Monday, June 29, 2015


WENYEJI Chile wametinga fainali ya Copa America 2015 kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Peru usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Taifa mjini Santiago:
Kwa ushindi huo, fainali Chile sasa itakutana na mshindi kati ya Argentina na Paraguay zinazomenyana usiku wa kuamkia kesho.
Eduardo Vargas aliifungia bao la kwanza akimalizia krosi ya Alexis Sanchez dakika ya 42.
Carlos Zambrano alitolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Charles Aranguiz.
Bao la kujifunga la Gary Medel dakika ya 60 liliwapa matumaini wageni, kabla ya Vargas kuifungia la ushidi Chile dakika ya 64.
Kikosi cha Chile kilikuwa; Bravo, Isla, Medel, Rojas, Albornoz/Mena dk46, Vidal, Diaz/D Pizarro dk46, Aranguiz, Valdivia/Gutierrez dk86, E Vargas na Sanchez. 
Peru; Gallese, Advincula, Zambrano, Ascues, Vargas, Carrillo/C Pizarro dk73, Ballon, Lobaton/Yotun dk73, Cueva/Ramos dk27, Farfan na Guerrero.

The former QPR loanee struck a superb winner into the top corner from well outside the box at the National Stadium
The former QPR loanee struck a superb winner into the top corner from well outside the box at the National Stadium
Peru goalkeeper Pedro Gallese could do nothing about Vargas' strike but the 10-man visitors put up a fight in Santiago
Carlos Zambrano caught Chile midfielder Charles Aranguiz on the back with his studs in the first half in Santiago
Carlos Zambrano caught Chile midfielder Charles Aranguiz on the back with his studs in the first half in Santiago
The Peruvian defender was booked earlier on in the contest but was still shown a straight red card by referee Jose Argote
The Peruvian defender was booked earlier on in the contest but was still shown a straight red card by referee Jose Argote
The Chile players celebrate at the end of the game - they will play either Colombia or Argentina in the Copa America final 
Vargas wheels away in celebration after opening the scoring for hosts Chile in the Copa America semi-final
Vargas wheels away in celebration after opening the scoring for hosts Chile in the Copa America semi-final
Vargas rolled the ball over the line after Alexis Sanchez' cross hit the post with the goalkeeper beaten
Vargas rolled the ball over the line after Alexis Sanchez' cross hit the post with the goalkeeper beaten
Arturo Vidal and Charles Aranguiz rush to congratulate Vargas after his strike put Chile in front in the first half

Gary Medel (right) stretches to cut out a cross but only manages to turn the ball past Claudio Bravo and into his own net

The Peru players celebrate after Medel's own goal gave them a route back into the Copa America semi-final

Aranguiz had to receive medical attention after he was caught by Zambrano during the first half of the Copa America semi-final in Santiago
 


c1
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea akizungumza na wanamichezo (hawapo pichani) kabla ya kuanza fainali ya Kombe la Chikawe katika Uwanja wa Sokoine, mjini Nachingwea. Timu ya Black Fire kutoka Kata ya Marambo na Timu ya Motisha kutoka Kata ya Kilimanihewa zilipambana na Timu ya Black Fire iliibuka mshindi kwa magoli 3 kwa 1. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema.
c2
Kapteni wa Timu ya Black Fire, Ally Njaidi (kulia) akipokea fedha taslimu Shilingi 500,000 pamoja na Kikombe cha ushindi kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema, baada ya kumalizika fainali ya Kombe la Mbunge wa Jimbo hilo, ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe. Timu hiyo iliirarua timu ya Motisha mabao 3 kwa 1 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Sokoine mjini Nachingwea. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Salimu Mwalimu, naye alihudhuria fainali ya mashindano hayo ambayo yalianzishwa na Mbunge Chikawe jimboni humo kwa kushirikisha timu 178 katika jimbo hilo.
c3
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea akimsalimia mchezaji wa Timu ya Black Fire, Faraji Mohamed wakati alipokuwa anaikagua timu hiyo kabla ya fainali ya Kombe la Chikawe ambayo yalifanyika katika Uwanja wa Sokoine, mjini Nachingwea. Timu ya Black Fire kutoka Kata ya Marambo iliibuka kidedea baada ya kuinyuka Timu ya Motisha, Kata ya Kilimani magoli 3 kwa 1. Nyuma ya Waziri Chikawe ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema.
c4
Kapteni wa Timu ya Motisha,  Saidi Chakupewa (kulia) akipokea zawadi ya ushindi wa pili, kikombe na fedha taslimu Shilingi 200,000 kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema, baada ya kumalizika fainali ya Kombe la Mbunge wa Jimbo hilo, ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe. Timu hiyo ilifungwa na Timu ya Black Fire mabao 3 kwa 1 katika mchezo uliofanyika katika Uwanja wa Sokoine mjini Nachingwea. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Salimu Mwalimu, naye alihudhuria fainali ya mashindano hayo ambayo yalianzishwa na Mbunge Chikawe jimboni humo kwa kushirikisha timu 178 katika jimbo hilo.
c5
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe  (aliyevaa kofia) akiwa na wachezaji wa timu ya Black Fire ambao ndio waliibuka washindi. Kushoto aliyesimama ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema.
c6
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe  (aliyevaa kofia) akiwa na wachezaji wa timu ya Motisha kutoka Kata ya Kilimanihewa. Kushoto aliyesimama ni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Pololeti Mgema.
c7
Msanii maarufu wa bongofleva, Seleman Jabir ‘Msaga Sumu’ akitumbuiza katika fainali ya Kombe la Chikawe lililofanyika katika Uwanja wa Sokoine mjini Nachingwea. Katika fainali hiyo, Timu ya Black Fire iliibuka kidedea baada ya kuifunga timu ya Motisha magoli 3 kwa 1.
c8
Mchezaji wa timu ya Black Fire (kulia) akisakata kabumbu katika fainali ya kombe la Mbunge Chikawe lililofanyika katika Uwanja wa Sokoine, mjini Nachingwea. Timu hiyo ya Black Fire iliinyuka timu ya Motisha magoli 3 kwa 1. Picha zote na Felix Mwagara.


xxx 
Baadhi ya Wanamichezo wa Polisi walioshiriki Michezo ya Wakuu wa Majeshi ya Polisi kusini mwa Afrika mwaka 2013 nchini Namibia wakiwa katika picha.

Timu za Jeshi la Polisi Tanzania zitakazoshiriki michezo ya Umoja wa Wakuu wa Majeshi ya Polisi kwa nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO),  mwishoni mwa mwezi julai nchini Swaziland zinaendelea kujifua vyema katika  kambi yao inayoendelea katika chuo cha Taaluma ya  Polisi Dar es Salaam (DPA).
Akizungumza na blog  hii Mkuu wa kitengo cha  michezo cha Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi SSP Jonas Mahanga alizitaja timu zilizopo kambini kuwa ni  pamoja na Timu ya Mpira wa miguu, pete, riadha na vishale ambapo hivi sasa zinajifua kuhakikisha kuwa zinakuwa vizuri pindi michuano hiyo itakapoanza kutimua vumbi.
Amesema timu hizo zitaanza kucheza michezo ya kirafiki ili kujipima nguvu na kuhakikisha wanafanya vizuri kwa kuwa michezo ya mwaka huu itakuwa na ushindani mkubwa kutokana na nchi zilizothibitisha kushiriki kujipanga vizuri.
SSP Mahanga amesema mpaka sasa nchi kumi na nne zimeshathibitisha kushiriki michuano hiyo na wanaendelea kuwakaribisha wadhamini mbalimbali watakaoweza kusaidia safari hiyo ili kuliletea taifa sifa.
Aidha amesema wachezaji wengi wa riaha wanaendelea na mazoezi katika timu ya taifa ya riadha na wengine wapo nchini Kenya ambapo muda utakapowadia wataungana na wenzao katika kambi hiyo ya Dar es Salaam.
Kwa upande wake kocha  wa timu ya mpira wa miguu Corporal John Tamba amesema wachezaji wake wamekuwa wakionyesha kiwango kizuri katika mazoezi kwa kuwa wengi wao wametoka katika mashindano hivi karibuni.
Amesema wachezaji wengi waliopo kambini wanatoka katika timu za Polisi Morogoro, Dodoma, Dar es Salaam, Tabora na Mara ambapo alisema kupitia michezo ya kirafiki atahakikisha timu yake inakuja na ushindi.

Sunday, June 28, 2015


Morgan Schneiderlin atakuwa ni wa pili kusajiliwa na klabu ya Manchester United Msimu 2015/2016 na atajiunga na Mashetani wekundu wiki ijayo Jumatano Dirsha la Usajili litakapofunguliwa rasmi.  Manchester United wamekamilisha usajili huo kwa kutoa kitita cha £25million kwa Morgan Schneiderlin – na taarifa zaidi kutoka Klabuni humo zinadai kuwa usajili unaendelea na ambao wamewaweka kwenye anga zao ni Kipa Jasper Cillsessen pamoja mchezaji wa Bayern Munich Bastian Schweinsteiger.
Kipa Jasper Cillsessen


Mshambuliaji Samuel Eto’o amejiunga na klabu ndogo ya Antalyaspor iliyopanda kucheza Ligi Kuu ya Uturuki msimu huu.
Makao makuu ya klabu hiyo ni mji wa Antalya ambao Yanga iliwahi kuweka kambi miaka miwili iliyopita. Kabla ya kutua hapo, Eto’o amewahi kuichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania, kabla ya Inter Milan ya Italia, Chelsea ya England na Everton ya England.


Paraguay wameifunga Brazil usiku huu kwa Mikwaju ya Penati (3-4) kwenye Michezo ya Copa America na Sasa kukutana uso kwa Uso na Argentina Nusu Fainali.Robinho akishangilia bao lake la dakika ya 15 kipindi cha kwanza kwa kuipatia bao 1-0 dhidi ya Paraguay baada ya kupata pasi safi kama kona kutoka kwa Dani Alves. 
Mpaka mapumziko Brazil ilikuwa ikiongoza kwa bao 1-0 dhidi ya Paraguay. Derlis González dakika ya 72 kipindi cha pili aliisawazishia bao kwa mkwaju wa penati na mtanange kumalizika dakika 90 kwa 1-1 na Mikwaju kupigwa.Shabiki wa Brazil wakiwa tayari kuangalia kipute!Brazil v Paraguay


HUKU ikishuhudiwa na  wachezaji wake wa kigeni Donaldo Ngoma na Joseph Tetteh Zutah waliowasili Dar es Salaam leo, Yanga ilijukuta ikitoka sare ya bila kufungana na Sports Club Villa ya Uganda kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwenye mechi hiyo maalumu kwa ajili ya kupinga mauji ya albino na mgeni rasmi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Saidi Mecky Sadiki, Yanga ilipoteza nafasi nyingi za kufunga kwenye mchezo huo.
Washambuliaji wa Yanga wakiongozwa na Amisi Tambwe na Simon Msuva walishindwa kufurukuta mbele ya ukuta thabiti wa Sports Club Villa ambao ni mabingwa wa Uganda.
Yanga iliwachezesha wachezaji wake wapya iliowasajili msimu huu kama vile winga Deus Kaseke aliyetoka Mbeya City, Malimi Busungu aliyetoka Mgambo JKT na chipukizi Godfrey Mwashuiya aliyesajiliwa wakati wa dirisha dogo walishindwa kabisa kuipenya na kushuhudia wakipoteza nafasi kadhaa za kufunga hasa kipindi cha kwanza.
Malimi Busungu alikosa bao la wazi kwenye dakika ya 31 baada ya kupokea pasi nzuri ya winga Goefrey Mwashuiya, lakini mpira aliopiga ulitoka pembeni kidogo ya Yanga la Sports Club Villa na dakika ya 39 Amis Tambwe alikosa bao la wazi akiwa ambeki peke yake na kipa wa Villa Sebweto Nicholaus.



Kwenye mechi hiyo timu zote zilifanya mabadiliko kadhaa kwa Yanga kuwapumzisha Malimi Busungu na kumuingiza Kpah Sherman na Nadir Haroub’Cannavaro’ alitoka baada ya kuumia na kuingia Pato Ngonyani.
Huku Villa ikiwatoa Kasule Abdulkarim na kumuingiza Dua Abeid na kisha kumtoa Kazibente James na kumuingiza Kamazi Dennis.
Hata hivyo Yanga walipata penalti kwenye dakika ya 79 baada ya Deus Kaseke kuangushwa kwenye eneo la hatari lakini Simon Msuva alipaisha penalti hiyo na kuinyima Yanga ushindi kwenye mechi hiyo ya kujipima nguvu kujiandaa na mashindano ya kombe la Kagame.
Yanga mpaka sasa imecheza michezo miwili ya kujipima nguvu ambapo wiki hii iliifunga klabu ya daraja la kwanza ya Friends Rangers kwa mabao 3-2 kwenye mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

Saturday, June 27, 2015

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu kutoka kwa Deogratius Mushi ya kuwania nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi vijijini wakati liporudisha katika ofisi za chama hicho zilizopo Majengo.
Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini ,Godlisen Maramia akimpongeza mtia nia Deuogratius Mushi kwa uamuzi wa kuingia katika kinya'ng'anyiri cha kuwania nafasi hiyo.
Mushi akipongezwa na makada wengine wa Chadema waliofika kumsindikiza ofisnini hapo.
Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu toka kwa Tally Kisesa ya kuwania Ubunge wa viti maalumu katika jimbola Moshi vijijini.

Mashindano ya Kombe la Meya Shinyanga 2015 (Pepsi Meya Cup 2015) yamezinduliwa rasmi leo na mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga.

Mashindano hayo ambayo yameandaliwa na mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam na kudhaminiwa na kampuni ya Vinywaji baridi ya  Pepsi (SBC Tanzania Ltd) yanashirikisha timu 17 za kata zote za manispaa hiyo na timu ya polisi Shinyanga.

Mashindano ya Kombe la Meya Shinyanga yakihusisha mpira wa miguu yataendelea kufanyika hadi tarehe 25,Julai 2015 na yatakuwa yanafanyika siku tatu kwa wiki yaani Ijumaa,Jumamosi na Jumapili.

Mshindi wa kwanza katika mashindano hayo ataondoka na kitita cha shilingi milioni moja na laki tano,kombe na medali ya dhahabu,wa pili shilingi milioni moja,kombe dogo na medali ya fedha na wa tatu shilingi laki tano,kombe dogo na medali ya shaba.

