Tuesday, August 19, 2014



Benfica wamekamilisha Usajili wa Kipa Brazil Julio Cesar ambaye alikuwa anaidakia timu ya QPR
Julio Cesar mwenye miaka 34 alisainiwa na Klabu ya Uingereza QPR mwaka 2012.


Julio Cesar akiokoa mkwaju wa penati kwenye Kombe la Dunia

LUIS SUAREZ: ‘SITAUMA MTU MENO TENA NIMEPATA USHAURI NA ONYO KALI...SASA NITUPIENI MACHO MUONE MAKALI YANGU UWANJANI!!

Thumbs up: The striker said he was delighted to be joining the Catalan giantsSTRAIKA wa Barcelona Luis Suarez ameahidi kutorudia tena kuuma Meno Wachezaji wenzake Uwanjani wakati wa Mechi baada ya kupata msaada wa Mabingwa wa Matibabu wa Magonjwa ya Akili.
Hivi sasa Suarez yupo kwenye Kifungo cha Miezi Minne alichopewa na FIFA baada ya kumuuma Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini wakati wa Mechi ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil hapo Juni 25 wakati Uruguay inacheza na Italy na hilo lilikuwa tukio lake la 3 la kung’ata Meno Uwanjani.
Smiles: Suarez strolled around the Camp Nou turf having had his ban lifted
Lakini Suarez, mwenye Miaka 27, amesema: “Nawaambia Mashabiki, msiwe na wasiwasi kwa sababu sitarudia tena!”

“Nimeongea na Madaktari wa Magonjwa ya Akili na wameniambia nilikabili tatizo hili na kuomba msamaha. Nimefanya hivyo. Sasa naangali baadae kuhusu Barcelona.”
Mara baada ya Kifungo hicho alichopewa Brazil ambacho kilimkataza kushughulika na lolote kuhusu Soka, Suarez alikata Rufaa huko CAS, Mahakama ya Usuluhishi Michezoni, na kupunguziwa Adhabu kwa kuruhusiwa kufanya Mazoezi na pia kucheza Mechi za Kirafiki.

Jana Usiku Suarez aliweza kuichezea Barcelona kwa mara ya kwanza kwenye Mechi ya Kirafiki Uwanjani Nou Camp alipoingizwa Dakika 13 za mwishoni wakati Barcelona ilipoichapa Club Leon ya Mexico Bao 6-0 na kutwaa Joan Gamper Trophy.
Expectation: He will be wearing the number nine shirt for Barcelona this season following Alexis Sanchez
Wakati huo huo, Barcelona imekanusha kuwa ilimnunua Suarez kwa Pauni Milioni 75 kutoka Liverpool na kusema Fedha sahihi ni Pauni Milioni 65.


SUAREZ: Matukio yake ya utata:
Juni 2014:   - Afungiwa Miezi 4 kwa kumng’ata Beki wa Italy Giorgio Chiellini
Aprili 2013: – Afungiwa Mechi 10 kwa kumng’ata Beki wa Chelsea Branislav Ivanovic
Des 2011: – Afungiwa Mechi 8 kwa kumkashifu Kibaguzi Patrice Evra wa Man United


Razack Siwa (kushoto) akiwa na aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Mholanzi, Ernie Brandits

Na Mwandishi Wetu, Tanga
ALIYEKUWA Kocha wa makipa wa timu ya Yanga Razack Siwa  hatimaye
ameingia mkataba wa kuwanoa makipa wa timu ya Coastal Union ya Tanga ambayo inajiandaa na maandalizi ya msimu ujao wa Ligi kuu Tanzania bara utakaoanza Mwezi ujao hapa nchini.


Siwa ameingia mkataba wa mwaka mmoja lengo likiwa kuipa mafanikio makubwa timu hiyo msimu ujao.
Tayari Kocha Siwa ameungana na wachezaji wa timu hiyo leo kupanda ndege kuelekea Visiwani Pemba ambapo timu hiyo inakwenda kuweka kambi ikijiwinda na michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.
Akizungumza kabla ya timu hiyo kuondoka  ,Katibu Mkuu wa Coastal Union ,Kassim El Siagi amesema kuwa kocha huyo wa makipa anachukua nafasi iliyokuwa wazi kutokana na kutokuwa na mwalimu maalumu wa kuwafundisha walinda milango wa Coastal Union.
Akizungumzia safari ya timu hiyo, El Siagi alisema kuwa safari ya timu hiyo leo wameondoka  wachezaji 27 wakiaambana na walimu wa timu hiyo ambao wameondoka ambapo watakapofika pemba watafanya mazoezi kwenye uwanja wa soka Gombani.
Safari hiyo imefadhiliwa na wadhamini wa timu hiyo kiwanda cha Pemba Floor Mils kilichopo mjini Tanga ambao wamedhamiria kuhakikisha wanaipa mafanikio timu hiyo.
Katibu huyo amesema wakiwa visiwani humo watacheza mechi nne za majaribio ambazo zilikwisha kutayarishwa na chama cha mpira wa miguu Pemba pamoja na kuwataka mashabiki na wapenzi wa timu hiyo kuacha kuwa na wasiwasi na timu hiyo kwa sababu wamefanya usajili wa nguvu .


Latest transfer insights of “Big 5” football markets revealed in new report from FIFA TMS
MFUMO wa usajili wa elekroniki wa Shirikisho la soka duniani FIFA,  ‘FIFA TMS’ leo ametoa ripoti mpya ukionesha hali halisi ya soka la usajili la kimataifa likizihusisha klabu kutoka nchi za England, Ufaransa, Ujerumani, Italia na Hispania katika majira haya ya kiangazi ya usajili .

Dirisha la usajili litafungwa septemba 1 mwaka huu. Na kwa mataifa haya matano yaliyopo katika soka la usajili kwa kiasa kikubwa, FIFA TMS imetoa ripoti baada ya kupata usajili kwa kiasi kikubwa mpaka sasa.

Ripoti mpya ya sasa inalinganisha usajili wa majira ya kiangazi mwaka huu na miaka mitatu iliyopita katika hatua zilezile. Taarifa kwa kifupi ni kama hapa chini.
·        Ada ya uhamisho ya jumla iliyotumiwa na mataifa matano makubwa majira haya ya kiangazi (mpaka Agosti 12, 2014) ni Dola za kimarekani Bilioni 1.36, ikionekana kukaribiana na mwaka jana (Dola za kimarekani bilioni 1.35).
·        Wastani wa ada ya uhamisho kwa kila mchezaji wa mataifa haya matano inaendelea kukua (Dola za kimarekani milioni 12.1 mwaka 2014 kutoka dola za kimarekani milioni 10.1 mwaka 2013).
·        Klabu za England na Hispania zinaongoza katika soko la usajili, zikichukua asilimia 74 ya matumizi ya jumla ya usajili uliorekodiwa kwa mataifa matano majira haya ya kiangazi.
·        Klabu za Hispania zimezidisha matumizi kwa zaidi ya mara 3.5 kulinganisha na kipindi cha mwaka jana (Dola za kimarekani 491 kutoka dola za kimarekani 139 mwaka 2013).

·        Matumizi ya usajili kwa Ufaransa na Italia yamekuwa yakishuka mwaka kwa mwaka ambapo yameshuka kwa wastani wa 64% kwa mataifa yote mawili.


Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
MAAFANDE wa JKT Ruvu wamekamilisha usajili wa wachezaji watatu kati ya wengi waliokuwa wanafanya majaribio chini ya kocha mkuu, Fredy Felix Minziro.
Beki wa kulia aliyeichezea Simba sc msimu uliopita, Haruna Ramadhan Shamte amesajiliwa na maafane hao na kusaini mkataba mwa mwaka mmoja.
Pia nyota wa zamani wa Simba sc na Azam fc, Jabir Aziz ‘Stima’ ameanguka mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu hiyo yenye nia ya kuonesha changamoto kubwa zaidi msimu ujao.
Katika kuhakikisha lango lake linakuwa mikono salama, klabu hiyo imemsainisha mlinda mlango mzoefu, Jackson Chove mkataba wa mwaka mmoja.
Wachezaji hao watatu walikuwa chini ya uangalizi wa kocha Minziro kwa muda mrefu kwa lengo la kujiridhisha na viwango vyao pamoja na suala muhimu la nidhamu.
Jabir Aziz 'Stima'

