Wednesday, August 5, 2015

LIP1
Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wafuasi wa chama hicho waliojitokeza katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Buguruni jijini Dar es salaam,na kuwaambia kuwa CUF ni Taasisi,hivyo wanachama wote wanatakiwa kukijenga chama hicho wawe na vyeo ama wasiwe na vyeo kazi kubwa ni kukijenga chama cha CUF,Pro Lipumba aliyasema maneno hayo bila kutoa ufafanuzi wa kina.

Profesa Lipumba alitakiwa kuzungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya chama hicho,lakini mpaka dakika za mwisho hakufanya mkutano huo badala yake alikuwa na kikao na wazee wa chama hicho na baadhi ya viongozi wa dini na wanachama,aidha wakati akiondoka katika ofisi hizo ndipo akazungumza maneno hayo hakuyafafanua zaidi.
LIP2
Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba akisisitiza jambo wakati akizungumza na baadhi ya wanahabari katika makao makuu ya CUF Buguruni jijini Dar es salaam
LIP3
Baadhi ya wanachama wa chama cha CUF wakiwa katika makao makuu ya chama hicho wakipiga kelele kuashiria kumuunga mkono mwenyekiti wao Profesa Ibrahim Lipumba.
LIP4
Wana CUF wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika makao makuu ya chama hicho Buguruni kumsikiliza Mwenyekiti wao Profesa Ibrahim Lipumba 
LIP5
Mpiga Picha wa Gazeti la Uhuru Emmanuel Ndege akisaidiwa na waandishi wenzake mara baada ya kujeruhiwa na feni wakati waandishi hao wakisubiri Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba kuzungumza nao katika makao makuu ya chama hicho Buguruni.PICHA KWA HISANI YA FULLSHANGWE BLOG.
 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jami.
 
MWENYEKITI wa Taifa wa  Chama Cha Wananchi (CUF),amewataka wanachama wa  chama hicho kukijenga kwa nafasi walizonazo iwe kiongozi au mwanachama wa kawaida.
 
Lipumba ameyasema hayo wakati akizungumza na wanachama waliofika katika ofisi ya makao makuu ya chama hicho wakitaka kauli ya yake juu ya chama na taarifa zilizopo katika mitandao juu ya kutaka kuachia nafasi yake uenyekiti wa chama hicho.
 
Lipumba  amesema kuwa chama ni taasisi sio chama mtu mmoja anaweza kufanya kila kitu hivyo wanachama tambueni hivyo.
 
Aidha amewataka wanachama waisome katiba ya chama hicho kwa sababu zipo ili kuweza kujua chama jinsi kinavyoendeshwa kutokana na katiba ambayo inapitishwa na wanachama.
 
Wakati huo huo  mkutano ulitishwa na chama hicho kwa lengo la Mwenyekiti wa Chama hicho Profesa,Ibrahim Lipumba umearishwa kutokana na wazee wa chama hicho kuvamia Ofisi hiyo na kwenda kuzungumza na mwenyekiti wa chama hicho.
 
Akizungumza wakati kuarisha Mkutano huo Mwenyekiti wa Naibu Katibu Mkuu Bara,Magdalena Sakaya amesema kuwa mkutano huo ulikuwa wa mwenyekiti Lipumba lakini wazee wa chama wamevamia hivyo hawezi kuzungumza tena.
 
Sakaya amesema kitu ambacho alikuwa anataka kuzungumza anajua mwenyewe hivyo haiwezekani mtu mwingine azungumze kitu cha mwenyekiti.
 
“Jamani tunaahirisha mkutano wetu ambao ulitakiwa kuzungumzwa na mwenyekiti lakini wazee wa chama wamevamia ofisi na kuwa na mazungumzo na mwenyekiti”amesema Sakaya Naibu Katibu Mkuu Bara.




Timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) inatarajiwa kuingia kambini kesho kisiwani Zanzibar kujiandaa na Fainali za Michezo ya Afrika (All Africa Games) zitakazofayika mwezi Septemba mwaka huu nchini Congo Brazzavile.

