Saturday, April 11, 2015


LA LIGA - RATIBA
Jumamosi Aprili 11

17:00 Real Madrid CF vs SD Eibar
19:00 Malaga CF vs Atletico de Madrid
21:00 Sevilla FC vs FC Barcelona
23:00 Celta de Vigo vs Rayo Vallecano
23:00 UD Almeria vs Granada CF 


Jumapili Aprili 12
13:00 Getafe CF vs Villarreal CF
18:00 RCD Espanyol vs Athletic de Bilba
20:00 Real Sociedad vs Deportivo La Coruna
22:00 Cordoba CF vs Elche CF
 

Jumatatu Aprili 13
21:30 Valencia C.F vs Levante



Wachezaji wa Manchester United wakijifuia leo Ijumaa tayari kwa Dabi yao ya Jumapili na Manchester City

Meneja Louis van Gaal akiangalia Vijana wake wanavyojituma kwenye mazoezi leo hii
Kipa David de Gea, Angel di Maria na Straika Radamel Falcao kwenye mazoezi leo

Straika Robin van Persie ameshatangaza kwa wadau kwamba katika kipute hicho cha Manchester atakuwepo na anategemea kucheza mchezo huo dhidi ya Manchester City
Falcao na Antonio Valencia
Nahodha wa Man United kwa sasa Rooney kuiongoza Debi hiyo Siku ya Jumapili dhidi ya City

Van Gaalakitathimini mazoezi hayo na akijiuliza juu ya mchezo huo wenye Upinzani mkali

Rooney, Ashley Young, goalkeeper Anders Lindegaard na Michael Carrick
NAHODHA wa Manchester United Wayne Rooney ameieleza Dabi ya Manchester ya Jumapili hii kuwa ni Gemu kubwa ya kuleta kiburi. Jumapili, Manchester United watakuwa kwao Old Trafford kuwakaribisha Mahasimu wao kwenye Mechi ya Ligi Kuu England ambayo inazikutanisha Man United iliyo Nafasi ya 3 Pointi 1 mbele ya City ambayo iko Nafasi ya 4.
Rooney, ambae ameshapiga Bao 11 kwenye Dabi ya Manchester akishikilia Rekodi ya Kihistoria ya kufunga Bao nyingi kwenye Dabi hii, amesema anataka Mashabiki wa Man United wakienda Makazini kwao Jumatatu wawacharure wale wa City.
Lakini hivi karibuni City ndio wamekuwa wakiiburuza United kwa kushinda Mechi 4 mfululizo ingawa Kihistoria hakuna hata Timu moja iliyowahi kuifunga Man United mara 5 mfululizo.
Baada ya kuwapiga nje ndani Mahasimu wao wengine LIverpool, Man United, chini ya Meneja Louis van Gaal, hivi sasa ni moto na Rooney ameazimia kudumisha hilo.

Akiongea na MUTV, Kituo cha TV cha Man United, Rooney alisema: "Hii ni Gemu muhimu kwa Manchester United na Manchester City...na kwa Mashabiki na kwangu mimi ni Gemu kubwa ya kuleta kiburi. Ukichezea Man United unataka ushinde Gemu hizi za Dabi!"
Aliongeza: "Tunataka tuwape Mashabiki wa United kitu cha kufurahia wakienda kazini JUmatatu, tunataka wao ndio wawacharure Mashabiki wa City huko kazini!"KUKUTANA USO KWA USO
-Manchester United: Ushindi Mechi 59
-Manchester City: Ushindi Mechi 49
-Sare: Mechi 50
-Jumla: Mechi 168

waliotembelea blog