Monday, August 4, 2014


Kocha mpya wa Uholanzi Guus Hiddink amemteua Pierre van Hooijdonk kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya nchi hiyo. 
Pia Hiddink amemwambia nahodha wa timu hiyo Robin van Persie kupatana na Pierre van Hooijdonk ambaye waligombana wakati wa fainali za kombe la dunia, wakati Pierre van Hooijdonk aliposema Van Persie hafai kucheza kwenye mchezo wa mshindi wa 3 kutokana na kutokuwa na kiwango kinachostahili.





Mheshimiwa Zitto Kabwe - "#TaifaStars imecheza mechi nyingi ambazo nimehudhuria, ndani na nje ya nchi. Sijaona wachezaji wakitokwa machozi kama Jana. Ndani ya chumba cha kubadilisha nguo niliona uchungu na machozi ya vijana wetu. Kwa pamoja walikuwa wanasema 'nyumbani kama ugenini, ugenini ugenini'. Somo kubwa sana hilo."



MABINGWA wa Ulaya, Real Madrid wamemsajili mlinda mlango na shujaa wa Costa Rica katika fainali za kombe la dunia majira ya kiangazi mwaka huu nchini Brazil, Keylor Navas.
Navas amekubali kusaini mkataba wa miaka sita na sasa anaingia katika ushindani na kipa Iker Casillas kwasababu kuna dalili kuwa kipa mwingine Diego Lopez anasepa zake.
View image on Twitter
Taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao rasmi wa klabu ya Real Madrid jana jioni inasomeka: "Real Madrid CF na Levante UD zimefikia makubaliano juu ya uhamisho wa Keylor Navas, ambaye atajifunga klabuni kwa misimu sita ijayo""Mchezaji atatambulishwa jumanne, Agosti 5, saa 7:00 mchana (saa za Hispania) kwenye uwanja wa Bernabeu, baada ya kuchukuliwa vipimo vya afya".


All smiles: Ashley Young joins team-mates Wayne Rooney and Danny Welbeck for Manchester United training
Tabasamu 'bab kubwa': Ashley Young akiungana na wachezaji wenzake Wayne Rooney na Danny Welbeck kwenye mazoezi ya Manchester United.
LOUIS van Gaal atawachana macho kwa macho wachezaji wake ambao wataachwa na Manchester United baada ya kumaliza ziara ya Marekani ambapo amewapa nafasi ya kumuonesha viwango vyao.

Anderson, Nani, Javier Hernandez, Shinji Kagawa na Marouane Fellaini ni miongoni mwa majina makubwa yaliyopo katika mstari mwekundu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.
Lakini inafahamika kuwa Van Gaal  hatakuwa na huruma kabisa ingawa hajafanya maamuzi ya hadharani.
'Nitafikia maamuzi baada ya ziara hii,' alisema. Nimewapa nafasi ya kucheza wachezaji wote na najua zaidi hata kabla ya ziara.
Plenty to ponder: Louis van Gaal will tell his unwanted players that they are free to find another club
Louis van Gaal atawaambia wachezaji asiowahitaji kuwa wapo tayari kutafuta timu nyingine.

'Kwa sasa nimefikia maamuzi kidogo, lakini kwenye mpira wa miguu lazima uamue. Unatakiwa kuwapa nafasi wachezaji kufanya usajili pale unapoona hawana nafasi ya kucheza kwenye kikosi chako.
'Unatakiwa kusema mapema kwasababu ni mbali sana baada ya Agosti 31. Nitawaambia wachezaji baada ya ziara hii, lakini nitawaambia wao na sio ninyi.'
Van Gaal aliyasema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Miami jana kuelekea mechi ya fainali ya leo usiku ya kombe la kimataifa nchini Marekani dhidi ya mahasimu wao wakubwa England, klabu ya Liverpool.

waliotembelea blog