1093
  • Serengeti fiesta Moshi wapewa fursa ya kuonja radha
Mhehimiwa Temba ametangaza rasmi kuachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la “Wazee wa jiji” jumamosi hii. Serengeti fiesta Moshi wamepewa fursa ya kuonja radha ya wimbo huo siku ya Jumamosi katika uwanja Majengo Jijini humo.
Mheshimiwa Temba ambaye ni mzawa wa jiji hilo anatarajia kutumia fura ya Serengeti fiesta Moshi kuuzindua wimbo huo kwa mara ya kwanza.
“Ni matumaini yangu kuwa Wanamoshi wataniunga mkono kwa kujitokeza kwa wingi katika viwanja wa Manjengo siku ya Jumamosi Agosti 30, kushuhudia shoo kali nitakayoifanya sanjari na nyota wengine wa muziki watakaotumbuiza katika tamasha hilo.
Baadhi ya wasanii watakaowasha moto katika jukwaa la Serengeti fiesta Moshi ni pamoja na Ali kiba, Ney waMitego, Dully Sykes, Jambo Squad, Stamina, Maua, Recho, Shaa and Mapacha, Chege na Temba na wengine wengi.
Chege ameishukuru kampuni ya Serebgeti kupitia kinyaji chake mashuhuri, Serengeti Premium Lager, kwa kutoa fursa kwa wasanii kukutana na mashabiki zao na kuwapa burudani. “Burudani la Serengeti fiesta ni moja ya mifano dhahiri inayoonyesha jinsi Watanzania tunavyopendana bila kujali utofauti wa makabila yetu na dini zetu.”
Temba ameyashauri makampuni mengine yanayopatikana ukanda wa Afrika Mashariki na kati kuiga mfano wa Serengeti Fiesta ili kudumisha udugu na ujamaa katika nchi wanazofanya kazi.
Pia ameishauri kampuni ya Serengeti fiesta kuangalia uwezekano wa kulisambaza burudani hili katika nchi nyingine Africa…ikianzia na Afrika ya Mashariki.
“Burudani inanguvu ya kipekee sana katika maisha ya manadamu. Kwa kuisambaza Serengeti fiesta katika nchi nyingine Afrika mashariki kutaifanya jumuia hii kuungana zaidi na kuwa kitu kimoja,” alisema Temba.
Baada ya Mohi, Burudani la Serengeti fiesta litaelekea mikoa mingine kama Musoma, Shinyanga, Kigoma, Tabora, Singida, Dodoma, Moshi, Arusha, Mtwara na baadae jijini Dar es salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi alipowasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi baada ya kuwasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi baada ya kuwasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Wengine ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Balozi wa Burundi nchini Tanzania Mhe Issa Ntambuka.
Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi akisalimiana na Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania Profesa Sospeter Muhongo eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Wasanii wa ngoma ya utamaduni kutoka Burundi wakiburudisha kwenye sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi akisalimiana na baadhi ya Watanzania walikuwepo eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipokea nyimbo za Taifa za nchi zao eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Sehemu ya umati wa wananchi wa Tanzania na Burundi kwenye sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi wa Tanzania na Burundi katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa meza kuu pamoja na Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Naibu Katibu Mkuu Wizara Uchukuzi Dkt Charles Tizeba eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi katika picha ya kumbukumbu na wataalamu wa Tanzania na Burundi eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi kuhudhuria sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakitembelea eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiangalia moja ya alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipata maelezo na kuangalia vifaa vya upimaji eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto kwa Rais Kikwete ni Waziri wa Ardhi na Maendeleo na Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakizindua kwa pamoja eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakipongezana kwa furaha katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014. Kushoto ni Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakichanganjya udongo na kujenga kwa pamoja alama katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi na wananchi wa nchi zao wakisimama wakati nyimbo za Taifa za Burundi na Tanzania zikipigwa katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakijipatia chakula cha mchana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi wakiagana katika eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa


Ethiopia na Kenya zimetangaza niya ya kutaka kuwa wenyeji wa kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwaka wa 2017 baada ya Libya kujiondoa.

Libya ilitangaza kauli hiyo baada ya mapigano kuchacha baina ya makundi mawili hasimu yaliyowanyima waandalizi fursa ya kujenga viwanja vipya vya mashindano hayo.

