Wednesday, November 4, 2015


Stori kuhusu bondia wa kitanzania Francis Cheka kusafiri kwenda Manchester Uingereza kupambana na bondia wa kiingereza zimezidi kuchukua headlines kutokana na safari yake kutoeleweka. Cheka aliripotiwa kusafiri kwenda Uingereza kwa zaidi ya wiki kadhaa nyuma lakini safari yake imekuwa ikihairishwa mara kwa mara.
Siku kadhaa nyuma meneja wa bondia huyo Juma Ndambile alifanya mahojiano na gazeti la The Citizen na kuthibitisha bondia huyo, kuwa yupo katika mpango wa kwenda Uingereza kupambana katika pambano lisilo la Ubingwa na bondia wa kiingereza licha ya kuwa hakuwa amewekwa wazi ila Juma alikiri kuwa bondia wake yupo tayari kupambana na bondia yoyote.
chekabc
November 4 pambano hilo limeingia katika headlines kwa mara nyingine baada ya Francis Cheka kushindwa kusafiri kutokana na sababu ambazo hata Cheka hajui kwa nini pambano hilo limekuwa likihairishwa kwa zaidi ya mara tatu na bado hapokea tiketi ya safari hiyo.
“Sifahamu ni kitu gani kinaendelea, hii mechi imekuwa ikihairishwa kama mara nne sasa siwezi kujua nini hao waingereza wanakusudia lakini sijui labda wanahofia kwa sababu mabondia wao wengi nimewahi kupigana nao na kuwapiga, Labda kuna mtu yupo Tanzania anatoa taarifa kuwa Cheka yuko vizuri hivyo mechi muhairishe” >>> Cheka
David Alaba celebrates after scoring the third goal for Bayern Munich Dakika ya 55 kipindi cha pili Arjen Robben aliipa bao la nne Bayern na kufanya matokeo kuwa 4-0 dhidi ya Arsenal baada ya kupokea mpira kutoka kwa David Alaba. Bao la Arsenal limefungwa na Olivier Giroud dakika ya 69 na kufanya 4-1. Thomas Müller aliandika bao la tano dakika ya 89 na mtanange kumalizika kwa 5-1 dhidi ya Arsenal.4-0Robert Lewandowski akishangilia bao lake.David Alaba dakika ya 44 aliipachikia Bayern bao la tatu na kufanya mtanange kwenda mapumziko kwa 3-0 dhidi ya Timu ya ArsenalMenenja wa Arsenal, Arsene WengerRobert Lewandowski dakika ya 10 kaifungia bao la kuongoza Bayern Munich kwa kufanya 1-0 dhidi ya Arsenal, Bao la pili kalifunga Thomas Müller dakika ya 29 baada ya kupata mpira ktoka kwa Kingsley Coman.Akitupia nyavuni..Kikosi cha Bayern kilichoanza dhidi ya Arsenal usiku huu OzilVIKOSI:
Bayern Munich:
Neuer, Lahm, Boateng, Javi Martinez, Alaba, Alonso, Coman, Muller, Thiago, Douglas Costa, Lewandowski.
Akiba: Ulreich, Benatia, Robben, Rafinha, Badstuber, Vidal, Kimmich.
Arsenal: Cech, Debuchy, Mertesacker, Gabriel, Monreal, Coquelin, Cazorla, Campbell, Ozil, Sanchez, Giroud.
Akiba: Macey, Gibbs, Koscielny, Flamini, Chambers, Iwobi, Reine-Adelaide.
Refa: Gianluca Rocchi (Italy)



 Neymar akishangilia bao lake baada ya kufanya 3-0

Luis Suarez nae alifanya 2-0 hapa

Mtu kati

Neymar akitupia...

