Monday, July 15, 2013




                                Xavi akiwa na mkewe Nuria Cunillera 
Htimaye kiungo wa Klabu ya Barcelona ya Hispania Xavi Hernandez ameamua 
kuachana na ukapela kwa kumuoa mchumba wake wa muda mrefu Nuria Cunillera, 
ndoa iliyofungwa siku ya jumamosi usiku huku ikihudhuriwa na wachezaji wenzake akiwemo gwiji Lionel Messi.
Shuhudia jinsi mambo yalivyokuwa katika picha

Ray mtayarishaji na muongozaji wa filamu Swahiliwood.
MWIGIZAJI, mtayarishaji na muongozaji mahiri wa filamu Swahiliwood Vincent Kigosi ‘Ray the Greatest’ hivi karibuni aliangusha bonge la sherehe ya siku yake ya kuzaliwa na kuwakaribishwa rafiki zake na wadau wa filamu katika moja ya Hotel, siku hiyo pia aliweza kumkumbuka swahiba yake marehemu Kanumba na kuhisi uenda angekuwepo siku hiyo.
. “Ni siku ambayo nimesheherekea siku yangu ya kuzaliwa na ndugu zangu wa karibu na wasanii wenzangu, ni siku ambayo nimekumbuka mambo mengi sana katika maisha yangu, mara nyingi swahiba wangu marehemu Kanumba siku kama ya leo ningekuwa naye katika sherehe kama hii, lakin ndio mambo ya Mungu huwezi kulaumu kilichobaki ni kumuombea Mwenyezi Mungu ampumzishe kwa amani Amen,” alisema The Greatest.

Steven Kanumba, Vincent KigosiMaswahiba wawili wakitoka safari marehemu Kanumba na Ray
Vincent Kigosi, InnoRay akiwa na mdau wa filamu Inno.
Katika sherehe hiyo iliyopambwa na vinywaji na malaji kibao ilijumuisha wasanii nguli katika tasnia ya filamu kama Bonge la bwana, JB, Maya, Odama, Chikoka na wasanii wengine kibao huku kukiwa na michezo kadha wa kadhaa ni jambo jema kwa marafiki kukumbuka katika matukio kama hayo.
.

Vincent Kigosi, steven kanumbaRay akiwa na marehemu katika filamu ya Oprah
Pengine sasa watu wanaona tasnia ya filamu kupwaya baada ya Ray kukosa mpinzani wa kweli katika tasnia ya filamu, tofauti na alivyokuwepo marehemu Kanumba ushindani wa mafanikio ulikuwa wazi kuanzia ubora wa kazi na umiliki wa mali ikiwa sambamba na magari mazuri, vifaa vya Production jambo ambalo kwa sasa analifanya Ray pekee hana mpinzani

Hii ndio Ndege ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inatambulika kama 5H - ONE

 

OPARESHENI Fichua Maovu (OFM) inayoendeshwa na mapaparazi wa Global Publishers inazidi kufichua ‘madudu’ kwenye jamii, safari hii imekutana na machangu ambao wamecharuka kuendeleza biashara hiyo kwa kisingizio cha kutafuta fedha za kununulia futari.


‘Askari’ wa OFM, wiki iliyopita alifanya uchunguzi katika viunga mbalimbali maarufu kwa biashara hiyo na kukuta machangudoa wakifanya biashara yao kama inavyokuwa katika miezi ya kawaida.
Maeneo ambayo yalionekana kushamiri zaidi kwa biashara hiyo ni Barabara ya Mwananyamala Hospitali, American Chipsi, Makaburi ya Kinondoni, Viwanja vya Leaders Club, Taasisi ya Moyo, Jolly Club (Masaki), Hospitali ya Agha-Khan, New Maisha Club (Masaki) na Coco Beach.

Idadi kubwa ya wadada hao walipohojiwa na paparazi wetu, walisema wanaendelea na biashara hiyo kwa kuwa ndiyo waliyoizoea kutafutia kipato na wakiiacha, watakufa kwa njaa katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Ili kujiridhisha kwa data, paparazi wetu alijifanya mteja na kukutana na machangu wa Makaburi ya Kinondoni ambao walidai wanapenda waitwe ‘scraper’ au vyuma chakavu pasipo kufafanua zaidi, bahati mbaya wakashtukia mchezo:
Changudoa: “We kaka mbona unatuzingua? We ulivyokuja si ulijifanya mteja, kumbe paparazi, sisi hatuwezi kuacha kujiuza kwa kuwa ndiyo kazi tuliyoizoea, sasa tukikaa nyumbani tutapata wapi futari?” alihoji mmoja wa machangudoa.
Paparazi: “Hivi ni kweli nyie mnafunga?”

Changudoa: “Wewe tumia ubongo na maswali yako yanayotia njaa, hata kama sisi tunafunga au hatufungi tuna watu wanaotutegemea majumbani kwetu kuwatafutia futari, sasa tusipohangaika itakuwaje?”
Baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu waliozungumza na Ijumaa Wikienda, walionesha kukerwa na tabia hiyo na kulaani vibaya kwani mwezi huu ni maalum kwa ajili ya kumrudia mwenyezi Mungu na kuacha dhambi.


Baadhi ya mashabiki wakiwa na furaha kuburudishwa na mwanamuziki Jose Chameleone.Erica Lulakwa (TZ), a Singer and SongWriter based in San Francisco CaliforniaErica Lulakwa (TZ akicheza na mashabiki wake Oakland


                                      Agnes Gerald ‘Masogange’.     
                                       Sandra Khan 'Binti Kiziwi'.
                                     Sharifa Mahamoud (27
                                              Melisa Edward
                                           Saada Ally Kilongo (26),           


MTANDAO wa wauza madawa ya kulevya unazidi kupukutika Bongo kufuatia madai ya kukamatwa kwa watu wanaodaiwa kujishughulisha na ubebaji ‘punda’ wa biashara hiyo haramu, Hivi karibuni, Video Queen wa Wimbo wa Masogange, Agnes Gerald ‘Masogange’ amedaiwa kunaswa nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ akiwa na kilo mia moja na hamsini za unga unaoaminika ni sehemu ya madawa ya kulevya. Ameshapanda kortini mara moja Ijumaa iliyopita.
Wakati Masogange akisota Sauzi kwa madai hayo mazito, habari ya mjini kwa sasa ni ya mtalaka wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Ally Mohammed ’Z-Anto’, Sandra Khan au Binti Kiziwi kudaiwa kutupwa jela miaka mitano kwa sakata la ‘unga’.
HABARI YA MJINI KWA SASA NI BINTI KIZIWI
Kuanzia Alhamisi iliyopita, habari zilizoligubika Jiji la Dar ni kuwa Binti Kiziwi amenyongwa nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya.
Kwa mujibu wa mitandao, Binti Kiziwi alinyongwa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, mitandao hiyo haikusema kama mrembo huyo alinyongwa hadi kufa au la! Sheria za hukumu hiyo, mwenye hatia anatakiwa kunyongwa hadi kufa.
UKWELI WA BINTI KIZIWI NI HUU
Baada ya kusambaa kwa manenomaneno hayo, Ijumaa Wikienda liliingia mtaani kuisaka familia ya Binti Kiziwi lakini bila mafanikio.
Kwenye makazi ya mama yake, Buguruni, Dar, majirani walisema mzazi huyo amehama baada ya kufunga ndoa siku chache kabla ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
IJUMAA WIKIENDA LAZIDI KUCHIMBA
Ijumaa Wikienda lilizidi kuzama ndani katika kuchimbua tetesi hizo ambapo lilifanikiwa kumpata ndugu wa kiume wa Binti Kiziwi na kufanya naye mazungumzo kama ifuatavyo:
Wikienda: Samahani, nimeambiwa wewe ni ndugu wa Binti Kiziwi, ni kweli?
Ndugu: (huku akitaja uhusiano wao) Ni kweli, nikusaidie nini?
Wikienda: Kuna manenomaneno kwamba Binti Kiziwi amenyongwa nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya, ni kweli?
Ndugu: Sijui hizo habari watu wanazipatia wapi?! Watanzania wana maneno sana. Si kweli ndugu mwandishi.
Wikienda: Ukweli ni upi?
Ndugu: Kwanza kabisa Binti Kiziwi hakukamatiwa China, alikamatiwa Hong Kong, kwa sheria za kule mtu akipatikana na hatia ya kukutwa na ‘unga’ anahukumiwa jela tu.
“Binti Kiziwi amehukumiwa miaka mitano jela Hong Kong, na si China. Watu wajue hilo na miaka mitano si mingi, atatoka.”
Wikienda: Nashukuru sana kwa ushirikiano ndugu yangu.
Ndugu: Asante, waambie Watanzania waache kuongeaongea sana
EMU WA KANUMBA NAYE ASOTA RUMANDE Msichana anayejulikana kwa jina la Saada Ally Kilongo (26), maarufu kama ‘Demu wa Kanumba’ yeye bado anasota kwenye Gereza la Segerea, Dar kwa tuhuma za kukutwa na madawa ya kulevya yanayokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 170. Saada alidakwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar Juni 24, mwaka huu.  Kesi yake ilisikilizwa kwa mara ya kwanza, Juni 29, mwaka huu kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu, Dar es Salaam. Mdada huyo mkazi wa Mbezi Beach, Dar aliwahi kutoka kwenye Gazeti la Ijumaa la Desemba 9, 2011 ukurasa wa mbele kwa kichwa cha habari kisemacho: SAA 7 USIKU KANUMBA AGANDANA NA DEMU.
Demu huyo ambaye wakati huo alikuwa mwanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama, Dar (alimaliza mwaka jana), picha yake akiwa na marehemu Kanumba ilipigwa Desemba 2, 2011 ndani ya Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambapo kulirindima Tamasha la Usiku wa Kiafrika lililopambwa na mkali wa dansi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ipupa Nsimba ‘Fally Ipupa’.
MSANII BONGO MUVI ‘ASUBIRI KITANZI’ MISRI
Wakati mlolongo wote ukiwa hivyo, mrembo aliyewahi kushiriki filamu Bongo, Sharifa Mahamoud (27) naye anashikiliwa katika gereza moja nchini Misri wakati kesi yake ya kukamatwa na madawa ya kulevya ikirindima nchini humo.
BALOZI WA TANZANIA -MISRI AZUNGUMZA
Kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania nchini Misri, Mohammed Haji, Mei 18, mwaka huu, Sharifa na nduguye, Abdallah Salum (28), wote wakazi wa Magomeni, Dar, walinaswa na unga jijini Cairo wakitokea Dar.
Mei 26, walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza. Madawa waliokutwa nayo ni heroine kilo saba (gharama ya fedha haikutajwa).
Kwa sheria za Misri, kosa la kukutwa na madawa ya kulevya ni kunyongwa hadi kufa. Lakini kwa mujibu wa Balozi Salum, hana kumbukumbu za raia wa kigeni aliyewahi kuhukumiwa kunyongwa nchini humo kwa kosa hilo.
Balozi alisema: “Endapo watapatikana na hatia kwamba kweli dawa hizo zilikuwa zao, hili litakuwa doa la kwanza kwa nchi yetu (Tanzania) hapa Misri.
Kwa mujibu wa Sharifa wakati akihojiwa na TV ya Misri, alishangaa kuona begi lake likiwa na madawa ya kulevya baada ya kukamatwa na kwamba aliingia nchini humo kumtafuta binamu yake.
STAA wa sinema za nyumbani, Jacqueline Wolper amemtemea cheche msanii mwenzake, Baby Joseph ‘Baby Madaha’ kuwa anatafuta ustaa (kiki) kupitia jina lake

