Friday, September 12, 2014


 
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
YANGA SC itakutana na Azam fc katika mchezo mkali wa Ngao ya Jamii kuashiria kupenuliwa kwa pazia la ligi kuu soka Tanzania bara jumapili (septemba 14 mwaka huu) uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam.
Kuelekea katika mchezo huo, mshambuliaji Jeryson Tegete hayuko fiti kucheza kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya nyonga.
Mbali na nyota huyo mzaliwa wa Mwanza, mshambuliaji mwingine wa Yanga, Mbrazil, Andrey Coutinho yupo hatarini kukosa mechi hiyo kutokana na majeruhi ya mguu aliyoyapa jumatano ya wiki hii katika mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Dar es salaam.
Mechi hiyo iliyomalizika kwa suluhu pacha ya bila kufungana ilipigwa uwanja wa Shule ya Sekondari, Loyola, Mabibo jijini Dar es salaam.
Kwa sasa Yanga wameweka kambi katika Hoteli ya Tansoma, iliyopo eneo la Gerezani, Dar es salaam.
Baada ya Coutinho kuumia siku hiyo, leo hii Polisi Dar wamesikitishwa na majeruhi hayo  na kumuombea dua njema ili awe fiti kwa ajili ya mechi ya keshokutwa uwanja wa Taifa.
Kocha na mratibu wa Polisi Dar, Kennedy Mwaisabula ‘Mzazi’ kwa niaba ya klabu hiyo amemtakia afya njema Coutinho akimuombea apone haraka.
“Kama kocha na mratibu wa Polisi Dar,  kwa niaba ya timu yetu tunamtakia afya njema na apone haraka Andrey Coutinho mchezaji wa Yanga,  Raia wa Brazil aliyeumia kwa bahati mbaya mno dhidi ya  mechi yetu siku ya jumatano.” Amesema Mwaisabula dakika chache zilizopita kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii ya facebook.
Coutinho ameonekana kuwateka mashabiki wa Yanga kwa uwezo wake wa kupiga mashuti ya mbali, kumiliki mpira, kupiga mipira ya adhabu ndogo na kupiga pasi za uhakika.
Nyota huyo amemzidia kete, Mbrazil mwenzake, Geilson Santos Santana ‘Jaja’ ambaye mpaka sasa hajakubalika miongoni mwa mashabiki wa Yanga wakidai ni mzito sana anapokuwa uwanjani.


Daniel Sturridge is out for three weeks after getting injured during training on England duty
Daniel Sturridge atakaa nje ya uwanja kwa wiki tatu baada ya kupata majeruhi katika mazoezi ya England

BRENDAN Rodgers ameponda matibabu wanayotoa England kwa mshambuliaji wake Daniel Sturridge baada ya kupata majeruhi ya mguu.
Sturridge aliumia ijumaa iliyopita, saa 48 baada ya kucheza dakika 89 katika ushindi wa England wa bao 1-0 dhidi ya Norway katika mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Nyota huyu alikosa mechi ya kuwania kufuzu Euro 2016 dhidi ya Uswizi ambapo England ilishinda mabao 2-0 na sasa yuko nje ya uwanja kwa wiki tatu.
Rodgers amechukia sana kwasababu mshambuliaji wake hakupewa muda mzuri wa kupumzika.
"Tumekatishwa tamaa sana kwasababu tunadhani majeruhi yake ingetibiwa haraka," Bosi wa Anfield alisema.

Daniel Sturridge's thigh strain in camp with the national team could have been avoided, says Brendan Rodgers+5
Daniel Sturridge amemtia hasara kocha wake Brendan Rodgers
Daniel Sturridge shows his skills in training for England against Phil Jones just before going down injured
Daniel Sturridge akionesha ufundi wake katika mazoezi ya England dhidi ya Phil Jones kabla ya kuumia


Oscar Pistorius has been found GUILTY of the manslaughter of girlfriend Reeva Steenkamp
Oscar Pistorius amekutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp

MWANARIADHA  Oscar Pistorius anakabiliwa na kifungo gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.
Jaji wa mahakamu kuu ya Afrika kusini, Thokozile Masipa mapema laisema siku ya wapendanao 'Valentine Day' mwaka jana, Pistorius alimpiga risasa mpenzi wake huyo.
Mara zote Pistorius amekuwa akikiri kuhusika na kifo chake nyumbani kwake mjini Pretpria, lakini alisema hakukusudia kumpiga risasi mpenzi wake na  alimpiga risasi nne kwa bastola yake.
Oscar Pistorius arriving in the dock as he awaited the second day of his verdict
Oscar Pistorius akiwasili mahamani siku ya pili leo kujibu mashitaka yake 

Judge Thokozile Masipa declaring that Pistorius was found not guilty for premeditated murder on Thursday+11
Jaji Thokozile Masipa akitangaza kuwa Pistorius hajakutwa na hatia ya kuuza kwa kukusudia jana alhamisi.

Mwanariadha huyo alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuua kwa kukusudia, lakini ushindi juu ya hilo haukujitosheleza.
Kwa mara ya pili leo, Pistorius  alisimama kizimbani kujibu shitaka lake, lakini hakuonekana kuwa na hisia zozote.
Jaji Masipa aliiambia mahakama: " Kwa kuzingatia ushahidi wote uliowasilishwa katika mahakama: Kosa la kwanza, muuaji hajakutwa na hatia ya kuua kwa kukusudia na anaachiwa huru kwa hilo".
"Badala yake amekutwa na hatia ya kuua"

waliotembelea blog