Malunde1 blog ilikuwepo wakati wa uzinduzi huo,Kadama Malunde,ametuletea picha kutoka eneo la tukio....
Mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akizungumza wakati wa ufunguzi wa Pepsi Meya Cup Shinyanga 2015,ambapo alisema lengo la mashindano hayo ya mpira miguu kwa vijana yatakayoshirikisha timu 18 za manispaa ya Shinyanga ni kwa ajili ya burudani,ajira na kusaka vipaji kutoka kwa vijana katika manispaa ya Shinyanga.
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh alisema mashindano hayo yatakuwa yatafanyika kwa muda wa mwezi mmoja na yatafanyika mara tatu kwa wiki katika viwanja vitatu vya Shycom,Kambarage na Polisi mjini Shinyanga.
Mashindano hayo yameanza leo Juni 26,2015 yatafikia tamati Julai 25,2015
Meza kuu wakiwa eneo la tukio.
Meneja mauzo wa Kampuni ya vinywaji baridi Pepsi kanda ya Ziwa Seni Makwaya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kombe la Meya Shinyanga 2015 ambapo alisema katika mkoa wa Shinyanga ndiyo mara ya kwanza kwa kampuni ya Pepsi kudhamini mshindano ya meya,ingawa huu ni mwaka wa tatu nchini Tanzania tangu waanze kudhamini mashindano ya namna hiyo.
Meneja mauzo  wa kampuni ya vinywaji baridi SBC Tanzania Limited (Pepsi) bwana Promod  Nair akizungumza wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kombe la meya Shinyanga 2015 ambapo alisema wameamua kudhamini mashindano hayo ili kuinua vipaji kutoka kwa vijana katika manispaa ya Shinyanga.
Meneja mauzo kampuni ya Pepsi mkoa wa Shinyanga bwana Benson Tweve akizungumza katika viwanja vya Shycom mjini Shinyanga ambapo alizitaka timu za Stand United na Mwadui FC kutumia fursa ya mashindano hayo ya Meya Cup kuchukua vijana wenye vipaji kwa ajili ya kuinua mkoa wa Shinyanga kimichezo.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kombe la Meya Shinyanga 2015,ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka vijana wa Shinyanga kutumia fursa ya mashindano hayo kuonesha vipaji vyao kwani michezo ni ajira.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akikabidhi vifaa vya michezo kwa afisa mtendaji wa kata ya Masekelo yenye Timu ya Masekelo fc iliyocheza mechi ya ufunguzi na Ngokolo fc kutoka kata ya  Ngokolo.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akikabidhi zawadi kwa mshindi wa kwanza katika mchezo wa mbio za baiskeli  Kulwa Ntyuki uliofanyika mjini Shinyanga wakati wa ufunguzi wa kombe la meya Shinyanga.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akikabidhi vifaa vya michezo kwa afisa mtendaji wa kata ya Ngokolo.

Waamuzi wa mchezo wa ufunguzi wakikagua wachezaji wa timu ya Masekelo FC na Ngokol0 FC.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akikagua timu ya Masekelo FC  kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Masekelo FC na Ngokolo fc haijaanza katika uwanja wa mpira wa Shycom Mjini Shinyanga .
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akikagua timu ya Ngokolo fc kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Masekelo fc na Ngokolo fc haijaanza katika uwanja wa mpira wa Shycom Mjini Shinyanga.
Waamuzi wa mchezo wakiwa uwanjani.
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine akizungumza na wachezaji wa timu ya Ngokolo fc  na  Masekelo fc na Ngokolo FC
Mgeni rasmi,ambaye ni mkuu wa wilaya ya Shinyanga ndugu Josephine Matiro akijiandaa kupiga penati huku meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akiwa golini.
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akihangaika golini baada ya kufungwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.
Mechi kati ya Masekelo fc na Ngokolo fc ukiendelea ambapo hadi mwisho wa mchezo,Masekelo fc bao 2,na Ngokolo fc bao 2.
Wakazi wa Shinyanga wakishuhudia mechi.
Wengine walipaki na baiskeli zao uwanjani kujionea kilichokuwa kinajiri uwanjani.
Mchezo unaendelea.
Tunafuatilia kinachoendelea....
Wachezaji wa Masekelo fc wakishangilia goli lao la kwanza.

Wakazi wa Shinyanga wakiwa juu ya ukuta wakifuatilia mechi.
Tunafuatilia mechi......
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam(mwandaaji wa Kombe la Meya Shinyanga 2015) akiteta jambo na  Meneja mauzo  SBC Tanzania Limited Pepsi bwana Promod  Nair( wadhamini wa kombe la meya Shinyanga 2015).
Meya wa manispaa ya Shinyanga Gulam Hafidh Mukadam akiteta jambo na msimamizi wa kituo cha Shycom bwana Geofrey Tibakenda,na mratibu wa Kombe la Meya bwana Paul Mganga,ambaye ni mkurugenzi wa Myklay Entertainment(katikati). 

Picha zote na Kadama Malunde.

waliotembelea blog