Wachezaji wengine waliokuwa wanafanya majaribio na klabu hiyo ni pamoja na Betram Mombeki na Henry Joseph, wote waliachwa na Simba sc mwishoni mwa msimu uliopita.
Pia Athumani Idd ‘Chuji’ alijitokeza mara kadhaa katika mazoezi hayo, lakini aliondoka zake baadaye na sasa anajifua na Mwadui FC ya Shinyanga inayoshiriki ligi daraja la kwanza.
Meneja wa JKT Ruvu, Frank Joel Cibaya aliwahi kukaririwa na mtandao huu akisema wachezaji wengi walioachwa na klabu kubwa za Simba na Yanga wanaomba kufanya majaribio klabuni hapo, lakini kocha Minziro yuko makini zaidi kuangalia nani anamfaa.
Jackson Chove

Cibaya alimtaja Aziz, Shamte na Chove kuwa walionesha juhudi kubwa kwa muda wote wa uangalizi, hivyo kocha amependekeza wasajiliwe rasmi kuitumikia klabu hiyo.
Meneja huyo alisema wachezaji wengi wanaotoka timu kubwa huwa wanasumbua sana wanapojiunga na timu ndogo wakitaka kupata kila kitu walichokuwa wanapata Simba na Yanga.

Dirisha la usajili limeongezwa kwa siku 10  hadi Agosti 27 mwaka huu, hivyo bado maafande wana nafasi ya kuongeza au kupunguza wachezaji wanaoona hawana manufaa kwao.

 

BEKI wa Kimataifa wa Argentina anaechezea Klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno, Marcos Rojo, amethibitisha kuhamia Manchester United.
Akiongea na Redio ya Nchini kwao Argentina, Kituo cha Radio Continental, Marcos Rojo, mwenye Miaka 24, amesema ameshakamilisha Uhamisho wa ‘Ndoto yake’ kwenda Man United.

Jana iliripotiwa kuwa Man United ilikubali kulipa Ada ya Uhamisho ya Euro Milioni 20
kwa ajili ya Rojo na pia kumtoa Winga wao Nani kwenda kwa Mkopo wa Msimu mmoja huko Sporting Lisbon.
Nani alihamia Man United kutoka Sporting Lisbon Mwaka 2007.
Rojo amekaririwa akisema: “Ni kama ndoto kuwa Mchezaji wa Manchester United! Kuhama Sporting haikuwa rahisi!”

Wiki iliyopita mzozo mkubwa ulizuka kuhusu mgao wa Fedha kwa Wamiliki wa Mchezaji huyo mara baada ya Man United kutoa Ofa yao.
Rojo alihamia Sportung Lisbon Mwaka 2012 akitokea Spartak Moscow na Kampuni ya Doyen Sport ililipa Asilimia 75 na Sporting Lisbon kulipa Asilimia 25 ya Ada ya Uhamisho wake.

Nae Rojo aligoma kufanya Mazoezi, na kuadhibiwa na Sporting Lisbon, alipotaka kuruhusiwa kuhamia Man United.

Rojo alicheza Mechi zote za Argentina huko Brazil kwenye Fainali za Kombe la Dunia ambapo Argentina ilifungwa kwenye Fainali Bao 1-0 na Germany na Meneja wa Man United, Louis van Gaal, anamwona Beki huyo ni kiraka kwenye Mfumo wake wa 3-5-2 kutokana na uwezo wake wa kucheza Sentahafu au Fulbeki wa Kushoto.
Beki huyo yumo kwenye Timu ya FIFA ya Fainali za Kombe la Dunia za Brazil 2014.

Kabla kuhamia Spartak Moscow na kisha Sporting Lisbon, Rojo aliichezea Estudiantes ya Argentina na kutwaa Copa Libertadores Mwaka 2009.
Giggs na Van Gaal wakiteta jamboKijana Jesse Lingard tayari ni mgonjwa aliumia Mguu kwenye mechi yao na Swansea juzi

waliotembelea blog