Ethiopia, ambayo imewahi kuwa mwenyeji wa mashindano hayo katika miaka ya 1962, 1968 na 1976, imesema kuwa itawasilisha rasmi ombi lake mara moja

Rasi wa Shirikisho la soka la Ethiopia Junedin Basha ameiambia BBCMichezo kuwa tayari taifa hilo linaviwanja viwili vyenye hadhi ya kimataifa (Addis Ababa na Bahir Dar), na hivyo hoja kuu itakuwa kukamilisha viwanja viwili vipya ambavyo tayari vinaendelea kujengwa.

"Serikali inaari ya kuyaleta mashindano hayo hapa Ethiopia ."alisema

Kenya kwa upande wake imetangaza niya ya kuandaa mashindano hayo kwa pamoja na Tanzania Uganda au Rwanda.

Shirikisho la soka barani Afrika limetangaza tarehe 30 Septemba kuwa siku ya mwisho ya mataifa kuwasilisha maombi yao.

Tangazo rasmi ya nani atakayeandaa mashindano hayo itakuwa mwakani

Straika wa Arsenal Olivier Giroud atakuwa nje ya Uwanja hadi baada ya Mwaka mpya kufuatia kufanyiwa upasuaji kutibu Mguu wake uliovunjika.
Mfaransa huyo mwenye Miaka 27 aliumia Jumamosi iliyopita huko Goodison Park wakati Arsenal inatoka Sare 2-2 na Everton kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.

Akitangaza habari hizi, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, alisema Giroud atakuwa nje kwa Miezi Mitatu hadi Minne.
Giroud alijiunga na Arsenal Mwaka 2012 kutokea Klabu ya France Montpellier na Msimu uliopita alianza Mechi 36 kati ya 38 za Ligi za Arsenal na kufunga Bao 16.
Licha ya pigo hili, Wenger ametangaza hatanunua Straika mwingine katika Kipindi hiki cha Dirisha la Uhamisho linalofungwa Septemba Mosi.

Arsenal sasa wamebakiwa na Mastraika Joel Campbell, Yaya Sanogo na Lukas Podolski lakini Mchezaji wao mpya, Alexis Sanchez, ambae kiasili ni Winga, huweza kucheza Sentafowadi na Jana Usiku ndie aliefunga Bao lilowapeleka Arsenal Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI wakati walipoipiga Besiktas Bao 1-0.


Alexis Sanchez akishangilia bao lake.Alexis Sanchez aliipachia bao na kufanya 1-0 dhidi ya timu ya Uturuki Besiktas kwenye dakika za majeruhi za kipindi cha kwanza baada ya Jack Wilshere wa Arsenal kufanya jitihada na kumwachia afunge Sanchez aliyekuwa sehemu nzuri na kufunga bao hilo. Arsenal mpira huu hawakuumaliza 11 dakika ya 75 kipindi cha pili mchezaji wao Debuchy alipewa kadi ya njano ya pili na kuondoshwa kwa kadi nyekundu baada ya kufanya ndivyo sivyo.Patashika zikiendelea kipindi cha kwanza..Kimbiza kimbiza kila mchezaji akiunyatia kuupata mpira Jack Wilshere akisikitika baada ya kukosa bao huku akiwa kwenye nafasi nzuri katika dakika za mapema kipindi cha kwanza.Demba Ba (kulia) akiendesha.......Alexis Sanchez kuanza katika mchezo wao kati ya Arsenal vs Besiktas na hii ni baada ya kuumia kwa Olivier Giroud na sasa anarajiwa kuwemo katika mtanange huu wa leo  mchezo wa marudiano wa Champions League unaotarajiwa kupigwa punde usiku huu. Mechi ya kwanza walitoka 0-0 huko Uturuki.Podolski nae yumo...Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger
Kocha Mkuu wa England Roy Hodgson (akiwa nyuma) nae akishuhudia kipute kwenye Uwanja wa Arsenal Emirates.
VIKOSI:
Arsenal:
Szczesny, Debuchy, Mertesacker, Koscielny, Monreal, Wilshere, Flamini, Oxlade-Chamberlain, Ozil, Cazorla, Sanchez.
Akiba: Martinez, Rosicky, Podolski, Chambers, Sanogo, Campbell, Coquelin.
Besiktas: Zengin, Koybasi, Franco, Gulum, Ramon, Hutchinson, Kavlak, Ozyakup, Pektemek, Sahan, Ba.
Akiba: Gonen, Kurtulus, Sivok, Tore, Uysal, Koyunlu, Tosun.
Refa: Pedro Proenca (Portugal)


