Monday, August 4, 2014


All smiles: Ashley Young joins team-mates Wayne Rooney and Danny Welbeck for Manchester United training
Tabasamu 'bab kubwa': Ashley Young akiungana na wachezaji wenzake Wayne Rooney na Danny Welbeck kwenye mazoezi ya Manchester United.
LOUIS van Gaal atawachana macho kwa macho wachezaji wake ambao wataachwa na Manchester United baada ya kumaliza ziara ya Marekani ambapo amewapa nafasi ya kumuonesha viwango vyao.

Anderson, Nani, Javier Hernandez, Shinji Kagawa na Marouane Fellaini ni miongoni mwa majina makubwa yaliyopo katika mstari mwekundu kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.
Lakini inafahamika kuwa Van Gaal  hatakuwa na huruma kabisa ingawa hajafanya maamuzi ya hadharani.
'Nitafikia maamuzi baada ya ziara hii,' alisema. Nimewapa nafasi ya kucheza wachezaji wote na najua zaidi hata kabla ya ziara.
Plenty to ponder: Louis van Gaal will tell his unwanted players that they are free to find another club
Louis van Gaal atawaambia wachezaji asiowahitaji kuwa wapo tayari kutafuta timu nyingine.

'Kwa sasa nimefikia maamuzi kidogo, lakini kwenye mpira wa miguu lazima uamue. Unatakiwa kuwapa nafasi wachezaji kufanya usajili pale unapoona hawana nafasi ya kucheza kwenye kikosi chako.
'Unatakiwa kusema mapema kwasababu ni mbali sana baada ya Agosti 31. Nitawaambia wachezaji baada ya ziara hii, lakini nitawaambia wao na sio ninyi.'
Van Gaal aliyasema hayo wakati akiongea na waandishi wa habari mjini Miami jana kuelekea mechi ya fainali ya leo usiku ya kombe la kimataifa nchini Marekani dhidi ya mahasimu wao wakubwa England, klabu ya Liverpool.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog