Wednesday, August 19, 2015


air1
Najua kuna watu wangu wanaopenda kufanya matembezi sehemu mbalimbali duniani iwe kwa issue zao binafsi au hata kwa issue za kibiashara. Lakini ulishawahi kujiuliza ni viwanja gani vya ndege vyenye mvuto zaidi duniani? na Africa viko vingapi?
Nimekutana na stori kwenye mitandao ambao wenyewe wamefanya utafiti na kuja na orodha ya viwanja 10 vya ndege vyenye mvuto wa kipekee kwa mwaka huu wa 2015 haswa ukiwa bado uko angani unakaribia kutua.
air2
Kwenye list upo uwanja wa Queenstown Airport uliyopo New Zealand,  uwanja wa McCarran Airport uliopo Las Vegas na uwanja wa Nice Cote D’Azur Airport uliopo Ufaransa. Na kwa Africa upo uwanja wa…!?
Hapa chini nimekusogezea picha 10 za viwanja vya ndege vyenye mvuto zaidi duniani, unaweza kuvitazama kujua uwanja gani wa ndege kutoka Africa umeingia.
new zealand
1. Queenstown Airport, New Zealand.
las vegas
2. Las Vegas McCarran Airport, United States.
france
3. Nice Cote D’Azur Airport, France.
Barra Airport, Traigh Mhor Beach, Isle of Barra, Outer Hebrides. PIC: P.TOMKINS / VisitScotland /SCOTTISH VIEWPOINT Tel: +44 (0) 131 622 7174   Fax: +44 (0) 131 622 7175 E-Mail : info@scottishviewpoint.com This photograph can not be used without prior permission from Scottish Viewpoint.
4. Barra Airport, Scotland, UK.
maarten
5. St. Maarten Airport (Princess Juliana International), Caribbean.
carebean island
6. Saba Airport (Juancho E Yrausquin), Caribbean Netherlands.
toronto
7. Billy Bishop Toronto City Airport, Canada.
british island
8. Gibraltar Airport, UK.
london
9. London City Airport, UK.
SA
10. Cape Town Airport, South Africa.
Unaambiwa uwanja namba 3 uliingia kwenye hii orodha mwaka 2014, uwanja namba 4 ulikuepo pia kwenye hii orodha mwaka 2013 na uwanja namba 5 ulikuwepo pia kwenye orodha ya viwanja vizuri zaidi duniani mwaka 2012 na hii ni mara ya pili kwa wao kuingia kwenye orodha hii.

Leo kwenye zile Stori za 255 amesikika Fid Q kuhusu akaunti yake iliyotekwa,,anasema anashukuru akaunti yake kurudishwa, aliyehusika amesikitishwa na alichokifanya, anasema baada ya kugundua amemkosea alisikitika na kuomba msamaha kwa kile kilichotokea..tayari alianza mikakati ya kumfungulia kesi lakini kabla ya kufanya hivyo alipata ujumbe kutoka kwa msichana huyo akiomba samahani kwa kilichotokea.
fii
Fid Q
Zaidi ya miei mitatu iliyopita Mo music alizungumzia biashara yake ya kuuza dagaa na Senene lakini imeonekana kuyumba kidogo, mwenyewe amezungumza na kusema ameegemea zaidi kwenye biashara ya kuuza unga wa sembe akishirikiana na baba yake.
mooo
Mo music
Nay wa Mitego amesema kitendo chake ya kutumia damu na masamu ya kishetani katika video zake amesema hata yeye hajui ni kwanini anatumia lakini amekua anapenda, anajikuta ana idea ya kutumia vitu hivyo..pia ni kama utambulisho wake..anapenda vitu vya kitofauti ambavyo wengi hawatarajii kama anaweza kufanya.
NY
Nay wa Mitego
Mshambuliaji  wa kimataifa wa Italia mwenye asili ya Ghana anayeichezea klabu ya Liverpool ya Uingereza Mario Balotelli ambaye amezoeleka kuingia katika headlines mbalimbali kuhusiana na tabia yake ya ukorofi na vituko vyake safari kaingia tena katika headlines ila sio kwa ukorofi au utukukutu.

Hii ni good news kwa mashabiki watoto wa mshambuliaji huyo kwani amekuja na Brand ya viatu vya mpira wa miguu na mipira, vifaa hivyo vitakuwa vinapatikana kwa ajili ya watoto, huku vikiwa vinastahili ya kipekee tofauti na tulivyozoea.
balo_ball_3411075b
Brand hiyo ya vifaa vya michezo ya Balotelli imetengenezwa na kampuni maarufu ya Kijerumani kwa utengenezaji wa vifaa vya michezo PUMA, vifaa hivyo vinastahili kama ya manyoya au nywele kama ambavyo Balotelli amekuwa akinyoa stahili ya kiduku katika kichwani kwake.