Akifafanua kauli yake mbele ya kinasa sauti cha Stori 3, Wolper alisema anamshangaa msanii huyo kumsemea vibaya, kutoa lugha ya matusi mtandaoni bila sababu za msingi

“Namshangaa Baby Madaha kwa aliyoyasema kuhusu mimi, anatafuta kiki. Watu wanafahamu mimi ni staa kuliko yeye kwa hiyo sidhani kama ana sababu ya kugombana na mimi,” alisema Wolper.


MTANDAO wa wauza madawa ya kulevya unazidi kupukutika Bongo kufuatia madai ya kukamatwa kwa watu wanaodaiwa kujishughulisha na ubebaji ‘punda’ wa biashara hiyo haramu, Ijumaa Wikienda lina mtiririko wote.

Hivi karibuni, Video Queen wa Wimbo wa Masogange, Agnes Gerald ‘Masogange’ amedaiwa kunaswa nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’ akiwa na kilo mia moja na hamsini za unga unaoaminika ni sehemu ya madawa ya kulevya. Ameshapanda kortini mara moja Ijumaa iliyopita.
Wakati Masogange akisota Sauzi kwa madai hayo mazito, habari ya mjini kwa sasa ni ya mtalaka wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Ally Mohammed ’Z-Anto’, Sandra Khan au Binti Kiziwi kudaiwa kutupwa jela miaka mitano kwa sakata la ‘unga’.

HABARI YA MJINI KWA SASA NI BINTI KIZIWI
Kuanzia Alhamisi iliyopita, habari zilizoligubika Jiji la Dar ni kuwa Binti Kiziwi amenyongwa nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya.
Kwa mujibu wa mitandao, Binti Kiziwi alinyongwa wiki mbili zilizopita.
Hata hivyo, mitandao hiyo haikusema kama mrembo huyo alinyongwa hadi kufa au la! Sheria za hukumu hiyo, mwenye hatia anatakiwa kunyongwa hadi kufa.


UKWELI WA BINTI KIZIWI NI HUU
Baada ya kusambaa kwa manenomaneno hayo, Ijumaa Wikienda liliingia mtaani kuisaka familia ya Binti Kiziwi lakini bila mafanikio.
Kwenye makazi ya mama yake, Buguruni, Dar, majirani walisema mzazi huyo amehama baada ya kufunga ndoa siku chache kabla ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

IJUMAA WIKIENDA LAZIDI KUCHIMBA
Ijumaa Wikienda lilizidi kuzama ndani katika kuchimbua tetesi hizo ambapo lilifanikiwa kumpata ndugu wa kiume wa Binti Kiziwi na kufanya naye mazungumzo kama ifuatavyo:
Wikienda: Samahani, nimeambiwa wewe ni ndugu wa Binti Kiziwi, ni kweli?
Ndugu: (huku akitaja uhusiano wao) Ni kweli, nikusaidie nini?
Wikienda: Kuna manenomaneno kwamba Binti Kiziwi amenyongwa nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na madawa ya kulevya, ni kweli?
Ndugu: Sijui hizo habari watu wanazipatia wapi?! Watanzania wana maneno sana. Si kweli ndugu mwandishi.
Wikienda: Ukweli ni upi?
Ndugu: Kwanza kabisa Binti Kiziwi hakukamatiwa China, alikamatiwa Hong Kong, kwa sheria za kule mtu akipatikana na hatia ya kukutwa na ‘unga’ anahukumiwa jela tu.
“Binti Kiziwi amehukumiwa miaka mitano jela Hong Kong, na si China. Watu wajue hilo na miaka mitano si mingi, atatoka.”
Wikienda: Nashukuru sana kwa ushirikiano ndugu yangu.
Ndugu: Asante, waambie Watanzania waache kuongeaongea sana.


waliotembelea blog