Thursday, July 24, 2014


DSC_0612-1 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamedhamiria kurejesha heshima yao iliyopotea kwa miaka mitatu mfululizo katika michuano ya ligi kuu soka Tanzania bara.
Simba ambayo imemuongezea mkataba wa mwaka mmoja kocha wake mkuu, Mcroatia, Zdravko Logarusic ipo katika maandalizi ya msimu mpya na malengo yao kwasasa ni kuelekea katika mchezo maalumu wa kirafki utakaopigwa siku ya Agosti 9 mwaka huu dhidi ya Ismailia ya Misri kwenye tamasha la klabu hiyo la ‘Simba Day’ ndani ya uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Tamasha la ‘Simba Day’ ni maalumu kwa mashabiki, viongozi na wanachama wa klabu hiyo kukutana kwa lengo la kubadilishana mawazo. Pia linatumika kama sehemu ya kutambulisha wachezaji wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu mpya.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog