Sunday, July 7, 2013

.

Dagaa mchelee, Changuuu, Kibuaaaa, Satoo, Dagaa kambaa, Sangaraaa, Peregeee.
  

Samakiiii. Kweli wote hao ni samaki, tena ni samaki wanaopendwa sana na wala samaki sio Tanzania tu, bali duniani kote. Upenzi wa samaki hautokani na utamu wake tu, bali pia unatokana na obora na virutubisho alivyonavyo samaki kwa afya ya binadamu.
Samaki ana madini ya Chuma, Chokaa na Ayodini kwa wingi yanayosaidia ukuaji wa mifupa kwa watu wa rika zote. Na mafuta yake yake yajulikanayo kama OMEGA 3 yanayosaidia ukuaji wa ubongo.
Wapo samaki wa kukaanga, samaki wa kuchemsha, samaki wa kupaka, samaki wa kukausha, samaki wa kubanika, mapishi yote hayo kuburudisha roho ya mlaji.

  Nchini THAILAND samaki wanaliwa kweli kweli. Katika mji wa BANGKOK kuna mgahawa maarufu unaouza aina zote za samaki wa baharini.
Mgawaha huo ulifunguliwa mwaka 1986, na walaji kutoka sehemu mbalimbali duniani hufika mgawaha huo kufaidi samaki.
Mteja huchagua samaki ambaye bado anapumua, ndipo wapishi humtoa ndani ya maji, wakakatisha maisha yake na kumuweka mekoni, akitayarishwa kwenda kwenye minywa cha mlaji ambako, ndiko yatakuwa maziko yake.
Hata hapa kwetu, samaki hawatoshi, wakati mwingine wavuvi wanatumia mbinu haramu kuwavua. Wavuvi, samaki watamu jamani, kuna mbinu mpya ya kuwaongeza? Tupeni mbinu hiyo tufaidi. Samakiii, Dagaa mchelee, Changuuu, Kibuaaaa, Satoo, Dagaa kambaa, Sangaraaa, Peregeee.

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog