Tuesday, May 26, 2015



Msanii Juma Nature ‘Kiroboto’ akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu tamasha kubwa la kuadhimisha miaka 16 ya kazi zake za muziki nchini pamoja na hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za Kituo cha Redio cha EFM linalofahamika kwa jina la Komaa Concert litakalofanyika kwa mara ya kwanza Jumamosi Ukumbi wa Dar Live Mbagala kuanzia saa 12 jioni.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano wa Kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo, ambao ni waandaaji wa tamasha hilo. Kulia ni Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Microphas Insurance Agency Ltd, Mansoor Kipolelo wa dhamini wa tamasha hilo.

Mkurugenzi wa Idara ya Mahusiano na Mawasiliano wa Kituo cha Redio cha EFM, Denis Ssebo (katikati), akizungumza katika mkutano huo. Kutoka kulia ni Msanii Said Christopher ‘Mucky), Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Microphas Insurance Agency Ltd, Mansoor Kipolelo wa dhamini wa tamasha hilo,Msanii Juma Nature, Msanii, Semani Jabiri ‘Msagasumu’ na Msanii Snura Mushi.

Wasanii watakaotoa burudani la nguvu siku hiyo ya tamasha. Kutoka kulia, Fredy Felix ‘Fredwayne’ Juma Nature, Snura Mushia, na Said Christopher ‘Mucky)

Ofisa Habari wa Kituo cha Redio cha EFM, Lydia Moyo (kushoto), akiperuzi simu yake katika mkutano huo.

Wanahabari wakichukua tukio hilo.



Carlo Ancelotti ametimuliwa kama Kocha wa Real Madrid baada ya kuiongoza kwa Misimu Miwili na kuiwezesha kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI kwa mara ya 10.
Ancelotti, Raia wa Italy mwenye Miaka 55 ambae Mkataba wake na Real ulitakiwa kwisha mwishoni mwa Msimu ujao, Msimu uliopita alileta mafanikio Klabuni hapo kwa kutwaa UEFA CHAMPIONZ LIGI na Copa del Rey na kisha kutwaa Kombe la Klabu Bingwa Duniani lakini Msimu huu wametoka kapa bila Kombe.

Mafanikio pekee ya Real Msimu huu ni toka kwa Mchezaji wao Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, ya kutwaa Pichichi, Tuzo ya Mfungaji Bora La Liga huku Ubingwa wa Ligi hiyo ukienda kwa Mahasimu wao Barcelona.
Carlo Ancelotti ametimuliwa na Klabu ya  Real Madrid baada ya kutoka kapa.
Msimu huu, Real walishindwa kutetea Taji lao la UEFA CHAMPIONS LIGI baada ya kutolewa Nusu Fainali na Juventus ambao sasa watacheza Fainali na Barcelona hapo Juni 6.
Kwenye Copa del Rey walibwagwa nje na Atletico Madrid ambao nao walitupwa nje na Barca ambao Wikiendi hii watacheza Fainali na Athletic Bilbao.
Kwenye La Liga, Kikosi cha Ancelotti kimemaliza Nafasi ya Pili, Pointi 2 nyuma ya Mabingwa Barcelona.
Akitangaza uamuzi wa kumwondoa Carlo Ancelotti, Rais wa Real, Florentino Perez, alisema Jana: "Nini Ancelotti alikosea? Sijui. Ila Klabu hii inadai mambo makubwa. Mapenzi ya Wachezaji na Washabiki kwa Carlo ni makubwa kama vile kwangu kwake!"
Perez ameahidi kutangaza Kocha mpya Wiki ijayo huku Mhispania Rafael Benitez akitajwa sana kuwa mrithi.

Alipokutana na Uongozi wa Bodi ya Klabu ya Real Madrid  Ancelotti leo JumatatuRais wa Real Madrid Florentino Perez ameweka wazi kumtimua kocha wake  Ancelotti leo hii Jumatatu

Perez amekuwa akitimua timua Makocha ndani ya miaka  12kashatimu amakocha tisa


Norwich City Leo hii wamefanikiwa kurudi tena Ligi Kuu England baada ya kuporomoka Msimu mmoja uliopita baada ya kuichapa 2-0 Middlesbrough
kwenye Fainali ya Mchujo wa Timu 4 za Daraja la Championship iliyochezwa Uwanjani Wembley Jijini London.
Mbele ya Watazamaji 85,656, Norwich City walipiga Bao zao 2 ndani ya Robo Saa ya Kwanza kwa Bao za Cameron Jerome alietumia vyema makosa ya Daniel Ayala na kufunga na kisha katika Dakika ya 15 Nathan Redmond alipiga Bao la Pili.