Kikosi hicho cha wachezaji 25 chini ya Kocha Mkuu Rogasian Kaijage, tayari kimeanza mazoezi kujiandaa na michuano hiyo ambapo Tanzania ilikata tiketi ya kushiriki fainali hizo baada ya kuiondoa Zambia kwa jumla ya mabao 6-5.

Twiga Stars inaingia kambini  kwa gharama za TFF, huku jitihada za TFF kuwasiliana na Kamati ya Olimpiki nchini (TOC) zikiendelea kuona ni jinsi gani kamati hiyo inaihudumia timu hiyo ya Taifa kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo ya Michezo Afrika.

TFF inatambua TOC ndio wana jukumu la kuhudumia timu za Taifa kuelekea kwenye michuano hiyo ya Michezo ya Afrika ikiwemo Twiga Stars.

Twiga Stars ambayo imefuzu kwa Fainali za Michezo ya Afrika itakayoanza kutimua vumbi Septemba 04 – 17 imepangwa kundi A na wenyeji Congo Brazaville na Nigeria pamoja na Ivory Coast.


barca
Kiungo raia wa Argentina Javier Mascherano ameteuliwa kuwa nahodha wa nne kwenye klabu ya Barcelona akiongeza idadi ya manahodha ambayo ilikuwa imebakia manahodha watatu baada ya kuondoka kwa Xavi Hernandez.
Kuondoka kwa Xavi Hernandez kumefungua nafasi moja ya unahodha baada ya kupandishwa kwa Andres Iniesta ambaye amekuwa nahodha wa kikosi cha kwanza huku Lionel Messi akiwa nahodha wa pili na Sergio Busquets akiwa nahodha wa tatu.
Kocha wa Barcelona Luis Enrique amemzungumzia Mascherano kama mchezaji ambaye ana sifa ya uongozi hata kama sio nahodha rasmi kwenye timu na kwa sababu hii ana kila sifa ya kuwemo kwenye orodha ya manahodha wa klabu.
Enrique ameongeza kuwa Mascherano ni mchezaji ambaye timu nzima inamheshimu na hivyo ni uchaguzi ambao haukuwa na pingamizi toka kwa wachezaji wengine.



Kevin De Bruyne kutua Man CityPedro kwenda Man United?




Wachezaji mpira ni miongoni mwa watu maarufu sana kutokana na kazi yao kupendwa au kuwa na mashabiki wengi kutoka sehemu mbalimbali, miongoni mwa vitu ambavyo huwezi kuvidhania kama unaweza kuviona kwa mastaa wako wa soka ambao umezoea kuwaona wakiwa katika muonekano uliozoeleka kuonekana labda wakiwa katika mechi au matukio ya kawaida.
Katika pitapita zangu mtandaoni nimekutana na hii list ya mastaa wa soka waivyoamua kujiachia kwa vioja kabisa.
Dani Alves
download (1)
Dani Alves aliwahi kuvaa wigi wakati akisherehekea ushindi wa Timu yake ya Taifa
Andrey Arshavin
download (2)
Ni mchezaji wa zamani wa Arsenal anatajwa kuwa sio miongoni mwa watu wanaouchukulia mchezo wa mpira wa miguu serious.. Ndani ya Uwanja akaona afanye kioja kupindisha uso wake.
Mario Balotelli
download (3)
Chochote anachokifanya Balotelli huwa hakiko mbali na headlines za Waandishi wa Habari.
Antonio Cassano
download (4)
Antonio Cassano akishangilia ushindi wa goli 2-0 Italy ilivyoifunga Ufaransa katika michuano ya Euro 2008.
Zlatan Ibrahimovic
download (6)
Zlatan Ibrahimovic wakati alipovua nguo Uwanjani bila hofu kabisa.
Stephen Ireland
download (7)
Kiungo wa zamani wa klabu ya Manchester City Stephen akishangilia goli kwa staili ya kuvua bukta
David Luiz
download (8)
David Luiz beki ghali wa klabu ya PSG ya Ufaransa akishangilia goli

waliotembelea blog