Friday, March 6, 2015


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe akiwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara pamoja na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Azam TV wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015.
 
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara pamoja na uongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Azam TV wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo kutoka kwa fundi mitambo Mkuu wa Azam TV Bw. Mehdoub al Hadad juu ya namna gari la kurusha matangazo nje ya studio (OB Van) linavyofanya kazi wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara wakitmbezwa sehemu mbali mbali za Azam TV na mwenyeji wao Bw. Saidi Salim Bakhressa wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Bw. Saidi Salim Bakhressa wakati alipohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Bw. Saidi Salim Bakhressa wakati alipohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa studio mpya za stesheni hiyo iliyopo Tabata Relini jijini Dar es salaam leo Machi 6, 2015. 


 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa pole wanafamilia wa MzeeZakaria  Limbe ambao wamepoteza wototo wane katika mafa ya mvua kubwa yenye upepo na  mawe iliyonyesha katika eneo la Mwakata Machi  3 usiku. Alikwenda katika maeneo yaliyoathirika leo  kuwapa pole wananchi. 
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akipa pole Shoma Petro  ambaye ni mmoja wa majeruhi wa maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa yenye upepo na mawe iliyonyesha kwenye  eneo la  Mwakata wilayani Kahama Machi 3, 2015 usiku. Mheshimiwa Pinda alikwenda kwenye hospitali a wilaya ya Kahama kuwapa pole  majeruhi waliolazwa hospitalini hapo.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpa pole Mzee  Donald Lubunda ambaye  amepoteza watoto wane katika maafa yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha  katika  eneo la Mwakata wilayani Kahama Machi 3 usiku. Mheshimiwa Pinda alikwenda kuwapa pole waathirka leo
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Waziri wa Nchi Ofisi yaWaziri Mkuu, Jenista Mhagama  (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa ShinyangaDr Rufunga kukagua maeneo yalyoathiriwa na mvua kubwa iliyoambatana  na upepo mkali na mawe katika eneo  Mwakata wilayani Kahama usiku Machi 3, 2015. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ametembelea baadhi ya familia zilizopoteza wapendwa wao pamoja na majeruhi waliolazwa kwenye hospitali ya wilaya ya Kahama kutokana na maafa ya mvua ya mawe iliyonyesha usiku wa kuamkia jana.

Akizungumza na wafiwa katika vijiji vya Mwakata na Magugung’hwa katika kata ya Mwakata wilayani Kahama leo mchana (Alhamisi, Machi 5, 2015) Waziri Mkuu alisema Serikali haitawaacha katika kipindi hiki kigumu walichonacho.

Waziri Mkuu pia alitumia fursa hiyo kuwafikishia wafiwa na waathirika wa maaafa hayo salamu kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye aliwaomba wawe na subira katika kipindi hiki kigumu wanachopitia.

Akiwa katika shule ya msingi Mwakata ambako watu 250 wanahifadhiwa hapo kwa muda, Waziri Mkuu aliwaambia wakazi hao pamoja na wananchi waliofika kumsikiliza kwamba Serikali imepanga kuleta vyakula, mahema, mablanketi na madawa ya hospitali ili kuwasaidia waathirika hao. “Serikali haitaacha mtu afe kwa njaa,” alisema.


Waziri mkuu Mizengo Pinda akitua na ndege katika uwanja wa ndege wa Buzwagi mjini Kahama mkoani Shinyanga kujionea hali hali ya maafa ya mvua kubwa ya mawe na upepo iliyonyesh juzi katika kata ya Mwakata-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
 
 Ndege aliyokuja nayo waziri mkuu Mizengo Pinda-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
 Waziri mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Kahama baada ya kuwasili-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
Waziri mkuu Mizengo Pinda akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Shinyanga akiongozwa na mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Rufunga-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama

Waziri mkuu Mizengo Pinda baada ya kufika katika kata ya Mwakata-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama

Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwa katika moja ya familia ya Masemba Mabuli iyofiwa na watoto watano katika maafa ya mvua-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama

 Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenister Muhagama, akielekeza kuwa misaada yote inayotolewa na wadau mbalimbali isipelekwe makao makuu ya wilaya, badala yake ipelekwe katika eneo la maafa-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
 Moja ya nyumba zilizoharibika-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
 Wakazi wa Mwakata wakiwa na ndugu jamaa na marafiki wakifarijiana katika moja ya familia iliyopatwa maafa wakiishi kwa pamoja baada ya kukosa makazi-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
Waziri mkuu akishuhudia makaburi katika kata ya Mwakata-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama

 Makaburi 5 ya familia moja-Picha na Marco Maduhu-Malunde1 blog Kahama
+++++++++++++++
Wakati idadi ya watu waliopoteza maisha katika maafa yaliyosababishwa na mvua iliyonyesha ikiambatana mawe, upepo mkali na kubomoa nyumba za wananchi Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, ikiongezeka kutoka 42 na kufikia 46, baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamelihusisha janga hilo na ushirikina.

 
Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Mwakata wilayani Kahama, Salum Mohamed, alimweleza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwa baadhi ya wananchi wamejenga dhana kuwa tukio hilo limetokana na ushirikina.
Hata hivyo, Pinda aliyewasili eneo hilo jana, aliwataka wananchi hao kuachana na dhana hiyo potofu kuwa mvua zilizonyesha na kusababisha maafa hayo, zimetokana na ushirikina.
Mvua hiyo ilinyesha juzi usiku na kuleta maafa katika vijiji vya Mwakata, Nhumbi na Magung’hwa vilivyopo kata ya Isaka wilayani Kahama.
Idadi hiyo imeongezeka kufuatia majeruhi wanne waliokuwa wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama kufariki dunia usiku wa kuamkia jana kuongeza idadi  ya waliokufa katika janga hilo kufikia 46.
Waziri Mkuu, alitembelea vijiji vilivyoathirika na kuwapa pole waathirika na kusema serikali itahakikisha waathirika wote wanapewa msaada unaotakiwa na kwamba tayari chakula kimeanza kugawiwa kwa wananchi na mahema ya kutosha yametolewa. 
Pinda aliagiza waatalam kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuweka kambi katika kijiji cha Mwakata kilichoathirika kwa ajili ya kufanya tathmini.
Waziri Mkuu alisema kutokana na janga hilo, kuna uwezekano wa kutokea magonjwa ya mlipuko.
Aidha, aliiagiza timu ndogo ya uratibu wa maafa iliyoundwa na Mkoa wa Shinyanga, isimamie vizuri misaada inayotolewa na wasamaria wema ili iwafikie waathirika wote.
MBUNGE WA MSALALA
Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, ambaye alitembelea katika hospitali hiyo jana, alithibitisha kuwa kati ya walioongezeka ni watoto watatu, wakazi wa kijiji cha Mwakata na mazishi yalifanyika jana katika kijiji hicho.
PINDA AWASILI, ATOA TAMKO 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, jana aliwasili Kahama na kutembelea vijiji vilivyoathirika na kuwapa pole waathirika na kuwataka wananchi waondokane na fikra potofu kuwa tukio limetokana na masuala ya kishirikina.
Alisema serikali itahakikisha waathirika wote wanapewa msaada unaotakiwa na kwamba tayari chakula kimeanza kugawiwa kwa wananchi na mahema ya kutosha yametolewa.
Pinda aliagiza waatalam kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuweka kambi katika kijiji cha Mwakata kilichoathirika kwa ajili ya kufanya tathmini.
Waziri Mkuu alisema kutokana na janga hilo, kuna uwezekano wa kutokea magonjwa ya mlipuko.
Aidha, aliiagiza timu ndogo ya uratibu wa maafa iliyoundwa na Mkoa wa Shinyanga, isimamie vizuri misaada inayotolewa na wasamaria wema ili iwafikie waathirika wote.
MISAADA KWA WAATHIRIKA
Serikali kupitia Kitengo cha Maafa kilichopo Ofisi ya Waziri Mkuu, imetoa tani 20 za chakula ambapo kati ya kiasi hicho, maharage tani tano, sukari tani 1.3 na mafuta ya kupikia lita 1,126.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Florens Turuka, katika taarifa yake jana kwa vyombo vya habari alisema misaada mingine iliyotolewa kwa waathirika hao ni blanketi 650, ndoo 82 zenye ujazo wa lita 20, ndoo 82 za lita 10 vifaa vya kupikia seti 82 na madumu 82.
Dk.Turuka alisema misaada zaidi inahitajika kwa waathirika kama vile sare za shule, madaftari ya wanafunzi, mavazi ya kike na kiume na chakula.
“Kwa kuzingatia kuwa waathirika hawa wamepoteza mali na fedha katika maafa haya, misaada ya vifaa vya ujenzi inahitajika, utaratibu wa kupokea misaada hiyo kwa walio Dar es Salaam wanaweza kuiwasilisha Idara ya Kuratibu Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu au kwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,” alisema.
Dk.Turuka alisema serikali itaendelea kuwasaidia waathirika dhidi ya changamoto zinazoweza kujitokeza hususani za kiafya zinazosababisha na uchafuzi wa vyanzo vya maji na mazingira.
WAZIRI JENISTER MHAGAMA
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Jenister Muhagama, alielekeza kuwa misaada yote inayotolewa na wadau mbalimbali isipelekwe makao makuu ya wilaya, badala yake ipelekwe katika eneo la maafa.
Kituo kikubwa cha waathirika kimewekwa katika Shule ya Msingi Mwakata ambako waathirika wamehifadhiwa kwa muda katika majengo matatu.
Mbunge wa Msalala, Maige alimuomba Waziri Mkuu kuangalia uwezekano wa kufuta kodi ya majengo ili vifaa vya ujenzi viuzwe kwa bei rahisi kuwawezesha wananchi kujenga nyumba bora.
Nyumba nyingi zilizobomoka katika tukio hilo zimejengwa kwa matofali ya tope, hivyo mvua kubwa zinaponyesha zinabomoka kirahisi.
 Maige aliomba ahadi ya serikali ya kuwasaidia waathirika wa tukio hilo ifanyiwe kazi haraka.