Norwich City, ambao walimaliza Ligi ya Championship Nafasi ya 3 na hivyo kukosa nafasi ya kupanda Ligi Kuu England moja kwa moja, kwenye Nusu Fainali ya Mechi hizi za Mchujo waliibwaga Ipswich Town Jumla ya Mabao 4-2 katika Mechi mbili.Boro walitinga Fainali hii kwa kuichapa Brentford Jumla ya Mabao 5-1 katika Mechi mbili.
Norwich City sasa wameungana na Bournemouth na Watford, ambazo zilimaliza Nafasi mbili za juu za Ligi ya Championship na kupanda Daraja moja kwa moja, kucheza Ligi Kuu England Msimu ujao kuzibadili Hull City, QPR na Burnley zilizoporomoka Daraja.
Mashabiki wa BoroTimu zikiingia Uwanjani WembleyKikosi cha NorwichKipute kimeanza ...mchezaji wa Boro chiniJerome ndie aliyeanza kufunga bao la kwanzaJerome akishangilia bao lake la kwanzaMeneja wa Noewich Alex Nail akishangilia naeNathan Redmond alipachika bao la piliWafungaji wakakutana live Nathan na JeromeWachezaji wa Boro hoi!! Mashabiki nao wakazimika!!Taswira Meneja wakiwajibika Uwanjani!Jerome alipumzishwa!

Mabingwa wapya wa England, Chelsea, Leo wamezunguka Mitaa ya London ya Magharibi wakiwa juu ya Basi la Ghorofa la wazi wakiwa na Kombe lao la Ubingwa wa Ligi Kuu England pamoja na Vikombe vingine Vitatu ambavyo Klabu hiyo ilitwaa Msimu huu.
Chelsea wametwaa Ubingwa huu wa England kwa mara ya kwanza baada ya Miaka Mitano.
Baada ya Jana kukabidhiwa Kombe la Ubingwa na kufanya sherehe Usiku kucha Leo wamezungukana Mitaa ya London huku Washabiki wakisimama kando kando na kuwashangilia.
Juu ya Basi hilo la Ghorofa la wazi walikuwemo Wachezaji wa Timu ya Kwanza ya Chelsea wakiwa na Kombe la Ligi Kuu England na lile la Capital One Cup pamoja na wa Timu ya Vijana ambao nao walikuwa na Kombe la Vijana la FA na lile la Vijana la Ligi ya UEFA.
Didier Drogba na Fabrigas wakipeta na Mwali wao mpyaDiego Costa na FabrigasDrogba na raha zake na Mwali mkononi!Drogba akiwaonesha Mashabiki Kombe lao wakati wa matembezi hayo leo hii jumatatu!Taswira kamiliKwenye mitaa ya LondonKepteni john terryMeneja Jose nae aliwapungia mkono Mashabikikwenye Mitaa


West Ham ilikubali kichapo kwenye mtanange wa kumalizia Msimu wa Ligi Kuu England 2014-2015 ambapo West Ham ilichapwa 2-0 huko Saint James Park na Newcastle ambao ushindi huo umewabakisha Ligi Kuu England, Klabu ya West Ham imetangaza kusaka Meneja mpya baada kuamua kutoongeza Mkataba wa Meneja wao Sam Allardyce.
Allardyce, maarufu kama Big Sam, alijiunga na West Ham 2011 wakati Timu hiyo iko Daraja la chini la Championship na kuirudisha Ligi Kuu England na Msimu huu walianza vizuri tu lakini mwishoni walififia na kumaliza Nafasi ya 12.
Wenyeviti wenza wa West Ham, David Sullivan na David Gold, wametoa shukran zao kwa Allardyce na pia kutamka kuwa wanayo Listi ya Watu wanaofaa kushika wadhifa huo wa Meneja.
Akiongea mara baada ya Mechi hiyo, Big Sam alisema uamuzi huu ni bora kwa kila upande.

West Ham ilikubali kichapo kwenye mtanange wa kumalizia Msimu wa Ligi Kuu England 2014-2015 ambapo West Ham ilichapwa 2-0 huko Saint James Park na Newcastle ambao ushindi huo umewabakisha Ligi Kuu England, Klabu ya West Ham imetangaza kusaka Meneja mpya baada kuamua kutoongeza Mkataba wa Meneja wao Sam Allardyce. Ametamka: "Nadhani ni sahihi kwa kila upande, kwangu na Klabu. Nilitimiza kila kitu walichonitaka, na nilifurahia hilo!"

waliotembelea blog