Thursday, July 24, 2014



KOCHA Mkuu wa Simba, Mcroatia Zdravko Logarusic, 


KWA muda mrefu tumekuwa tukizungumzia suala la klabu kuwa na viwanja vyake vya soka kwa ajili ya mazoezi huku mkazo wetu ukiwa katika klabu za Ligi Kuu.
Hoja yetu hii kwa wakati wote imekuwa ikizinyooshea kidole klabu kongwe za Simba na Yanga ambazo hazijalipa umuhimu wa kipekee suala hili.
Klabu hizi ambazo zimeanzishwa miaka zaidi ya 70 iliyopita hadi sasa havina viwanja vyenye hadhi japo kwa ajili ya  kufanyia mazoezi.
Hili ni jambo la aibu ambalo tumekuwa tukilikemea mara zote hasa inapotokea timu kama Azam ambayo imeanza kutamba katika Ligi Kuu katika kipindi kisichozidi miaka mitano iliyopita kumiliki uwanja wenye hadhi ya kucheza hata mechi za kimataifa.
Hivyo hivyo na Mtibwa Sugar ambayo haina miaka 20 katika ligi ya juu nchini lakini inamiliki uwanja wake unaofaa kwa mazoezi na hata mechi za ligi.
Kilio chetu hicho walau kimesaidia kuiamsha Simba ambayo imeanza harakati za ujenzi wa uwanja wake maeneo ya Bunju B nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Hali ni hivyo hivyo kwa Yanga ambao tofauti yao na Simba ni kwamba wao wana eneo lakini hawalijali na hawaonyeshi nia ya dhati ya kulifanya liwe uwanja wenye hadhi japo ya mazoezi.
Wakati Yanga na Simba wakionekana kupuuza hoja hiyo, juzi Jumanne Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura alinukuliwa akisema kwamba kuanzia mwaka ujao hakuna klabu ya Ligi Kuu itakayoruhusiwa kushiriki mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) bila ya kuwa na leseni ya shirikisho hilo pamoja na uwanja.
Ni dhahiri kwamba Agizo hilo la CAF ambalo limo kwenye katiba ya TFF linaziumbua klabu hizi na nyinginezo zilizodhamiria kushiriki michuano inayoandaliwa na CAF.
Kwa kuwa Yanga na Simba ndizo ambazo zimekuwa zikichuana mara kwa mara kuwania tiketi ya kushiriki mashindano ya CAF, agizo hilo ni mtihani mwingine kwao.
Ni vyema viongozi wa klabu hizo wakaweka mikakati thabiti ya kuepukana na fedheha ambayo itajitokeza siku za mbele kwa kujikuta wakihaha kutafuta uwanja wa kuazima wakati wana uwezo wa kuwa na viwanja vyao.
Tunaamini kwamba iwapo CAF watawabana, watatafuta viwanja vya kuwalinda ambavyo vina hadhi lakini jambo hilo kwetu tunaliona kuwa ni la aibu.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog