Tuesday, May 12, 2015



Jumatano Mei 13 

Real Madrid CF vs Juventus FC [1-2]


Sasa ni rasmi, mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa amemwaga wino kuichezea klabu ya Free State Stars ya Ligi Kuu Afrika Kusini kwa miaka minne .
Ngasa ameripotiwa kufurahia mkataba huo mnono na kuanza kwake kwa maisha mapya baada ya kucheza nyumbani kwa miaka kadhaa.

Ngasa ameonekana katika mitandao kadhaa akiwa na kocha wa timu hiyo baada ya kusaini mkataba.
“Nataka kutumia fursa hii kuitangaza soka ya Tanzania na nitajituma ili kufanya vizuri zaidi", amesema mchezaji huyo.


KEPTENI wa Liverpool Steven Gerrard Jumamosi ataichezea Klabu yake kwa mara ya mwisho Uwanjani kwao Anfield na Tiketi za Mechi hiyo zimefika Bei ya Shilingi Milioni 4, 090, 680/=.
Jumamosi Liverpool watacheza Mechi yao ya mwisho ya Ligi Kuu England Msimu huu Uwanjani kwao Anfield dhidi ya Crystal Palace.


Hii Leo mtandao unaouza Tiketi kwa ajili ya Mechi hiyo, www.ticketbis.net umeanika Bei za Tiketi za kuanzia Pauni 100 hadi 1,324.64 ikiwa ni takriban Shilingi 314,727 hadi Shilingi 4,166, 985.

Kwa Mechi ya kawaida kwenye Jukwaa Kuu la Anfield Tiketi huuzwa Pauni 47 yaani Shilingi 147,922.
Gerrard, mwenye Miaka 34, anastaafu kuicheza Liverpool Msimu huu baada ya kuwa nao kwa Miaka 17 na Mechi yake ya mwisho kabisa itakuwa Wiki ijayo Ugenini wakicheza na Stoke City.
Hata hivyo, Gerrard ataendelea kusakata Soka huko Marekani akichezea Ligi ya MLS na Klabu ya LA Galaxy.
Zipo habari zinasema Gerrard atawekewa Gwaride la Heshima na WAchezaji kabla ya Mechi ya Jumamosi kuanza kati ya Liverpool na Crystal Palace.
 
Steven Gerrard na Alex wakipozi kupata picha kabla ya kupanda ndege ya BA777Alex Gerrard kwenye pozi la hatariKinywaji!


Gerrard, mwenye Miaka 34, anastaafu kuicheza Liverpool Msimu huu baada ya kuwa nao kwa Miaka 17 na Mechi yake ya mwisho kabisa itakuwa Wiki ijayo Ugenini wakicheza na Stoke City.
Hata hivyo, Gerrard ataendelea kusakata Soka huko Marekani akichezea Ligi ya MLS na Klabu ya LA Galaxy.
Kwa raha zao Barca!2-1Neymay alifunga bao mbili kipindi cha kwanza!Wachezaji wa Barca wakipongezaNeymar akishangilia kwa raha zake!Neymar akishangilia moja ya bao zake mbili za kipindi cha kwanza dakika ya 15 na 29.Medhi Benatia dakika ya 7 kipindi cha kwanza anaipatia Bayern Munich bao la kuongoza. Dakika ya 15 Neymar alisawazisha bao baada ya kupewa pasi na Luis Suarez.Dakika ya 29 tena Neymar akawachapa bao la pili na kufanya 2-1 dhidi ya Bayern Munich.Medhi Benatia dakika ya 7 kipindi cha kwanza aliziona nyavu za barca.
Akipongezwa na AlonsoRaha ya bao la kwanza!!

Neymar akishangilia bao lake la kwanza!Thomas Muller hoi!Mchezo umekwisha!! 
Mpaka mapumziko Bayern walikuwa nyuma ya bao 2-1 kwenye uwanja wao wa Allianz Arena.Suarez na mbwembwe zake katika kipindi cha kwanza...Rafinha dhidi ya IniestaKikosi cha Bayern MunichKikosi cha Barcelona kilichoanza 11Taswira kamili!Wamekutana tenaaa!Mwali anayetafutwa huyu hapa!


