Friday, December 11, 2015


Kiungo wa kimataifa wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City ya Uingereza Yaya Toure alikuwa ni mmoja kati ya wachezaji watano waliokuwa wanawania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika inayotolewa na shirika la utangazaji la Uingereza BBC, Yaya Toure amefanikiwa kuibuka na ushindii wa baada ya kupata kura nyingi zaidi ya Pierre-Emerick Aubameyang, Andre Ayew, Yacine Brahimi na Sadio Mane.
86610826_afoty-2015
List ya wachezaji watano waliokuwa wanawania tuzo ya mchezaji bora wa BBC
Kutwaa tuzo hiyo kwa Yaya Toure kunamfanya kuwa mchezaji wa tatu kuingia katika rekodi ya wachezaji wa zamani wa Nigeria Nwankwo Kanu na Jay-Jay Okocha ambaoo kila mmoja katwaa tuzo hiyo mara mbili, rekodi ambayo inashikiliwa na wachezaji watatu kwa sasa ikiwemo Toure.
e
List ya wachezaji waliowahi kutwaa tuzo hiyo
Toure kwa mara ya kwanza alifanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa BBC mwaka 2013, baada ya ushindi wa tuzo hiyo hii ni moja kati ya sentensi za Yaya Toure “Najivunia kupokea tuzo hii kutoka kwa mashabiki wangu siwezi kuamini”

0 maoni:

Post a Comment

waliotembelea blog