Thursday, July 24, 2014



Wayne Rooney  


WAYNE Rooney amempagawisha Kocha Louis van Gaal mazoezini. Wakati kikosi cha Manchester United kikiwa kwenye maandalizi ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu England huko Marekani, straika Rooney alionyesha maajabu mazoezini na kumfanya kocha kupagawa.
Kocha Van Gaal alimkimbilia Rooney na kumkumbatia baada ya straika huyo kufunga moja kwa moja kwa mpira wa kona aliopiga mazoezini juzi Alhamisi.
Baada ya kuonyesha kiwango hicho kwa kupiga kona na kutinga moja kwa moja wavuni, Van Gaal hakuna njia nyingine iliyobora kumpongeza mchezaji huyo zaidi ya kumfuata na kumkumbatia.
Akiwa hana siku nyingi kwenye kikosi hicho cha Man United, tayari Van Gaal amejikusanyia mashabiki wengi kutokana na kufurahishwa na mbinu zake mazoezini.
Kwenye mazoezi ya juzi Van Gaal alikuwa akiwanoa wachezaji wake namna ya kupiga mipira iliyokufa ndipo Rooney alipopiga kona na kwenda moja kwa moja wavuni. Kocha Van Gaal anaonekana kuwa na bahati ya mastaa wake kufanya maajabu ndani ya uwanja baada ya straika wake mwingine, Robin van Persie kufunga kwa kichwa kwa staili ya ajabu kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka huu wakati Uholanzi ilipoichapa Hispania mabao 5-1 mwezi uliopita.
Mwanzoni ilidhaniwa kwamba Rooney angekuwa kwenye wakati mgumu chini ya Van Gaal, lakini kwa sasa mambo yamekuwa tofauti na staa huyo anaonekana kuelewana na kocha wake mpya tangu alipotua kwenye kikosi hicho cha Old Trafford.
Man United inafanya mazoezi California na Alfajiri ya leo Alhamisi ilitarajiwa kumenyana na LA Galaxy kwenye mchezo wao wa kwanza wa kirafiki wa kujiandaa na msimu mpya.
Man United ambayo ilidai kwamba mwaka huu itafanya usajili utakaovunja rekodi ya uhamisho Uingereza ni miongoni mwa timu zitakazocheza Kombe la Chevrolet linalozishirikisha pia Washington DC, Detroit, AS Roma, Inter Milan na Real Madrid.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog