Saturday, November 15, 2014

unnamed.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  akisindikizwa na Daktari Bingwa
Edward Schaeffer kutoka
Hospitali ya Johns Hopkins alipokuwa amelazwa baada ya kufanyiwa
upasuaji wa kuondoa tezi dume mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya

kupata nafuu.Kulia nia Mke wa Rais Mama Salma Kikwete. Hali ya Rais
Kikwete imezidi kuimarika baada ya kutoka wodini na kuwa mapumzikoni
akiuguza kidonda kilichotokana na upasuaji aliofanyiwa, kabla ya
kwenda kuondolewa nyuzi siku chache zijazo. Huku akiendelea kufanya
mazoezi kila siku, Rais Kikwete pia ameendelea kupokea salamu za
Watanzania kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kila pembe ya dunia
pamoja na salamu za kumtakia nafuu mapema kutoka kwa viongozi
mbalimbali wakiwemo mabalozi na wawakilishi wa nchi za nje. Naye
amekuwa akizijibu kwa kadri anavyoweza.
1Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Daktari Edward Schaeffer
muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya Johns
Hopkins huko Baltimore, Maryland nchini Marekani ambapo alifanyiwa
upasuaji wa kuondoa tezi dume mwishoni mwa wiki iliyopita. Hali ya

Rais Kikwete imezidi kuimarika baada ya kutoka wodini na kuwa
mapummzikoni akiuguza kidonda kabla ya kwenda kuondolewa nyuzi siku
chache zijazo. Huku akiendelea kufanya mazoezi kila siku, Rais Kikwete
pia ameendelea kupokea salamu za Watanzania kwa njia ya ujumbe mfupi
(SMS) kutoka kila pembe ya dunia pamoja na salamu za kumtakia nafuu
mapema kutoka kwa viongozi mbalimbali wakiwemo mabalozi na wawakilishi
wa nchi za nje. Naye amekuwa akizijibu kwa kadri anavyoweza




Wafanyakazi wa Kampuni ya Mafuta ya ENGEN Tanzania leo Novemba 14,2014 wameungana na wafanyakazi wenzao Barani Afrika kusherehekea Maadhimisho ya Miaka 21 ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo,ambayo husherehekewa kila Mwaka ifikapo tarehe kama ya leo.Engeni ni Kampuni iliyojikita katika uuzaji wa Mafuta bora ndani na nje ya Tanzania,huku ikiendelea kujivunia kwa Ubora wake.Pichani ni Sehemu ya Wafanyakazi wa Kampuni hiyo ya Engen hapa nchini wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya jengo lao Kurasini jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya ENGEN Tanzania,Mubita Akapelwa (wa pili kulia) akikata keki wakati wa Kusherehekea Miaka 21 ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo,ambayo husherehekewa kila Mwaka ifikapo tarehe kama ya leo,iliyofanyika kwenye Makao Makuu ya Ofisi za Kampuni hiyo,Jijini Dar es Salaam.Katikati ni Meneja Masoko wa Kampuni hiyo,Shaaban Kayungilo.

Meneja Masoko wa Kampuni hiyo,Shaaban Kayungilo akichua kipande cha Keki iliyokatwa vyema na Dada Jullieth Lwato (alieshika sahani) wakati wa Kusherehekea Miaka 21 ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo,ambayo husherehekewa kila Mwaka ifikapo tarehe kama ya leo,iliyofanyika kwenye Makao Makuu ya Ofisi za Kampuni hiyo,Jijini Dar es Salaam.


Rais wa shirikisho la soka barani afrika Issa Hayatou
Taifa la Equitorial Guinea ndilo litakaloandaa michuano ya dimba la mataifa ya Afrika mwaka 2015.
Kulingana na shirikisho la soka barani Afrika, taifa hilo limetajwa baada ya Morrocco kukataa kuandaa michezo hiyo kutokana na hofu ya kusambaa kwa ugonjwa wa Ebola nchini humo.
Morrocco ilikuwa imeiomba CAF kuahirisha dimba hilo la January 17 hadi Feruary 8.
CAF vilevile imeipiga marufuku Morrocco kushiriki katika dimba hilo ambalo sasa litaandaliwa na taifa lililoandaa kombe hilo na Gabon mwaka 2012.
Kombe la michuano ya bara Afrika
Equitorial Guinea sasa itachukua jukumu lote la kuandaa michuano hiyo yenye mataifa 16.
CAF imetangaza kuwa mechi hizo zitachezwa katika miji minne ikiwemo Malabo,Mongomo na Ebebiyin. Droo ya mechi hizo itafanyika mjini Malabo tarahe 3 mwezi Disemba.

Haijabainika iwapo mwenyeji huyo mpya atashiriki katika dimba hilo kwa kuwa timu hiyo ilipigwa marufuku mwezi Julai kwa kuchezesha mchezaji asiyetakikana katika mechi ya kufuzu kwa dimba hilo dhidi ya Mauritania mnamo mwezi May 17.

A file picture taken on October 29, 2011 shows Equatorial Guinea President Teodoro Obiang Nguema holding the trophy of the African Nations football Cup during the draw ceremony in Malabo. The African Cup of Nations (CAN 2015) will be held in Equatorial Guinea an announcement was made on November 14,2014.


