Thursday, August 28, 2014


DSCN1093
  • Serengeti fiesta Moshi wapewa fursa ya kuonja radha
Mhehimiwa Temba ametangaza rasmi kuachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la “Wazee wa jiji” jumamosi hii. Serengeti fiesta Moshi wamepewa fursa ya kuonja radha ya wimbo huo siku ya Jumamosi katika uwanja Majengo Jijini humo.
Mheshimiwa Temba ambaye ni mzawa wa jiji hilo anatarajia kutumia fura ya Serengeti fiesta Moshi kuuzindua wimbo huo kwa mara ya kwanza.
“Ni matumaini yangu kuwa Wanamoshi wataniunga mkono kwa kujitokeza kwa wingi katika viwanja wa Manjengo siku ya Jumamosi Agosti 30, kushuhudia shoo kali nitakayoifanya sanjari na nyota wengine wa muziki watakaotumbuiza katika tamasha hilo.
Baadhi ya wasanii watakaowasha moto katika jukwaa la Serengeti fiesta Moshi ni pamoja na Ali kiba, Ney waMitego, Dully Sykes, Jambo Squad, Stamina, Maua, Recho, Shaa and Mapacha, Chege na Temba na wengine wengi.
Chege ameishukuru kampuni ya Serebgeti kupitia kinyaji chake mashuhuri, Serengeti Premium Lager, kwa kutoa fursa kwa wasanii kukutana na mashabiki zao na kuwapa burudani. “Burudani la Serengeti fiesta ni moja ya mifano dhahiri inayoonyesha jinsi Watanzania tunavyopendana bila kujali utofauti wa makabila yetu na dini zetu.”
Temba ameyashauri makampuni mengine yanayopatikana ukanda wa Afrika Mashariki na kati kuiga mfano wa Serengeti Fiesta ili kudumisha udugu na ujamaa katika nchi wanazofanya kazi.
Pia ameishauri kampuni ya Serengeti fiesta kuangalia uwezekano wa kulisambaza burudani hili katika nchi nyingine Africa…ikianzia na Afrika ya Mashariki.
“Burudani inanguvu ya kipekee sana katika maisha ya manadamu. Kwa kuisambaza Serengeti fiesta katika nchi nyingine Afrika mashariki kutaifanya jumuia hii kuungana zaidi na kuwa kitu kimoja,” alisema Temba.
Baada ya Mohi, Burudani la Serengeti fiesta litaelekea mikoa mingine kama Musoma, Shinyanga, Kigoma, Tabora, Singida, Dodoma, Moshi, Arusha, Mtwara na baadae jijini Dar es salaam.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog