Sunday, July 7, 2013

SIMBA NA YANGA (WABUNGE) WAKIPASHA MISULI KABLA YA MECHI KUANZA



 
.
 
Wabunge wa Simba na Yanga wakipasha misuli kabla ya mtanange wao kuanza
 
 



Ulijua kwamba Baba yake Beyonce kaoa huyu mwanamke mwingine?

Ulijua kwamba Baba yake Beyonce kaoa huyu mwanamke mwingine?

Beyonce na Solange wamepatiwa mama mpya na baba yao ambaye pia ni mkuu wa Music Entertainment world na pia alikuwa manager wa kundi la Destiny Child.Matthew Knowles ambaye ndiyo baba yake Beyonce na Solange kwa mama Tina Knowles, ambao wote waliachana na kumalizana mambo ya talaka mwaka 2009.
 
 
 
 Gena Charmaine ns Matthew Knowles
 
 Hivi karibuni, Matthew Knowles alifunga ndoa na model wa zamani Gena Charmaine ambaye alikuwa mchumba wake kwa muda wa mwaka mmoja na nusu, hii inamaanisha kwamba Beyonce na Solange wana haki zote za kumuita Gena mama kwa sababu ameolewa na baba yao ambae ni Matthew mwenye umri wa miaka 61, Gena ana 48 ambapo harusi hiyo inasemekana haikuhudhuriwa na mabinti hao wa mzee Matthew.
 
 
 

DK SHEIN ATEMBELEA MAONYESHO YA SABA SABA LEO

Rais wa Zanzibar na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akipata maelezo kutoka kwa Leila Issa Ali,katika mabanda ya washiriki wa maonesho ya sabasaba alipotembelea leo  jijini Dar es Salaam, (katikati) Waziri wa  Biashara Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Mazrui {Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}

ULEVI KWA WATU WENYE WANAOUGUA MARADHI YA UGONJWA WA UKIMWI NI HATARI. 

ULEVI miongoni mwa watu wenye Virusi Vya Ukimwi (VVU) umeelezwa kuwa ni hatari kwani pombe inaharibu mfumo wa kinga mwilini na kupunguza chembe hai za kinga -CD4 na kusababisha virusi kuzalishwa kwa wingi. 


Chembe za CD4 ni jeshi la kingamaradhi linalohusika na kukabiliana na magonjwa wakati mwili unapogundua kuna virusi au vimelea vya magonjwa.

Kwa mujibu wa kipeperushi cha madhara ya Pombe kwa Wenye VVU kilichoandaliwa na Mpango wa Taifa wa Kudh
ibiti Ukimwi (NACP), aidha kuchanganya dawa za ARV na pombe kunasababisha usugu na kuzalisha virusi hatari zaidi.

Pia, NACP ilisema pombe inasababisha madhara kwenye ini na kwamba baadhi ya dawa za Ukimwi ili zifanye kazi kikamilifu ni lazima zipitie kwenye ini na kwa mlevi linaweza kuwa na matatizo.

NIPASHE Jumapili ilifuatilia athari za ulevi kwa wenye VVU baada ya kupokea taarifa za baadhi ya watoa huduma wanaofuatilia mwenendo wa wagonjwa wa Dar es Salaam na mikoa ya jirani zikieleza kuwa wapo watu hunywa pombe licha ya kutumia dawa.

Walieleza kuwa baadhi ya watumiaji dawa wanabadili ratiba kwa kunywa vidonge asubuhi, wakati mwingine wanachanganya na kumeza dawa za mchana na usiku ili waende vilabuni kunywa pombe jioni.

Watoa huduma walisema wagonjwa huacha kunywa dawa kwa mujibu wa maelekezo jambo walilosema linakwamisha mikakati ya tiba.

”Utawakuta wanakimbilia kunywa komoni, kimpumu hata gongo” alisema mtoa huduma wa kituo cha afya kilichoko mkoani Pwani.

Wahudumu wengine waliozungumzia ukiukwaji wa masharti ya kumeza ARV walishauri kutoa dawa hizo chini ya usimamizi wa mtaalamu wa afya kama inavyofanyika kwa watumiaji wa dawa za kifua kikuu (TB) na kuandaa muongozo wa Wizara ya Afya unaoelekeza matumizi ya dawa na kukataza ulevi.

Walisema baadhi ya wagonjwa hupendelea pombe kwa madai kuwa hawaogopi kifo kwani wao ni “marehemu japo wanaishi” na wakidai ARV zina madhara mengine mwilini.

 



SPITBANK FORT, HOTEL ILIYOJENGWA MIAKA 134 ILIYOPITA KATIKATI YA MAJI HUKO UINGEREZA.



HOTELI ya Spitbank Fort ikionekana
 kwa juu ikiwa imejengwa mwaka 
1879 katikati ya kina maji ya
 habari nchini Uingereza 
ikiwa na umri wa miaka 134



Hapa ikionekana katikati ya kina cha maji

SIKU MOJA MOJA SIO MBAYA KUVUNJA SHERIA


 Askari wa jeshi la polisi wakiwa wamepakiwa katika pikipiki  wakisafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine wakati wakitekeleza majukumu yao ya kazi maarufu kama mshikaki kiten do ambacho ni uvunjaji wa sheria za usalama barabarani.

.

Dagaa mchelee, Changuuu, Kibuaaaa, Satoo, Dagaa kambaa, Sangaraaa, Peregeee.
  

Samakiiii. Kweli wote hao ni samaki, tena ni samaki wanaopendwa sana na wala samaki sio Tanzania tu, bali duniani kote. Upenzi wa samaki hautokani na utamu wake tu, bali pia unatokana na obora na virutubisho alivyonavyo samaki kwa afya ya binadamu.
Samaki ana madini ya Chuma, Chokaa na Ayodini kwa wingi yanayosaidia ukuaji wa mifupa kwa watu wa rika zote. Na mafuta yake yake yajulikanayo kama OMEGA 3 yanayosaidia ukuaji wa ubongo.
Wapo samaki wa kukaanga, samaki wa kuchemsha, samaki wa kupaka, samaki wa kukausha, samaki wa kubanika, mapishi yote hayo kuburudisha roho ya mlaji.

  Nchini THAILAND samaki wanaliwa kweli kweli. Katika mji wa BANGKOK kuna mgahawa maarufu unaouza aina zote za samaki wa baharini.
Mgawaha huo ulifunguliwa mwaka 1986, na walaji kutoka sehemu mbalimbali duniani hufika mgawaha huo kufaidi samaki.
Mteja huchagua samaki ambaye bado anapumua, ndipo wapishi humtoa ndani ya maji, wakakatisha maisha yake na kumuweka mekoni, akitayarishwa kwenda kwenye minywa cha mlaji ambako, ndiko yatakuwa maziko yake.
Hata hapa kwetu, samaki hawatoshi, wakati mwingine wavuvi wanatumia mbinu haramu kuwavua. Wavuvi, samaki watamu jamani, kuna mbinu mpya ya kuwaongeza? Tupeni mbinu hiyo tufaidi. Samakiii, Dagaa mchelee, Changuuu, Kibuaaaa, Satoo, Dagaa kambaa, Sangaraaa, Peregeee.

