Monday, February 16, 2015


Mkuu wa wilaya ya mtwara Mh, Wilman Kapenjama akimpongeza mzee Sefu Namtapika (60) baada ya kumkabidhi gari yake aina ya Toyota IST mpya aliyojishindia kupitia promosheni ya Airtel Yatosha zaidi na kukabidhiwa katika viwanja vya Mashujaa mkoani Mtwara mwishoni mwa wiki hii.
Mkuu wa wilaya ya Mtwara Mh, Wilman Kapenjama akikabidi funguo ya gari kwa Mshindi wa Promosheni Airtel yatosha Zaidi mkoani Mtwara bw, Sefu Namtapika (60) ambae ni mwalimu mstaafu aliyeibuka na ushindi wa Toyota IST kupitia droo ya kwanza ya promosheni Yatosha zaidi inayoendesha na Airtel. Wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni toka kushoto nyuma ni Meneja mauzo wa Airtel mkoa wa Mtwara Bw, Batlomeo Masatu, Afisa Masoko wa Airtel Bi Aminata Keita, na Meneja Biashara wa kanda ya Pwani Bw Albert Majuva.
Meneja Biashara wa kanda ya Pwani Bw Albert Majuva (wakwanza kulia) akimpongeza Mshindi wa Promosheni ya Airtel yatosha Zaidi mkoani Mtwara bw, Sefu Namtapika ambae ni mwalimu mstaafu aliyeibuka na ushindi wa Toyota IST kupitia droo ya kwanza ya promosheni Yatosha zaidi inayoendesha na Airtel. Anaefuata ni Afisa Masoko wa Airtel Bi Aminata Keita na Meneja mauzo wa Airtel mkoa wa Mtwara Bw, Batlomeo Masatu wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika mkoani humo kwenye viwanja vya mashujaa mwishoni mwa wiki.
Meneja uhusiano wa Airtel bw, Jackson Mmbando akiongoza umati wa wakazi wa mkoani mtwara waliojitokeza katika viwanja vya Mashujaa kushudia hafla ya makabidhiano ya gari Toyota IST kwa mshindi wa droo ya kwanza ya promosheni ya Airtel yatosha Mzee Sefu Namtapika mwishoni mwa wiki hii.
Mshindi wa gari aina ya Toyota IST mzee Sefu Namtapika akipongezwa na mke wake Bi… mara baada ya kukabidhiwa zawadi yake ya gari alilojishindia kupitia promosheni ya Airtel Yatosha zaidi. Hafla ya makabidhiano ilifanyika katika viwanja vya mashujaa mkoani mtwara mwishoni na wiki na kuhudhuriwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara mjini mh, Wilman Kapenjama.
Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel imekabidhi Gari aina ya Toyota IST kwa mshindi wa Tatu wa droo ya kwanza Promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi inayofanyika kwa kipindi cha miezi mitatu ambapo jumla ya magari 60 yatatolewa kwa wateja wanaotumia mtandao huo.
Gari hilo la tatu limetolea kwa mshindi kutoka mkoani Mtwara ambaye ni mwalim mstaafu Seif Namtapika Katika hafla iliyofanyika katika Viwanja vya mashujaa. Namtapika amesema hakuweza kuamini mpaka hapo alipouliza katika ofisi za Airtel za mkoani hapo.


www.bukobasports.comUEFA CHAMPIONS LIGI inarudi tena dimbani Jumanne Februari 17 kwa Mechi mbili za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 wakati FC Shakhtar Donetsk ya Ukraine watakapokuwa Wenyeji wa Bayern Munich na Paris Saint-Germain kuikaribisha Chelsea ndani ya Parc des Princes Jijini Paris Nchini France.
Jumatano Raundi ya Mtoano ya Timu 16 pia itaendelea kwa Mechi mbili ambapo Mabingwa Watetezi Real Madrid watakuwa Wageni wa Schalke huko Ujerumani.
Mechi nyingine Siku hiyo ni ile ya kule Uswisi kati ya Wenyeji FC Basel 1893 na FC Porto ya Portugal.
Mechi nyingine 4 zilizobakia za Raundi hii zitachezwa Wiki ijayo.
Msimu uliopita, Chelsea iliitoa PSG kwenye Robo Fainali za UEFA CHAMPIONS LIGI kwa faida ya Bao la Ugenini baada ya kupigwa 3-1 huko Parc des Princes katika Mechi ya Kwanza.
Mechi kati ya FC Shakhtar Donetsk na Bayern Munich huko Nchini Ukraine imehamishwa toka Mji wa Nyumbani wa FC Shakhtar, Donetsk, kwenda Lviv kwa sababu Mji huo umeshikiliwa na Wapinzani katika Vita ya wenyewe kwa wenyewe Nchini humo.
Jumatano Mabingwa Real wanacheza Nyumbani kwa Schalke ambako Msimu uliopita Uwanjani hapo hapo kwenye hatua kama hii ya Mashindano haya haya Real iliinyuka Schalke 6-1.
Msimu huu, kwenye hatua ya Makundi, Schalke pia walidundwa Bao 5-0 na Chelsea hapo hapo kwao na kupenya toka hatua hiyo baada ya kuifunga Sporting Lisbon 4-3 wakati Mabingwa Watetezi Real walivuka hatua ya Makundi kwa kushinda Mechi zao zote 6.
Katika Mechi nyingine ya Jumatano, Mabingwa wa Uswisi FC Basel, ambao waliwapiku na kuwatupa nje ya Mashindano haya Liverpool katika hatua za Makundi, wanaivaa Porto ya Ureno ambayo haikufungwa hata Mechi kwenye hatua hiyo ya Makundi.
Baadhi ya Mechi nyingine za mvuto za Wiki ijayo za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ni ile ya Uwanja wa Etihad kati ya Manchester City na Barcelona hapo Februari 24 ikiwa pia ni Marudio ya Raundi kama hii ya Msimu uliopita ambayo Barcelona walishinda kwa Jumla ya Bao 4-1 katika Mechi mbili.
Siku hiyo hiyo, Mabingwa wa Italy na Vinara wa Ligi Serie A, Juventus watakuwa Wenyeji wa Borussia Dortmund iliyoanguka vibaya huko kwao kwenye Bundesliga.
Jumatano Februari 25, Arsenal ya Arsene Wenger itaivaa AS Monaco ya France ikiwa ni mara ya kwanza kwa Wenger kucheza na Klabu yake ya zamani katika Mashindano rasmi.
Mechi ya Pili ya Jumatano hiyo hiyo, ambayo itakamilisha Mechi za Kwanza za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ni kati ya Bayer Leverkusen na Atletico Madrid ambao ndio Washindi wa Pili wa UEFA CHAMPIONS LIGI Msimu uliopita.
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
RATIBA:

Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku leo
Jumanne 17 Februari 2015
FC Shakhtar Donetsk vs Bayern Munich
Paris Saint-Germain vs Chelsea FC

Jumatano 18 Februari 2015
Schalke 04 vs Real Madrid CF
FC Basel 1893 vs FC Porto 


Dakika ya 88 Wayne Rooney aliipachikia bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya kuangushwa ndani eneo la hatari na kipa wa Preston North End Thorsten Stuckmann kwenye Uwanja wao Deepdale Stadium, Preston  mtanange ukichezeshwa na Mwamuzi P. Dowd.Ushindi huu unawarudisha Man United Old Trafford kujiandaa na  Raundi ya 6 kuwakaribisha Wazee wa Mtutu wa London Gunners (Arsenal) Old Trafford kwenye Mchezo wa Robo Fanali katika igi hii ya FA Cup, Mtanange unaoonekana utakuwa wa kukata na Shoka siku hiyo.  

Kwa Timu ya Preston North End safari imeishia hapa na Wanajiandaa kuendelea na Ligi yao ya Championship.Dakika ya 73 Marouane Fellaini aliwapa bao la pili na kufanya 2-1 baada ya kupata krosi safi kutoka kwa Valencia na kupiga kwa kichwa langoni mwa Preston na kipa kuutema na kisha Fellaini kumalizia mpira huo lango na kufanya 2-1.
Dakika ya 65 Ander Herrera aliisawazishia bao Man united baada ya kupata pasi kutoka kwa Ashley Young aliyeingia kipindi cha pili akichukukuwa nafasi Radamel Falcao na kufanya 1-1.

Scott Laird akishangilia bao lake kwa Preston North End baada ya kufanya 1-0 dhidi ya United.Scott Laird dakika ya 47 anaipachikia bao Preston North End na kufanya 1-0 dhidi ya Manchester United akitanguliziwa  pasi na Joe Garner.

Mchezaji wa zamani wa Stevenage Laird akifurahia ushindi wa bao lake mapema kipindi cha pili huko kwenye Uwanja wao Deepdale
Laird is mobbed by his team-mates after giving the League One side a surprise lead against Premier League outfit Manchester United
Laird akiwa amezungukwa na kukumbatiwa chini na Wachezaji wenzake wa Preston baada ya kuipa bao.
Falcao akimtoka mchezaji wa Preston North End.

Marouane Fellaini akichuana na mchezaji wa Preston North End difenda Bailey Wright na kuumia pua baada ya kupigwa na kiwiko.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Preston North End 0-0 Manchester United.


