Thursday, July 3, 2014

JUMATANO Klabu za Liverpool na Barcelona zilifanya mazungumzo kuhusu Uhamisho wa Luis Suarez ambae kwa sasa yuko kwenye Kifungo cha Miezi Minne alichopewa na FIFA kwa kumuuma Meno Beki wa Italy Giorgio Chiellini wakati wa Mechi ya Kombe la Dunia kati ya Uruguay na Italy huko Brazil.
Mtendaji Mkuu wa Liverpool, Ian Ayre, alikutana na Maafisa kutoka Barcelona na mazungumzo zaidi yamepangwa.

Huku pande zote zikitarajia kukamilika majadiliano yao haraka, inaaminika Dau la kumuuza Suarez kutoka Liverpool kwenda Barcelona huenda likagonga Pauni Milioni 70 kwani Liverpool wanataka Pauni Milioni 80 na Barca wanadaiwa kukubali Pauni Milioni 60.
Chanzo kutoka Anfield kilikaririwa kikisema: “Mazungumzo yalikuwa mazuri yenye mafanikio na kila upande ulifikia matarajio yake. Mazungumzo zaidi yatafanyika. Kwa sasa hakuna kilichokubaliwa.”
Inaaminika Barca wako tayari kumtoa Winga wao kutoka Chile, Alexis Sanchez, kwa Liverpool kwenye Dili ya kumchukua Suarez lakini pia mazungumzo hayo ya Jana yaligusia kutoka Dau lote bila kuweka Mchezaji juu.
Lakini, hata kama Barca watamnunua Suarez, Mchezaji huyo haruhusiwi kufanya nao Mazoezi na hata kukanyaga Uwanjani kama Mtazamaji hadi baada ya Oktoba 26 atakapomaliza Kifungo chake cha Miezi Minne kilichoanza Juni 26.

Pamoja na Kifungo hicho, Suarez pia amefungiwa kucheza Mechi 9 za Nchi yake Uruguay na pia kutwangwa Faini Dola 111,000.
Baada ya kukanusha kumuuma Chiellini, Juzi Suarez alimwomba radhi Mchezaji huyo wa Italy pamoja na Ulimwengu wa Soka kitu ambacho kilikubaliwa na Chiellini na Barca kukiita ni ‘unyenyekevu.’

waliotembelea blog