Wananchi kwa upande wao, waliiomba serikali kuwajengea vyoo zaidi katika kambi waliyohifadhiwa kwa kuwa wanachokitumia sasa ni kimoja tu.

 Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji cha Mwakata, Salum Mohamed, alisema kutokana na idadi kubwa ya wananchi walioathirika kuendelea kutumia choo kimoja ni hatari kiafya kwa kuwa kunaweza kutokea magonjwa ya mlipuko.

Mohamed aliomba huduma ya umeme irejeshwe kijijini hapo kufuatia nguzo za umeme zilizokuwapo kuharibiwa na mvua.
DC KAHAMA
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya, alisema katika tukio hilo kaya zilizoathirika ni 400 zenye idadi ya watu zaidi ya 1,500.
Mpesya alisema majeruhi 52 ambao ni kati ya 98 waliokuwa wamelazwa katika Hospitali ya wilaya hiyo, wameruhisiwa baada ya hali zao kuwa nzuri.
CUF WATOA SALAMU
Wakati huo huo, Chama cha Wananchi (CUF), kimetoa salamu za rambirambi kwa ndugu na jamaa za watu waliopoteza maisha katika tukio hilo.
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Shaweji Mketo, katika taarifa yake kwa vyombo vya habari alisema chama hicho kimebaini kuwa madhara makubwa ya mafuriko yanayotokea katika maeneo mbalimbali nchini yanasababishwa na miundombinu ya mikondo ya maji kutozingatiwa kurekebishwa.
Alisema mfano katika Wilaya ya Kahama, imebainika kwamba wakazi walio pembezoni mwa barabara, kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kupunguza madhara endapo barabara zingejengwa mitaro yenye uwezo wa kupitisha maji ili kuyaelekeza mahali stahiki na siyo kwenye nyumba za watu.
Mketo alisema CUF inaitaka serikali kupitia upya utaratibu wa  kukabiliana na majanga makubwa ili kuongeza uharaka wa kuyashughulikia. 
Alisema serikali inapaswa kuhakikisha mazingira yote yanayoweza kuleta madhara ya mafuriko yanaepushwa mapema na mikondo yote ya maji hasa mito, ilindwe na kuangaliwa mara kwa mara kuhakikisha uwezo wake wa kutiririsha maji unaongeza ufanisi wake.
“CUF kinatoa pole kwa wananchi wote wa Kahama, Moshi, Rufiji, Morogoro na Katavi walioathiriwa na mafuriko haya. Pia CUF inatoa salamu za rambirambi kwa wote waliofiwa na ndugu na jamaa zao katika mvua hizi,” alisema Mketo.




Wanafunzi wakisoma Risala mbele ya Viongozi waliohudhuria hafra hiyo katika shule ya Msingi Bunena wakati wa Kukabidhi Msaada wa Madawati.

Risala ikikabidhiwa kwa mgeni Rasmi Meneja wa TTCL Bw. Salum Mbaya(kulia).
Na Faustine Ruta, BukobaKwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu (TTCL) leo Kampuni hiyo imekabidhi Madawati 50 yenye thamani ya Tsh 2.5 Milioni. Kila Dawati lina uwezo watoto 3 hivyo watoto 150 wataweza kukaa katka Madawati hayo. Msaada huo ikiwa ni kuitikia Wito wa kuchangia Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Kagera na hatimae Taifa zima.







Mcheza Filamu wa Hollywood Harrison Ford
Mcheza filamu wa Hollywood,Harrison Ford, anapatiwa matibabu katika Hospitali moja mjini Los Angels baada ya ndege yake kuukuu kuanguka katika uwanja wa Gofu.
Mcheza filamu huyo mwenye umri wa miaka 72 alikuwa akiendesha ndege hiyo mwenyewe.
Ndege hiyo ndogo ilinasa kwenye mti wakati ilipokuwa ikitua kwa dharula.

Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema Harrison Ford alikuwa amejeruhiwa, akionekana kuwa na damu iliyotapakaa usoni.
Matabibu wamesema Ford anaendelea vizuri na kuwa hali yake itatengamaa kabisa.
Harrison Ford Hospitalized After Crashing Plane
Soma Zaidi Hapa »


MAPENDEKEZO KWA DK. JAKAYA KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MAUUNGANO WA TANZANIA KATIKA KIKAO CHAKE NA WAWAKILISHI WA CHAMA CHA ALBINO TANZANIA, IKULU, TAREHE 5/3/2015 JUU YA NAMNA YA KUSAIDIA KUKOMESHA MAUAJI, UKATAJI VIUNGO, UTEKAJI NA UKATILI DHIDI YA WATU WENYE UALBINO NA FAMILIA ZAO


Mh. Rais,
Kutokana na kuendelea kushamiri kwa mauaji, ukataji viungo, utekwaji na ukatili dhidi ya watu wenye ualbino na familia zao, Chama Cha Albino Tanzania kina mapendekezo yafuatayo kwako:


Ushughulikiwaji wa kesi zinazohusiana na mauaji, ukataji viungo, utekwaji na ukatili wa aina hiyo kwa watu wenye ualbino upewe kipaumbele, kupitia mkakati maalum, kwamba:


Mashauri yote ambayo hayajapelekwa mahakamani uchunguzi na upelelezi ukamilishwe mapema na yapelekwe mahakamani;
Kesi zilizoko mahakamani zisikilizwe mapema, kupitia mahakama au utaratibu maalum na kwa watakaokutwa na makosa hukumu itekelezwe mara moja;


Kuwepo mpango maalum wa kufuatilia kesi hizi, hasa kupitia Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, ili kutoa msaada wa kisheria ikiwemo kwa wale ambao hawajaridhishwa na maamuzi ya mahakama waweze kukata rufaa.

Ulinzi shirikishi katika jamii uimarishwe katika ngazi zote, kuanzia ngazi ya vijiji au mitaa zijengewe uwezo ili ziwe na mipango maalum ya kutoa ulinzi kwa watu wenye ualbino kwa kushirikiana na jamii kwani pia wao ndio wanaowatambua wageni na kupitia wao ni rahisi hata kupata ushahidi katika kesi mbalimbali. 


Ni rahisi pia kupitia kamati hizi kuzitambua kaya zilizoko katika mazingira ambayo sio salama na kufanya uraghbishi, ikiwemo kuzihamishia katika makazi salama.

Serikali iwe na mkakati maalum, endelevu na shirikishi wa kuelimisha jamii juu ya ualbino na haki za binadamu na mpango huu wa elimu kwa jamii uwe na bajeti maalum ambayo itakuwa vyema kwa kuanzia ijadiliwe katika bunge lijalo la bajeti;


Wahanga wa matukio haya wakiwemo watoto wasaidiwe ili kuboresha maisha yao na kuwajengea misingi mizuri ya maisha ya baadae:



Watoto walio katika kambi wasaidiwe kupata mahitaji yao ya msingi kama vile chakula, afya, malazi na mavazi kupitia serikali;


Kambi hizi ziangaliwe kwa namna pana, ikiwa ni pamoja na kuwapa mafunzo kupitia vyuo mbalimbali vijana walioishi kwa muda mrefu kambini ili waweze kujitegemea na pia kupunguza athari nyingine zinazoweza kutokea,ikiwemo mimba na udhalilishwaji wa kingono kama ambavyo imekuwa ikiripotiwa katika taarifa mbalimbali;


Watu wazima wanaoishi katika kambi hizi wasaidiwe kuishi maisha ya staha, ikiwemo kupata ajira japo ndani ya kambi hizo hizo ili waweze kujikimu na kutoa mchango wao kwa kuwatunza watoto wakati huu ambao hawawezi kurudi nyumbani;


Wale waliopata ulemavu au kujeruhiwa serikali iwasaidie waweze kujimudu. Kuna ambao maisha yao yamekuwa ya magumu sana kwa mambo mengi hivyo kuwa mzigo mzito kwa familia zao ambazo nazo nyingi ni masikini;


Kambi hizi zisichukuliwe kama za kudumu,ila zijengewe mazingira ya kutoa elimu jumuishi, kuanzia elimu ya awali;
Wahanga na familia zao wapewe ushauri (counseling) kwani wengi huwa wanaathirika sana kisaikolojia na hapajawa na mkakati wa kuwafuatilia.


Kwa kuwa mauaji yanayoendelea yanatokana na imani za kishirikina, na katika matukio waganga wa kienyeji wanahusika, Sheria ya Tiba Asili na Tiba Mbadala pamoja na Sheria ya Uchawi zipitiwe upya, zifanyiwe maboresho ili kuweza kutofautisha vizuri juu ya aina hizi za tiba au huduma, na jamii ishirikishwe katika uratibu wa shughuli za waganga wa tiba mbadala au tiba asili.


Kiundwe Kikosi Kazi maalum kufanya uchunguzi wa kina kubaini wanaotuma na wanaoununua viungo vya watu wenye ualbino ili washughulikiwe na kuondoa kabisa jambo hili ambalo limekuwa na kadhia kubwa kwa watu wenye ualbino, familia zao na jamii na Taifa kwa ujumla.


Itengenezwe kanzidata (database) kwa watu wenye ualbino kote nchini ambayo itakuwa na taarifa mbalimbali (demographic information), zikiwemo idadi na mahali (makazi); jinsi na umri; elimu na ajira na; hali ya saratani ya ngozi, ili kuisaidia serikali na wadau wengine waweze kupanga na kutekeleza mikakati mbalimbali ya ulinzi na jinsi ya kuboresha maisha ya watu wenye ualbino kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya Taifa letu.


Tunapendekeza kukawepo na Kamati Maalum ya Kitaifa, ambayo ni jumuishi, iwe inakutana kwa vipindi maalum (mara kwa mara) kila mwaka kujadili, kutoa mrejesho na kuishauri serikali na wadau wengine. Kamati hii iwe chini ya Ofisi ya Rais au Makamu wa Rais au Waziri Mkuu ili iwe rahisi kuratibu mambo yake kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Watu Wenye Ulemavu. Kwa kuanzia, kamati hiyo pia ifuatilie utekelezaji wa mapendekezo haya kama ambavyo utaona yafaa, Mh. Rais.


Mh. Rais tunakushukuru sana kwa kutusikiliza. Mapendekezo haya na mengine yatakayochangiwa na wadau yatasaidia kukomesha mauaji na kuwafanya watu wenye ualbino na familia zao kuishi kwa amani kama watu wengine. Utayari wetu wa kushirikiana nawe na serikali yetu kama ambavyo tumekuwa tukifanya wakati wote hauhitaji msisitizo.

waliotembelea blog