Dakika ya 88 Wayne Rooney aliipachikia bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya kuangushwa ndani eneo la hatari na kipa wa Preston North End Thorsten Stuckmann kwenye Uwanja wao Deepdale Stadium, Preston  mtanange ukichezeshwa na Mwamuzi P. Dowd.Ushindi huu unawarudisha Man United Old Trafford kujiandaa na  Raundi ya 6 kuwakaribisha Wazee wa Mtutu wa London Gunners (Arsenal) Old Trafford kwenye Mchezo wa Robo Fanali katika igi hii ya FA Cup, Mtanange unaoonekana utakuwa wa kukata na Shoka siku hiyo.  

Kwa Timu ya Preston North End safari imeishia hapa na Wanajiandaa kuendelea na Ligi yao ya Championship.Dakika ya 73 Marouane Fellaini aliwapa bao la pili na kufanya 2-1 baada ya kupata krosi safi kutoka kwa Valencia na kupiga kwa kichwa langoni mwa Preston na kipa kuutema na kisha Fellaini kumalizia mpira huo lango na kufanya 2-1.
Dakika ya 65 Ander Herrera aliisawazishia bao Man united baada ya kupata pasi kutoka kwa Ashley Young aliyeingia kipindi cha pili akichukukuwa nafasi Radamel Falcao na kufanya 1-1.

Scott Laird akishangilia bao lake kwa Preston North End baada ya kufanya 1-0 dhidi ya United.Scott Laird dakika ya 47 anaipachikia bao Preston North End na kufanya 1-0 dhidi ya Manchester United akitanguliziwa  pasi na Joe Garner.

Mchezaji wa zamani wa Stevenage Laird akifurahia ushindi wa bao lake mapema kipindi cha pili huko kwenye Uwanja wao Deepdale
Laird is mobbed by his team-mates after giving the League One side a surprise lead against Premier League outfit Manchester United
Laird akiwa amezungukwa na kukumbatiwa chini na Wachezaji wenzake wa Preston baada ya kuipa bao.
Falcao akimtoka mchezaji wa Preston North End.

Marouane Fellaini akichuana na mchezaji wa Preston North End difenda Bailey Wright na kuumia pua baada ya kupigwa na kiwiko.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Preston North End 0-0 Manchester United.


Dakika ya 88 Wayne Rooney aliipachikia bao la tatu kwa mkwaju wa penati baada ya kuangushwa ndani eneo la hatari na kipa wa Preston North End Thorsten Stuckmann kwenye Uwanja wao Deepdale Stadium, Preston  mtanange ukichezeshwa na Mwamuzi P. Dowd.Ushindi huu unawarudisha Man United Old Trafford kujiandaa na  Raundi ya 6 kuwakaribisha Wazee wa Mtutu wa London Gunners (Arsenal) Old Trafford kwenye Mchezo wa Robo Fanali katika igi hii ya FA Cup, Mtanange unaoonekana utakuwa wa kukata na Shoka siku hiyo.  

Kwa Timu ya Preston North End safari imeishia hapa na Wanajiandaa kuendelea na Ligi yao ya Championship.Dakika ya 73 Marouane Fellaini aliwapa bao la pili na kufanya 2-1 baada ya kupata krosi safi kutoka kwa Valencia na kupiga kwa kichwa langoni mwa Preston na kipa kuutema na kisha Fellaini kumalizia mpira huo lango na kufanya 2-1.
Dakika ya 65 Ander Herrera aliisawazishia bao Man united baada ya kupata pasi kutoka kwa Ashley Young aliyeingia kipindi cha pili akichukukuwa nafasi Radamel Falcao na kufanya 1-1.

Scott Laird akishangilia bao lake kwa Preston North End baada ya kufanya 1-0 dhidi ya United.Scott Laird dakika ya 47 anaipachikia bao Preston North End na kufanya 1-0 dhidi ya Manchester United akitanguliziwa  pasi na Joe Garner.

Mchezaji wa zamani wa Stevenage Laird akifurahia ushindi wa bao lake mapema kipindi cha pili huko kwenye Uwanja wao Deepdale
Laird is mobbed by his team-mates after giving the League One side a surprise lead against Premier League outfit Manchester United
Laird akiwa amezungukwa na kukumbatiwa chini na Wachezaji wenzake wa Preston baada ya kuipa bao.
Falcao akimtoka mchezaji wa Preston North End.

Marouane Fellaini akichuana na mchezaji wa Preston North End difenda Bailey Wright na kuumia pua baada ya kupigwa na kiwiko.
Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika Preston North End 0-0 Manchester United.

waliotembelea blog