Tuesday, September 16, 2014



Warembo wanaoshiriki shindano la Redd’s Miss Tanzania 2014 leo wameingia siku ya pili ya kambi yao jijini Dar es Salaam na baada ya semina asubuhi na mapumziko ya mchana jioni hii wamefanya mazoezi katika chumba maalum cha mazoezi ‘Gym’, ungana na mpigapicha wa Father Kidevu Blog katika picha mbalimbali za warembo hao katika kambi yao.









Kikosi cha Timu ya Wakata Miwa Kagera Sugar wameanza leo hii safari kuelekea jijini Tanga kwa ajili ya mchezo wa ufunguzi wa Ligi kuu soka Tanzania bara katika uwanja wa CCM Mkwakwani dhidi ya wenyeji Mgambo JKT, septemba 20 mwaka huu.
Kocha msaidizi wa Kagera Sugar, Murage Kabange amesema klabu hiyo ina jumla ya wachezaji 25 na hii leo tayari wapo safari na viongozi watano kwenda kusaka pointi tatu muhimu.
Kabange aliongeza kuwa wameamua kuanza safari mapema kwasababu kutoka Kagera kwenda Tanga ni mbali sana.
Viongozi wa Kagera Sugar
Ubutu wa safu ya ushambuliaji lilikuwa tatizo la kudumu kwa Kagera Sugar lakini kwa sasa limepata marekebisho kwani wamesajili Vijana wa nguvu msimu huu.
WAKATA miwa wa Kaitaba, `Wanankulukumbi` Kagera Sugar wakijifua kwenye Uwanja wa Kagera Sugar hivi karibuni tayari kwa Ligi kuu Vodacom sep 20 mwaka huu. Kagera Sugar wataanza ufunguzi wa Ligi kuu Vodacom Ugenini na timu ya Mgambo JKT mkwakwani Mjini Tanga wikiendi hii.
Kocha huyo alisema: “Tuna imani na vijana wetu kuwa wanaweza kutufikisha tunapotaka, japokuwa ligi ya msimu huu inaonekana itakuwa ngumu, lakini tutajitahidi kupigana ili kuweza kushika nafasi za juu”.



Wachezaji wa Kagera Sugar wakifaya mazoezi yao kwenye Uwanja wa Kaitaba Hivi karibuni.

Baadhi ya Viongozi wa Timu ya Kagera Sugar wakiwa Uwanjani Kaitaba wakishuhudia mazoezi ya Vijana wao. Wakijifua kujiandaa na Ligi Kuu Vodacom msimu mpya 2014/15 inayotarajia kuanza hivi Karibuni sep.20 mwaka huu.


Murage Kabange, kocha msaidizi wa Kagera Sugar (kulia) tayari amebainisha kuwa mapungufu waliyokuwa nayo katika kikosi chao kuwa wameishayafanyia marekebisho na wako tayari kupambana na Mgambo JKT ya Mjini Tanga.
Kocha Mkuu wa Kagera Sugar (kulia) Bw. Jackson Mayanja akiangalia vijana wake wakati w mazoezi yao kwenye Uwanja wao wa Nyumbani Kaitaba hivi karibuni


Msanii mwingine anaekuja vyema kwenye anga ya muziki wa Bongofleva aitwaye Kadja ambaye anatamba na wimbo wake wa Maumivu niache akiimba pamoja na Linah.

Mkali wa Bongo Hip Hop Farid Kubanda a.k.a Fid Q akikamua vilivyo juu ya jukwaa na la Fiesta.

Msanii wa Bongofleva,Kadja akiimba wimbo wake wa Maumivu niache mbele ya maelfu ya wakazi wa Tabora (hawapo pichani) waliofika kwenye tamasha la Fiesta usiku wa kuamkia leo.

Ilikuwa buruuudani ya kusambaza upendo wa kweli kwa wakazi wa Tabora ndani ya tamasha la Fiesta

Palikuwa hapatoshi usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora,ambapo tamasha la Fiesta lilirindima.

Wasanii chipukizi kutoka Tabora nao walionesha umahiri wao jukwaani

Sehemu ya umati mkubwa wa watu waliofika kulishuhudia tamasha la Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya uwanja wa Al-Hassan Mwinyi mjini Tabora.


Aaron Ramsey and Mesut Ozil celebrate the Welshman's goal away at Dortmund last November, in a game the Gunners won 1-0

EUROPE: Champions League - Group Stage
11:45 Benfica-Zenit Petersburg


11:45 Dortmund-Arsenal


11:45 Galatasaray-Anderlecht


11:45 Juventus-Malmo FF


11:45 Liverpool-Ludogorets


11:45 Monaco-Bayer Leverkusen


11:45 Olympiakos Piraeus-Atl. Madrid


11:45 Real Madrid-Basel

waliotembelea blog