balo_boots_3411072b

3-1 Fellaini akishangilia bao lake la dakika za nyongeza Old Trafford!Pongezi!Marouane Fellaini alitokea Benchi dakika ya 84 akichukua nafasi ya Nahodha wa Man United Wayne Rooney dakika ya 90 kwenye muda wa nyongeza aliipa Man United bao la tatu na kufanya Man unitedkuibuka na Ushindi wa bao 3-1 leo kwenye mechi ya Kwanza ya Klabu Bingwa Ulaya hatua ya Makundi. Club Brugge hawajawahi kushinda England katika Mechi zao 11, wakifungwa 9, na tangu waifunge Chelsea 1-0 kwenye Robo Fainali ya UEFA CUP ya Msimu wa 1994/5 hawajashinda Mechi yeyote katika 6 walizocheza na Timu za England.Depay akipongezwa baada ya kuipatia bao mbili Man United.
Dakika ya 79 Club Brugge wanapata pengo baada ya mwenzao Mechele kucheza rafu tena na kuoneshwa kadi nyekundu na kubaki 10 Uwanjani.Timu hizi zitarudiana Wiki ijayo Jumatano Agosti 26 huko Belgium na Mshindi kutinga hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.Depay akishangilia bao lake2-1Carrick alipoteza machungu ya kujifunga hapa!Mpaka nyavuni!Chicharito kauanza msimu mpya leo hii...alichukuwa nafasi ya Januzaj kipindi cha piliDakika ya 43 Memphis Depay aliwapachikia tena bao la pili Man United na kufanya bao kuwa 2-1 dhidi ya Club Brugge na mtanange kwenda mapumziko United ikiwa mbele.Rooney akipambana Rooney tena"Rooney hatari kabisa!Wachezaji wawili wa Club Brugge wakipongezana baada ya kupata bao la zawadi dakika ya 8 kupitia kwa Carrick.Wachezaji wa Man United wakijiuliza baada ya kutanguliwa bao na wapinzani wao Club bruggeSalaam! 1-0Carrick alipojimaliza!Dakika ya 13 Depay anaisawazishia Man United baada ya kuwakaanga mabeki ndani ya 18 na kumfunga kipa wa Club Brugge Bruzzese.
Michael Carrick anajinga bao dakika ya 8 baada ya kupigwa mpira wa adhabu na kuutengua na kumwamisha kipa na mpira kujaa kambani..Sir Alex Ferguson Ndani Old TraffordKikosi cha Man United kilichoanza dhidi ya Club BruggeDepay kacheza kwa kiwango cha juu na kuipa bao mbili Man United


Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajiwa kuondoka nchini siku ya jumamosi usiku kuelekea Muscat Oman, kucheza mchezo wa kirafiki kabla ya kuunganisha kuelekea Istanbul Uturuki kwa kambi ya wiki moja.
Taifa Stars imepata mwaliko wa kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Oman tarehe 24 Agosti, 2015 usiku, ambapo baada ya mchezo huo timu itasafiri kuelekea nchini Uturuki katika jiji la Istambul.
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Oman (OFA) liliomba kucheza mchezo wa kirafiki na Taifa Star kabla ya kuwavaa Turkemekistan katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia Septemba 03, 2015 kwa bara la Asia, ambapo kocha wake mkuu Mfaransa Paul Leguen aliomba kucheza na vijana wa Charles Mkwasa kujiandaa na mechi hiyo.
Mara baada ya mchezo huo Taifa Stars itaelekea Istambul katika mji wa Kocael hoteli ya Kartepe kwa kambi ya wiki moja, ikiwa nchini Uturuki Stars inatarajiwa kucheza michezo miwili ya kirafiki kabla ya kurejea nchini kucheza na Nigeria Septemba 05, 2015 mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika.
Kocha mkuu wa Taifa Stars, Charles Mkwasa anatarajiwa kutoa orodha ya kikosi chake cha wachezaji 22 mwishono mwa wiki watakaosafiri kuelekea nchini Uturuki kwa kambi ya hiyo ya kujiandaa na mchezo dhidi ya Nigeria.

Mshambuliaji Adi Yussuf anayechezea klabu ya Mansfield Towny ya Uingereza alitarajiwa kujiunga na timu nchini Uturuki, lakini kutokana na majeruhi aliyoyapata hivi karibuni katika michezo ya ligi, uongozi wa Mansfield umeomba mchezaji huyo kutojiunga na timu ya Taifa kwa ajili ya kupata mataibabu zaidi.

Adi aliumia wiki iliyopita katika mchezo dhidi ya Nottingham Forest ambapo kwa sasa anaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa klabu hiyo, na pindi atapokuwa fit atapata nafasi ya kujumuika na kuitumika timu ya Taifa ya Tanzania.


Mabingwa wa Super Cup 2015 Athletico Bilbao baada ya wakuchapa Mabingwa Barca bao 5-1 usiku huu.Pique hoi!! akijificha uso! Gerard Piqué laomeshwa kadi nyekundu kipindi cha pili dakika ya 56.Lionel Messi alifunga bao dakika ya 43 kipindi cha kwanza na kufanya 1-0(Agg 1-4) dhidi ya Athletico Bilbao.

Aritz Aduriz dakika ya 74 aliwasawazishia bao Bilbao na kufanya 1-1 na kufanya (Agg. kuwa 1-5)

waliotembelea blog