Friday, December 11, 2015



Mchezaji wa timu ya taifa ya Honduras Arnold Peralta ambaye amewahi kucheza katika vilabu vya Olimpia na Rangers ya Scotland ameuwawa kwa kupigwa risasi wakati akiwa katika Parking za magari jijini La Ceiba Honduras, Arnold Peralta alikuwa likizo nyumbani kwao Honduras.
Kifo cha Arnold Peralta ambaye anamudu kucheza nafasi ya kiungo kwa ufasaha kinachunguzwa na maafisa usalama wa nchi hiyo, ila taarifa za awali zinaonesha kuwa Arnold Peralta alipigwa risasi sio na majambazi ila inasadikika ni watu wenye visasi lakini tukio bado linachunguzwa.
Olympics+Day+2+Men+Football+Spain+v+Honduras+ENz_YKSG4G9l
Headlines za kifo cha Arnold Peralta kupigwa risasi zinakuja ikiwa ni mwaka mmoja umepita toka auwawe kwa risasi golikipa wa timu ya taifa ya Afrika Kusini na klabu ya Orlando Pirates Senzo Meyiwa, ambaye nae alipigwa risasi na majambazi ambao walienda kufanya uharifu katika nyumba ya mpenzi wake.
TL_1081310-602x400
Senzo Meyiwa


Kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City ya Uingereza Yaya Toure alikuwa ni mmoja kati ya wachezaji watano waliokuwa wanawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika inayotolewa na shirika la utangazaji la Uingereza BBC, Yaya Toure amefanikiwa kuibuka na ushindii wa baada ya kupata kura nyingi zaidi ya Pierre-Emerick Aubameyang, Andre Ayew, Yacine Brahimi na Sadio Mane.
86610826_afoty-2015
List ya wachezaji watano waliokuwa wanawania tuzo ya mchezaji bora wa BBC
Kutwaa tuzo hiyo kwa Yaya Toure kunamfanya kuwa mchezaji wa tatu kuingia katika rekodi ya wachezaji wa zamani wa Nigeria Nwankwo Kanu na Jay-Jay Okocha ambaoo kila mmoja katwaa tuzo hiyo mara mbili, rekodi ambayo inashikiliwa na wachezaji watatu kwa sasa ikiwemo Toure.
e
List ya wachezaji waliowahi kutwaa tuzo hiyo
Toure kwa mara ya kwanza alifanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa BBC mwaka 2013, baada ya ushindi wa tuzo hiyo hii ni moja kati ya sentensi za Yaya Toure “Najivunia kupokea tuzo hii kutoka kwa mashabiki wangu siwezi kuamini”

waliotembelea blog