Friday, January 8, 2016


Mwanasoka raia wa Tanzania   anayechezea TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mbwana Ally Samatta amenyakua tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anachezea ndani ya bara la Afrika.
Tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika imemwendea Pierre-Emerick raia wa Gabon anayesakata kambumbu katika klabu ya Borussia Dotmund nchini Ujerumani.
Tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika almaarufu kama CAF zimetolewa usiku wa kuamkia Ijumaa mjini Abuja nchini Nigeria.
Timu bora kwa wanaume kwa mwaka uliopita ni kutoka Ivory Coast.
Kwa upande wa timu ya wanawake ya mwaka tuzo imekwenda kwa timu ya Cameroon


Kocha bora wa mwaka ni – Herve Renard, kutoka Ivory Coast, tuzo ambayo ameishinda kwa mwaka wa pili mfululizo.
Klabu bora ya soka barani Afrika ni TP Mazembe, kutoka DR Congo
Mwanasoka bora wa kike Afrika ni Gaelle Enganamouit kutoka Cameroon
Mwamuzi bora wa mwaka ni Bakary Gassama kutoka nchini Gambia
Tuzo hizo zilipambwa na shamra shamra za kila aina kutoka kwa wasanii maarufu pamoja na wanenguaji walitumbuiza akiwemo mwanamuziki nguli kutoka nchini Mali, Salif Keita pamoja na mwanamuziki kutoka Nigeria Omowumi.

FA CUP, ambalo sasa linaitwa Emirates FA Cup kwa sababu za kiudhamini na ni Kombe kongwe kabisa Duniani, litaanza kurindima Ijumaa Usiku huko England kwa Mechi pekee huko Mjini Exeter kati ya Exeter City FC na Liverpool.
Huu ni mwanzo wa Mechi za Raundi ya 3 FA CUP, inayoshirikisha jumla ya Timu 64, ambayo Klabu za Ligi Kuu England na Daraja la chini yake, The Championship, huanzia kampeni zao na nyingine hufuzu toka Raundi zake za awali kabisa.
Exeter City, Timu ya Ligi 2, ambayo ni Daraja la 4 kwa Mfumo wa England, wamefanikiwa kutinga Raundi ya 3 na sasa ni Wenyeji wa Klabu kigogo Liverpool.

Raundi hii ya 3 imeibua Mechi 5 za Timu za Ligi Kuu England kuvaana wenyewe kwa wenyewe na moja ya hizo ni ile Mechi tamu huko White Hart Lane ambako Tottenham watawavaa ‘Maajabu’ ya Ligi Kuu England Leicester City ambao wako Nafasi ya Pili katika Msimamo wa Ligi hiyo. Arsenal, ambao ndio Mabingwa Watetezi baada ya kulitwaa Kombe hili kwa mara ya pili mfululizo Mwezi Mei Mwaka huu, Jumamosi watakuwa kwao Emirates kucheza na Sunderland wakati Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, Chelsea, Jumapili wapo kwao Stamford Bridge kucheza na Timu ya Daraja la chini Scunthorpe United.
Siku ya Jumamosi Manchester United wapo kwao Old Trafford kucheza na Sheffield United wakati Man City wako Ugenini kucheza na Norwich City.

FA CUP
Raundi ya 3
Ijumaa Januari 8

22:55 Exeter v Liverpool

Jumamosi Januari 9
15:45 Wycombe v Aston Villa
[Mechi kuanza Saa 12:00 Jioni]
Arsenal v Sunderland
Birmingham v Bournemouth
Brentford v Walsall
Bury v Bradford
Colchester v Charlton

Doncaster v Stoke
Eastleigh v Bolton
Everton v Dag & Red
Hartlepool v Derby
Huddersfield v Reading
Hull v Brighton
Ipswich v Portsmouth
Leeds v Rotherham
Middlesbrough v Burnley
Newport v Blackburn
Northampton v MK Dons
Norwich v Man City
Nottm Forest v QPR
Peterborough v Preston
Sheff Wednesday v Fulham
Southampton v Crystal Palace
Watford v Newcastle
West Brom v Bristol City
West Ham v Wolves
20:30 Man United v Sheffield United

Jumapili Januari 10
15:00 Oxford United v Swansea
17:00 Carlisle v Yeovil
17:00 Chelsea v Scunthorpe
19:00 Tottenham v Leicester
21:00 Cardiff v Shrewsbury



THE EMIRATES FA CUP 2015/16
TAREHE MUHIMU
Raundi ya 3
Ijumaa 9 Januari 2016
Raundi ya 4

Jumamosi 30 Januari 2016
Raundi ya 5
Jumamosi 20 Februari 2016

Raundi ya 6-Robo Fainali

Jumamosi 12 Machi 2016

Nusu Fainali
Jumamosi 23 Aprili 2016 & Jumapili 24 Aprili 2016
Fainali Jumamosi 21 Mei 2016


www.bukobasports.comBelgium imebaki Nambari Wani kwenye FIFA Listi ya Ubora Duniani iliyotolewa Leo huku Tanzania ikipanda Nafasi 6.
20 Bora imebaki vilevile bila mabadiliko huko Mabingwa wa Dunia, Germany, wakiwa Nafasi ya 4.
Tanzania sasa ipo Nafasi ya 126 baada ya kupanda Nafasi 6 toka Mwezi uliopita.
Kwa Afrika, Timu ya juu kabisa kwenye Listi ya Ubora ni Ivory Coast ambayo ipo Nafasi ya 19.

"TOP 20" BORA:
1. Belgium
2. Argentina
3. Spain
4. Germany
5. Chile
6. Brazil
7. Portugal
8. Colombia
9. England
10. Austria
11. Uruguay
12. Switzerland
13. Ecuador
15. Italy
16. Romania
17. Wales
18. Croatia
19. Côte d'Ivoire
20. Hungary

waliotembelea blog