Neymar aliruka juu baada ya kufunga bao la kwanza kwa mkwaju wa penati

Mashabiki wa Barca wakiwa na bendera zao

Taswira

Ndani ya box


Javier Mascherano akichuana vikali na Mikhail Gordeichuk leo kwenye Uefa(Klabu Bingwa Ulaya)
Neymar dakika ya 30 kaifungia bao Barcelona kwa mkwaju wa penati.
Mbele ya Mashabiki 68502

Neymar 30' PEN
Luis Suárez 60'
Neymar 83' 


 VIKOSI:
Barcelona:
Ter Stegen, Dani Alves, Mascherano, Vermaelen, Adriano, Rakitic, Busquets, Sergi Roberto, Suarez, Iniesta, Neymar.
Akiba: Bravo, Pique, Bartra, Munir, Jordi Alba, Sandro, Gumbau.

BATE: Chernik, Palyakow, Hayduchyk, Milunovic, Mladenovic, Stasevich, Alyaksandr Valadzko, Yablonskiy, Maksim Valadzko, Gordeichuk, Mozolewski.
Akiba: Soroko, Dubra, Karnitskiy, Nikolic, Jevtic, Ryas, Hleb.


Chelsea 2-1 Dynamo Kiev: Willian scores stunning free-kick to rescue crucial ChampionsAleksandar Dragovic dakika ya 77 aliisawazishia bao na kufanya 1-1 dhidi ya Chelsea baada ya mchezaji huyo huyo kuwapa bao la zawadi Chelsea kwa kujifunga katika kipindi cha kwanza dakika ya 34.VIKOSI:
Chelsea:
Begovic; Azpilicueta, Zouma, Terry, Baba Rahman; Ramires, Matic; Willian, Fabregas, Oscar; Diego Costa.
Akiba: Blackman, Cahill, Loftus-Cheek, Kenedy, Hazard, Pedro, Remy.
=
Kocha wa kijerumani ambaye ana muda wa wiki kadhaa toka ajiunge na Liverpool kama kocha mkuu wa klabu hiyo, baada ya uongozi wa Liverpool kumfuta kazi Brendan Rodgers. Ikiwa ni siku moja imepita toka kiungo mwenye heshima kubwa katika klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uingereza Steven Gerrard athibitishe kuwa anafikiria kustaafu soka.
Baada ya siku ya November 3 Gerrard kuthibitisha kuwa huenda akastaafu soka mwishoni mwa mwaka 2016 kocha wa Liverpool Jurgen Klopp leo November 4 amethibitisha kuzungumza na Steven Gerrard na kuwa ana mpango wa kutaka kumrudisha kiungo huyo Anfield.
2AA4506100000578-3303156-image-a-2_1446628682150
Awali kabla ya Brendan Rodgers hajafukuzwa aliwahi kumwambia Gerrard kuwa wakati atakapokuwa Uingereza kwa mapumziko aende kufanya mazoezi pamoja na Liverpool katika uwanja wao wa mazoezi wa timu hiyo Melwood ila stori za zilizotoka November 4 Jurgen Klopp kathibitisha kuongea na kiungo huyo kuhusu kurejea Liverpool klabu ambayo ndio alianza kucheza soka la ushindani.
2E15032F00000578-3303156-image-m-30_1446629718334


Mkufunzi wa Manchester United Louis van Gaal amefichua kuwa anatambua mashabiki wa klabu hiyo hawajafurahia mbinu zake.
va Gaal aliongezea kusema kuwa ushindi wao dhidi ya CSKA Moscow ulileta tabasamu Old Trafford.
Uamuzi wa kocha huyo kumuondoa Anthoy Martial na badala yake kumleta Fellaini mechi ikiwa 0-0 ulishtumiwa vikali huku mashabiki wakionyesha hisia zao kwa kumzomea.
Rooney aliipa United goli la kipekee na la ushindi kunako dakika ya 79.
"Mimi si kiziwi. Naelewa maoni ya mashabiki lakini mwishowe watafurahia," alijitetea Van Gaal.
Bao la Rooney ambalo lilikuwa goli lake la 237 katika timu hiyo na kumweka katika nafasi ya pili pamoja na Denis Law kwenye orodha ya wafungaji bora wa United, lilikuwa la kwanza la klabu hiyo baada ya muda wa dakika 404.
Man United iliandikisha matokeo ya kutofungana kwenye mechi zake dhidi ya Manchester City, Middlesbrough na Crystal Palace.
Bao la mwisho kabla ya ukame wa magoli lilifungwa na Anthony Martial mnamo tarehe 21 Oktoba wakichea dhidi ya CSKA Moscow
Mchezaji wa zamani wa klabu hiyo, Paul Scholes amelaumu mbinu za Van Gaal kwa kusababisha ukosefu wa ubunifu katika timu hiyo.
Uamuzi wake wa kumchezesha Martial katika wingi ya kushoto na kumtumia Rooney kama mshambuliaji pekee umevutia shinikizo kutoka wafuasi wa klabu hiyo.
Kiungo wa timu ya taifa ya Ufaransa, Anthony Martial amecheza pamoja na Rooney kwenye safu ya ushambulizi lakini kuondolewa kwake katika dakika ya 66 iliwakashirisha mashabiki ambao waliimba jina lake wakiwataka wachezaji wa klabu hiyo kushambulia Zaidi.
"Niko na furaha kwa sababu nimechezesha Rooney kushambulia na amefunga,’’ aliongeza Van Gaal.



 Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes nchini Naigeria, Bw. Jack Liu (wa pili kulia) akiwa ameshikilia sare ya kampuni hiyo pamoja na mabalozi wapya Jonathan Akpoborie (wa kwanza kushoto) na Kanu Nwankwo (katikati) wakati wa hafla fupi ya kuwatambulisha mabalozi wapya wa kampuni hiyo jijini Lagos Naigeria mwishoni mwa wiki. Wakijumuika kwa pamoja katika tukio hilo ni wafanyakazi wa kampuni hiyo nchini Naijeria Bw. Maxwell Loko na Dare kafar (wa kwanza kushoto).

 Ofisa Mtendaji Mkuu wa StarTimes nchini Naigeria, Bw. Jack Liu (wa pili kulia) akiwa ameshikilia sare ya kampuni hiyo pamoja na mabalozi wapya Jonathan Akpoborie (wa kwanza kushoto) na Kanu Nwankwo (katikati) wakati wa hafla fupi ya kuwatambulisha mabalozi wapya wa kampuni hiyo jijini Lagos Naigeria mwishoni mwa wiki. Wakijumuika kwa pamoja katika tukio hilo ni wafanyakazi wa kampuni hiyo nchini Naijeria Bw. Maxwell Loko na Dare kafar


Mwanamitindo wa hapa nchini, Mustafa Assanali kulia na Katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania, Godfrey Mngereza wakifungua pazia kuzindua Onesho la Swahili Fashion Week leo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam aambalo litakuwa na mwendelezo wa kuonesha ubunifu wa mitindo kwa siku tatu mfululizo litakalokuwa likifanyika katika hoteli ya Sea Clief jijini Dar es Salaam.
Mwanamitindo wa hapa nchini, Mustafa Assanali akizunguza na waandishi wa habari leo katika mkutano na waandishi wa habar jijini Dar es Salaam leo kuhusiana na uzinduzi wa onesho la Swahili Fashion week iliyozinduliwa leo ikiwa tunakaribia mwishoni mwa mwaka Mwanamitindo huyo amesema kuwa katika uzinduzi huo kutakuwa na  siku tatu mfululizo za wanamitindo mbalimbali wataonyesha mitindo, Urembo na mitindo ya maisha katika onyesho litalokuwa likifanyika katika hoteli ya Sea Clif jijini Dar es Salaam.
Pia amesema kuwa onyesho hilo la mavazi lina nia ya kusisitiza jamii kuwa mitindo ni pato linalozalisha tsinia ya ubunifu pia ni kukuza dhana ya bidhaa ya Afrika ikiwa kwa mwaka huu onesho la Swahili Fashion Week ni la nane tangu lianzishwe hapa nchini.
Kushoto ni Afisa Udhamini na matukio wa kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania, Ibrahim Kaude akizungumza na waandishi wa habari leo katika mkutano wa uzinduzi wa Onesho la Swahili Fshion Week uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Maneja wa masoko wa kapuni ya magari ya Jaguar hapa nchini, Jennifer Gower.
Baadhi wa habari wakiwa katika mkutano wa uzinduzi wa Onesho la Swahili Fashion Week iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.

waliotembelea blog