Monday, December 16, 2013

MUONEKANO WA BASI LA BUKOBA EXPRESS T 315 BLC BAADA YA KUANGUKA ,BASI LILIKUWA LINATOKEA DAR ES SALAAM KUELEKEA BUKOBA MUDA MCHACHE BAADA YA KUANZA SAFARI ALFAJIRI YA LEO KUTOKA LILIPOKUWA LIMELALA,TAYAR KUANZA SAFARI YA KUELEKEA BUKOBA,WATU WOTE WAMENUSURIKA KIFO NA WENGINE KADHAA WAMEPATA MAJERAHA !!!

Sanamu hii ya Mandela iko mikono wazi ishara ya Mandela kukumbatia watu wa Afrika Kusini
Sanamu kubwa zaidi duniani ya Nelson Mandela imezinduliwa katika mji mkuu wa Afrika kusini Pretoria siku moja baada ya rais huyo wa zamani kuzikwa.
Sanamu hiyo iliyotengenezwa kwa shaba ina urefu wa mita tisa na ina uzani wa tani nne unusu. Ilizinduliwa katika bustani la majengo ya bunge na inaonyesha Nelson Mandela akihimiza umoja na maridhiano.
Sanamu hiyo yenye mikono ya Mandela ikiwa wazi ilinuiwa kuonyesha Mandela alivyoliungaisha taifa zima kwa mapenzi yake.
Bwana Mandela lipewa mazishi ya kitaifa nyumbani alikozaliwa katika kijiji cha Qunu Jumapili
Familia ya Madiba , viongozi wa ANC , viongozi wa Afrika na maafisa wengine wakuu walihudhuria mazishi hayo katika kijiji cha Qunu mkoani Cape Mashariki.
Kifo cha Mandela kilifuatwa na maombolezi ya siku kumi na sherehe za kukumbuka maisha ya Mandela aliyefariki akiwa na umri wa miaka 95.
Bendera ya nchi hiyo ilirejeshwa kupepea katika urefu wake wa kaiwada.
Mandela anakumbukwa kwa juhudi zake za kupatanisha wananchi na kupigia debe msamaha miongoni mwa watu na ndio maana leo ikawa siku iliyotengwa kwa ajili ya uzinduzi wa sanamu hiyo.
Wakati wa utawala wa wazungu, terehe 16 Disemba ilijulikana kama siku ya kuwakumbuka mashujaa wa Afrikaners walioshinda vita dhidi ya jeshi la Zulu mwaka 1883.
Zaidi ya karne moja baadaye mwaka 1961, Mandela alizindua jeshi lake la Umkhonto we Sizwe kupigana dhidi ya utawala wa wazungu.
Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza MABINA ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe huko maeneo ya Kiseke jijini Mwanza.

Chanzo cha kuuwawa ni kwamba mabina aliwanyang'anya ardhi wananchi hao na kesi ikawa mahakamani na leo mchana Mabina bila kibali cha mahakama alikuwa anapanda miti na kujenga msingi wa nyumba ndipo wananchi wakaenda kumhoji iweje anapanda miti na kuweka msingi kwenye viwanja hivyo ilhali kesi ipo mahakamani? 

Mabina akaanza kutoa lugha chafu na kurusha risasi hewani. Kwa mujibu wa Katibu wa CCM ndg Joyce Masunga (maarufu kama Maziwa Fresh) ni kweli kuwa tukio hili limetokea na tunaendelea kufuatilia kupata habari zaidi.
After school bash!! tamasha kubwa la kila mwaka ,linalokuwa
 linawaunganisha wanafunzi  Town baada ya shule zao 
kufungwa hivyo kupata fursa ya  kujumuika  pamoja, pia  kuwakutanisha na wasanii
 wanaowapenda ,limemalizika

 usiku huu..WCB president na team yangu yoote tulikuwepo
 na tukawapa kile walichokikosa kwa mda 
mlefu wakiwa busy na masomo...
angalia baadhi ya picha za matukio hali ilivyokuwa


 





 My brother on one n two,Romy Jones


love from the heart...........



Mazishi ya Nelson Mandela yanaendelea katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape na kumaliza wiki moja ya maombolezi ya shujaa wa Afrika mwendazake Nelson Mandela.

 
Takriban watu 4,500 wakiwemo wageni wa kimataifa wanahudhuria mazishi hayo ambayo ni ya mchanganyiko wa tamaduni za kale na mambo ya kisasa.
 
Familia ya Mandela ilikesha wakijiandaa kwa mazishi ya leo huku kukiwa na muimbaji ambaye atakuwa anaita mizimu ya mababu wa kale na pia wakiongelesha mwili wa Mandela kumwambia kuwa sasa anazikwa.




 Rais Jakaya Kikwete ni mmoja wa viongozi mbalimbali wanaoshiriki kwenye mazishi ya hayati Mzee Nelson Mandela yanayofanyika leo kijijini kwao Qunu, nchini Afrika Kusini.


Watu wengi maarufu Duniani wapo eneo hili hivi sasa kuhudhuria mazishi ya Mzee Nelson Mandela yanayoendelea hivi sasa katika kijiji cha Qunu,baadhi yao ni Oprah Wilfrey,Forest Whitaker,Richard Branson,Idris Ebra na wengine wengi.


Mwili wa Mzee Mandela ukiwasili ukumbini.

waliotembelea blog