Samuel Eto'o ametupilia mbali madai kuwa ana bifu na Jose Mourinho wakati timu yake mpya Everton ikijitayarisha kuikabili Klabu yake ya zamani Chelsea hapo Jumamosi.
Eto’o, Mchezaji wa Kimataifa wa Cameroon, na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho walikuwa pamoja huko Inter Milan na kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na akaja England Mwaka mmoja uliopita kuungana na Mourinho huko Chelsea.
Lakini uhusiano wa Eto’o na Mourinho ulipata msukosuko pale Mreno huyo aliponaswa kwenye Kamera bila kujijua akidhihaki Umri wa Eto’o na kudai ni Mzee kupita Miaka inayodaiwa anayo.
Mara baada ya tukio hilo Eto’o, mwenye Miaka 33, alifunga Bao akiichezea Chelsea na kwenda kushangilia mithili ya Mzee akishika Kibendera cha Kona kama Mkongojo huku akijishika Kiuno ili kumdhihaki Mourinho.
Akiongea na Wanahabari mara tu baada ya kutambulishwa kama Mchezaji mpya, Eto’o alipuuza madai hayo ya kuwa na bifu na Mourinho na badala yake kusema anamshukuru Mourinho kwa kumleta Ligi Kuu England.
Nae Meneja wa Everton Roberto Martinez amedokeza kuwa huenda Mkongwe huyo wa Cameroon akaivaa Chelsea Jumamosi wakati watakapopambana Goodison Park katika Mechi ya Ligi Kuu England.

Crystal Palace imemteua Bosi wao wa zamani Neil Warnock kama Meneja wao mpya.
Warnock, mwenye Miaka 65 na ambae alikuwa Palace kati ya Mwaka 2007 na 2010, amesaini Mkataba wa Miaka Miwili.
Mkongwe huyo mwenye makeke na vituko anachukuwa wadhifa kutoka kwa Tony Pulis ambae alibwaga manyanga Masaa 48 tu kabla Msimu mpya wa Ligi Kuu England kuanza hapo Agosti 16.
Msimu uliopita, Tony Pulis, aliteuliwa kuwa Meneja wa Msimu wa Ligi Kuu England baada ya kuiongoza Palace kutoka mkiani wakati akishika wadhifa huo kutoka kwa Ian Holloway Mwezi Novemba 2013 na kumaliza Ligi ikiwa Nafasi ya 11.
Warnock amekuwa hana kazi tangu Aprili 2013 alipoachana na Klabu ya Leeds United.

Kurudi kwa Warnock kumeleta mvuto hasa kufuatia tukio la Winga wa Klabu hiyo, Jason Puncheon, kupandwa ghadhabu na kubatuka kwenye Mtandao wa Twitter akimponda Warnock ambae, wakati akiwa Mchambuzi kwenye TV, alimkosoa Puncheon kwa kukosa Penati na tukio la Puncheon kutoa maneno makali kwenye Twitter liliifanya FA imtwange Mchezaji huyo Faini ya Pauni 15,000.

Mwaka 2010, Warnock aliondoka Palace baada ya Klabu hiyo kuwekwa chini ya Mwangalizi maalum ili kuepuka kufilisiwa, kitendo ambacho kiliifanya Klabu hiyo ikatwe Pointi 10 na kuiweka kwenye hali ngumu na nusura ishushwe kutoka Daraja la Championship.

Choices: Co-chairman Steve Parish has been looking for a new manager since Tony Pulis left earlier this month
Mwenyekti msaidizi Steve Parish alikuwa akitafuta Kocha mpya tangu Tony Pulis atimke zake Klabuni hapo.
Manager: Neil Warnock previously managed Crystal Palace between 2007-10, but left to join QPR
Neil Warnock pia alishaiongoza Crystal Palacekati ya mwaka 2007-10, lakini pia alioongoza QPR

waliotembelea blog