KOCHA wa Yanga, Marcio Maximo amesema pamoja na kumpa mkataba wa
miaka miwili mshambuliaji Geilson Santana Santos ‘Jaja’, bado anahitaji
kuona uwezo wa washambuliaji wawili raia wa Uganda, Hamisi Kiiza na
Emmanuel Okwi.
Yanga inalazimika kuachana na mchezaji mmoja wa kigeni kama kanuni za
usajili zinavyoagiza, baada ya sasa kuwa na wachezaji sita wa kimataifa
ambao ni Haruna Niyonzima, Mbuyu Twite, Andrey Coutinho, Jaja, Kiiza na
Okwi. Kanuni za usajili zinaruhusu timu kusajili wachezaji watano wa
kigeni.
“Nalazimika kuwaona mazoezini Okwi na Kiiza ndiyo nitakuwa na jibu la
kusema, lakini kwa sasa bado ni mapema mno kusema nitampunguza nani,
kwa sababu hata katika rekodi za klabu naona wachezaji hawa wamekuwa na
mchango mkubwa ndani ya timu ukitoa usumbufu ambao inasemekana wanao,”
alisema Maximo.
Maximo alisema anaufahamu fika uwezo wa kiungo wa Rwanda, Niyonzima
hana shaka naye, lakini naye pia alazimika kumuangalia kwa mara nyingine
uwezo wake ili ajiridhishe kwa sababu ni muda mrefu tangu amuone
akicheza.
“Ninachokitaka ni kuwa na kikosi imara ambacho hakitakuwa kikitegemea
baadhi ya wachezaji na ndiyo sababu ya kutaka kuwaona wachezaji hao ili
nijue uwezo wao na baada ya hapo nitaweka hadharani nani ambaye
hatutakuwa naye,” alisema Maximo.
Baada ya Maximo kumsajili Jaja wanachama na mashabiki wa timu hiyo
wamekuwa wakiumiza kichwa kutaka kujua mchezaji gani kati ya Kiiza na
Okwi atakatwa kwenye usajili wa msimu ujao huku kila mtu akiwa na
mapendekezo yake.
RSS Feed
Twitter
6:51 AM
Unknown

Manchester
City wamevunja Mechi yao ya Vijana wa chini ya Miaka 21, U-21, dhidi ya
HNK Rijeka huko Novigrad, Croatia hapo Jana kwa madai ya kukashifiwa
Kibaguzi kwa mmoja wa Wachezaji wao. 




Barcelona wamemsaini Beki wa Valencia Jeremy Mathieu kwa Mkataba wa Miaka Minne kwa Ada ya Euro Milioni 20. 




Rooney na Welbeck wakipongezana

Rooney akikatiza mbele kipa wa LA Galaxy na kufunga bao!
Wayney Rooney akichonga penati katika kipindi cha kwanza
Herrera aliongoza sana kwa kutoa mapande kwa wenzake
Nani akibanwa
James akipongezwa kwa kufunga bao la pili