FIFA
  • Wachezaji watatakiwa kuonesha pasi zao halisi za kusafiria (passport) kabla ya mechi ili kuhakikisha kama wanastahili.
FIFA imerekebisha sheria zake, ikiwa pamoja  na kufuta  maamuzi ya  kurudia mechi nzima ya kufuzu Kombe la Dunia ambayo ilivunjika/iliishia katikati (haikufika dakika 90), kwa sasa mechi iliyovunjika itaanzia katika dakika ya mwisho wakati mechi inavunjika.
Wachezaji watatakiwa kuonesha pasi halisi za kusafiria massa 24 kabla mechi haijaanza kama uthibitisho wa kustahili kulichezea taifa husika.
Mwaka 2014, Uongozi wa FIFA ulithibika kuwa na udhaifu mkubwa hasa  kwa kushindwa kuwatambua wachezaji waliokuwa hawastahili  kuchezea baadhi ya nchi katika mechi za makundi.
Africa lilikuwa ni Bara pekee, kati ya mabara sita wanachama wa FIFA lililokuwa na matatizo katika kuidhinisha uhalali wa wachezaji.
Mataifa saba ya Africa – Burkina Faso, Equatorial Guinea, Ethiopia, Gabon, Liberia, Sudan and Togo –  yalichezesha wachezaji ambao hawakuweza kuthibitisha uhalali wao, kitu kilicholazimisha FIFA kuwazawadia wapinzani wao ushindi wa 3-0.

Hizi ndizo sheria za FIFA zilizobadilika kwa ajili ya Kombe la Dunia 2018:
  • FIFA inataka mechi zote zilizovunjika (zilizoishia katikati, kabla ya dakika 90), zichezwe tena katika tarehe ya mbele na vikosi vilevile na zianzie katika dakika ileile ilipoishia wakati mechi inavunjika. Kabla ilikuwa mechi inarudiwa dakika 90.

  • Mchezaji asiye na pasi halisi ya kusafiria hataweza kucheza mechi. Vitambulisho au nyaraka zozote rasmi za kiserikali hazitakubaliwa.

  • FIFA imefuta kikomo cha faini ya Franc milioni moja za Uswisi (zaidi ya Tsh. bilioni moja na Milioni 900) kwa mashirikisho endapo timu iliyofuzu fainali za Urusi itatolewa siku 30 kabla ya mashindano kuanza au wakati mashindano yanaendelea.

  • Teknolojia ya kugundua goli (Goal-line technology) itaweza kutumika katika mechi za kufuzu endapo timu zitakubaliana kwa maandishi.

  • Vipindi vya kutulia kidogo (Cooling breaks) vitaamuliwa na refa katika mechi za kufuzu.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na viongozi mbalimbali katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Raymond Mushi alipowasili kutoka Algeria katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Kamanda wa Polisi Kanda ya Dar es salam Suleiman Kova, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Raymond Mushi, Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe. Sophia Mjema na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Paul Makonda alipowasili kutoka Algeria katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipanda ndege katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Houari Boumediene jijini Algiers Jumatatu May 11, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini humo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiaga wenyeji wake katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Houari Boumediene jijini Algiers Jumatatu May 11, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini humo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na Marubani na Wafanyakazi wa Shirika la ndege la Tassili la Algeria baada ya kuwsili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo May 12, 2015 baada ya kuhitimisha ziara yake rasmi ya siku tatu nchini Algeria.
 PICHA NA IKULU 

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo leo asubuhi nyumbani kwa Baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye John Nyerere kilichotokea hivi karibuni.Aliyesimama pembeni ya Rais ni mdogo wa marehemu Makongoro Nyerere.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiifariji familia ya marehemu John Nyerere nyumbani kwao Msasani jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha mwanaye John Nyerere kilichotokea juzi .Mwili wa Marehemu John Nyerere rubani wa zamani wa ndege za kivita nchini aliyeshiriki kikamilifu vita vya Uganda kati ya mwaka 1978 na 1979, unatarajiwa kusafirishwa leo kwenda kijijini Butiama mkoani Mara kwa maziko.(picha na Freddy Maro).
Afisa mahusiano Mkuu wa TEITI, Catherine Mbatia akimkaribisha rasmi Mwenyekit wa TEITI, Jaji Mark Boman kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Warsha hiyo iliyowakutanisha wandishi wa habari za biashara na wadau mbalimbali ikiwemo wadau wa madini.
6
Meneja Mahusiano, Alex Modest, (kulia)akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika semina hiyo watatu kulia ni Meneja mikakati kutoka (TBDC) George Kibakaya (kushoto) Mwenyekiti TEITI,Jaji Bomani,wa pili kushoto mwandishi mchambuzi, John Bwire,(katikati) ni Halfani Halfani kutoka (Oil Gas Association Tanzania-OGAT).
2
Afisa mahusiano Mkuu wa TEITI, Catherine Mbatia akielezea juu ya TEITI, wakati wa Warsha hiyo iliyowakutanisha wandishi wa habari za biashara na wadau mbalimbali ikiwemo wadau wa madini.
13
Mwenyekiti TEITI, Jaji Bomani (kushoto ) akichangia mada katika warsha hiyo, wengine ni Mwanahabari na mchambuzi John Bwire, akifuatiwa na Halfani Halfani wa OGAT, Meneja mikakati kutoka (TBDC) George Kibakaya pamoja na Godvictor kutoka kampuni ya madini ya Geita.
14
Wadau wa sekta ya madini na wanahabari wakifuatilia mada katika warsha hiyo.

waliotembelea blog