AFCON 2015
MECHI ZA MAKUNDI

RATIBA/MATOKEO:
Ijumaa Novemba 14

Sierra Leone 1 vs Ivory Coast 5 
Botswana 0 vs Tunisia 0

Jumamosi Novemba 15
15:30 Malawi v Mali 
16:00 South Africa v Sudan 
16:00 Uganda v Ghana 
16:30 Togo v Guinea 
17:00 Cape Verde v Niger 
17:00 Cameroon v DR Congo 
17:00 Lesotho v Burkina Faso 
17:00 Mozambique v Zambia 
17:30 Congo v Nigeria 
18:00 Angola v Gabon 
20:00 Egypt v Senegal 
22:30 Algeria v Ethiopia  

Jumatano Novemba 19
16:00 Senegal v Botswana 
17:00 Ethiopia v Lesotho  
17:00 DR Congo v Sierra Leone  
17:00 Gabon v Lesotho  


David Moyes, Meneja alietimuliwa Manchester United Mwezi Aprili Mwaka huu, ametua rasmi huko San Sebastián Nchini Spain kujiunga na Real Sociedad kama Meneja wao mpya.

Mara baada ya kutua kwenye Klabu hiyo ya La Liga ambayo Jina lake la ubatizo ni La Real, Moyes alikiri kuwa kabla hajakubali rasmi kujiunga na Real Sociedad alimtaka ushauri Sir Alex Ferguson ambae alimbariki kuchukua nafasi hiyo.

Feguson, ambae alistaafu kuwa Meneja wa Man United Mei Mwaka Jana baada ya himaya ya Miaka 26 na kubakia hapo kama Mkurugenzi, ndie aliependekeza mrithi wake awe David Moyes.

Akikiri kuwa hadi hii leo ni marafiki, Moyes alieleza: “Niliongea na Sir Alex na akaniambia hii ni nafasi nzuri.”

Moyes pia alikumbushia himaya yake ya Miezi 10 Old Trafford na kusisitiza hakupewa muda wa kutosha.

Moyes, ambae kabla ya kujiunga Man United alikuwa Meneja wa Everton, amesisitiza ni ngumu kwa Mtu yeyote kumrithi Sir Alex Ferguson.
Lakini pia Moyes amesema uzoefu wake na Man United utaisaidia sana Real Sociedad.
Huko Real Sociedad Moyes anambadili Jagoba Arrasate aliefukuzwa Wiki 2 zilizopita baada ya matokeo mabovu ambayo yameifanya Klabu hiyo iwe Nafasi ya 15 kwenye La Liga.
Moyes amesaini Mkataba hadi Juni 2016 na Mechi yake ya kwanza kama Meneja ni hapo Novemba 22 watakapocheza ugenini Mechi ya La Liga na Deportivo La Coruna.

Kwa Real Sociedad Moyes anakuwa Meneja wa nne kutoka Uingereza katika historia yao na wengine waliowahi kuongoza Klabu hiyo ni Harry Lowe aliekaa huko Miaka 5 kuanzia 1930, John Toshack aliekaa kwa vipindi vitatu tofauti na Chris Coleman alieteuliwa Julai 2007 na kudumu Miezi 7 tu.

Msimu huu kwenye Ligi, licha ya kusuasua, Real Sociedad tayari wamewafunga Vinara wa La Liga, Real Madrid, na Jumapili iliyopita kuwatwanga Mabingwa Watetezi Atletico Madrid Bao 2-1.




Pichani Kutoka kushoto ni Bella Kombo akiongoza mashambulizi ya jukwaa akipewa sapoti na Digna Mbepera(katikati) na kwa mbaliiiii ni Aneth kushaba.Kama kawaida yetu inapofika mwishoni mwa juma yaani Ijumaa huwa inakuwa ni siku ya furaha na kubadilishana mawazo, kupunguza stress za kazini.....paleee Thai Village Masaki.Kwenye Jukwaa Bendi yako matata na inayotikisa Tanzania na Jiji la Dar Skylight Band wanakuwa wanakupa burudani ya nguvu na iliyoenda shule.Karibu leo kuanzia saa 3 kamili usiku upate zile Afropop, Zouk, Lingala,Sebene, Reggae, Naija Flava na zingine kibao!

Aneth Kushaba AK 47 akizipiga vocal za kutoshaaaa ili kuwapa burudani wapenzi wa Skylight Band ndani ya Thai Village Ijumaa iliyopita.

Bella Kombo akitia madaha yake na swagga kibao ndani ya Thai Village.

Digna Mbepera (Mtoto Mzuri) akiimba kwa hisia kali kuwapa ladha wapenzi wa Skylight band ndani ya Thai Village
Anaitwa Hashimu Donode mkali wao akizipiga zile vocal kaliiii na tamuuu kuwapa raha mashabiki wake ndani ya Thai Village

Wanamwita tamu ya warembo au Sukari ya warembo si mwingine ni Sam Mapenzi akizipiga zile Vocal lainiii za taratibu kuwapa raha mashabiki wake ndani ya Thai Village

Muziki ni hisia na hapa ndicho anachokifanya Aneth Kushaba hebu mtazame anavyoimba kwa hisia kali na Vitendo ili kuwapa raha mashabiki wake huku akipewa sapoti kwa mbaliiii na Digna Mbepera(katikati) na Bela Kombo wa mwisho kushoto.

Mikono kichwaniii,ahhh ahhhh majembe ya Skylight wakishambulia jukwaa kwa nguvuuuu

Joniko Flower baba ya congo akiongoza kushambulia huku akipewa sapoti na Sony Masamba(katikati) pamoja na Sam Mapenzi.

Mtia ladhaa mahiri wa Skylight akiwa anasahangaa kupata Ukodak kutoka kwa mpiga picha wetu,Huku mpiga drums Idrisa akichunguliaaa kwa mbaliiiii

Huyu jamaa ni muhimu sanaaa ndani ya Sklight Band anaitwa Daudi Tumba,akizipiga Tumba zake lazima ufurahie

waliotembelea blog