Safari ya Rais KIkwete Sunderland huenda ikawa mwisho wa kiu ya mpira Tanzania

Jumapili iliyopita nilibahatika kuwa ndani ya msafara mahususi uliozunguka na mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete.
Ingawa msafara huo ulihusu michezo na mpira, uliwakutanisha pia baadhi ya Watanzania wakazi wa Jiji la Sunderland na wale wasomao Chuo Kikuu cha New Castle, Kaskazini Mashariki ya Uingereza
Rais Kikwete alipotua jijini Sunderland jua lilikuwa liking’ara, saa za adhuhuri...Mwezi wa sita huwa kiangazi ndiyo kinaanza anza Ulaya hivyo siyo lazima kuvaa makoti mazito. Mkuu wa nchi alikuwa nadhifu na wasaizidi wake kama kawaida, akiwemo Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk Fenella Mukangara, Balozi wetu hapa Peter Kallaghe na maofisa wengine husika walichangamkia shughuli hii muhimu na ya kihistoria, kama tutakavyoona.
Upande wa wenyeji je?
Mmiliki klabu ya Sunderland ni tajiri wa Kimarekani, Ellis Short kipato chake kinakisiwa kuwa Dola za Marekani 3.5 bbilioni, ndiye alimwalika Rais Jakaya Kikwete na Paul Hinks, Mwendeshaji Mkuu wa Kampuni ya Ujenzi Umeme ya Symbion Power, yenye makao Marekani. Pande hizi mbili ndizo zitashirikiana, moja kujenga Symbion chuo cha kufundishia watoto mpira, mwingine kutoa mafunzo hayo Sunderland AFC.
Kwa vipi klabu iliyochukua nafasi ya 17 mwaka huu ndani ya Ligi ya Uingereza kati ya timu 20, ichaguliwe kutufariji, aliulizwa Rais Kikwete baadaye na wanahabari? Kwa nini wasiwe Arsenal, Chelsea, Liverpool au watemi wa Manchester United?
Rais Kikwete akajibu ilitokana na Ellis Short mwenyewe kuitembelea Tanzania kwa shughuli zake nyingine; Hapo msosi ukatayarishwa. Sunderland inasifika kwa kituo chake bora kufunzia watoto kiitwacho “Academy of Light.” Ukichunguza sana maendeleo ya wachezaji wote wakubwa duniani, huanzia vilabu vidogo ndiyo wakanunuliwa na hatimaye kutamba na timu zenye fedha na uwezo zaidi. Mfano mzuri ni wanasoka maarufu wa ligi ya Uingereza Theo Walcott (Arsenal) Oxlade Chamberlain( Arsenal ) na Gareth Bale wa Tottenham walioanzia mpira utotoni Southampton Football Academy.
Sidhani ni wengi tunaoijua au kuisikia, Southampton, barani Afrika. Lakini huu ni ushahidi wa namna klabu ndogo zisizojulikana zinavyoivisha na kumeng’enya wachezaji chipukizi. Gareth Bale sasa hivi anapiganiwa na kila klabu na inasemekana Real Madrid wanamtamani kwa mate na udenda. Hata kwetu Bongo wachezaji wengi huanzia klabu ndogo za mikoani kabla ya kununuliwa Simba na Yanga.
Hivyo Sunderland inaweza isiwe kubwa, lakini uwezo wake wa kiufundi utaikidhi sana Tanzania. Msafara wa Rais ulionyeshwa eneo hili kubwa lililokamilika miaka kumi iliyopita. Humo mna sehemu za kuogelea, viwanja vyenye majani safi ndani na nje, Gym za mazoezi, madarasa na vyombo mbalimbali vya mafunzo. Mbali na chuo, Rais Kikwete alitembezwa uwanja wa “Stadium of Light” ambao hujaza watazamaji 49,000. Huu ni uwanja wa tano kwa ukubwa Uingereza nzima. Hapa huwepo vilevile maonyesho siyo madogo ya muziki, kama lile la mwimbaji nguli Rihanna toka Barbados aliyetumbuiza juzi Alhamisi.
Kuna hilo la kiufundi, halafu historia.
Si wengi wanaofahamu historia za vilabu vyetu.
Rais alipowaeleza wanahabari wa Kizungu kuwa zamani Simba ilipoanzishwa mwaka 1936 iliitwa Dar Sunderland, alikuwa akikumbusha tulikotoka.

PILIKA PILIKA ZA SABA SABA YA 37.

 Wakazi wa Jiji la Dar Wakiwa kwenye foleni tayari kwa kuingia kwenye viwanja vya Sabasaba vilivyopo katika barabara ya kilwa Jijini Dar Es Salaam Mapema leo Asubuhi.

 Baadhi ya Wafanyabiashara wakiendelea kuingia vifaa vyao tayari kwa maonyesho na kuuza bidhaa na huduma zao


waliotembelea blog