Tuesday, January 5, 2016


MENEJA wa Liverpool Jurgen Klopp yupo hatua za mwisho kukamilisha usajili wake wa kwanza wa Mchezaji mpya na huyo ni Marko Grujic.
Grujic, mwenye Miaka 19, Leo ametua Anfield kwa upimwaji wake wa afya ili kukamilisha Dili ya Pauni Milioni 5.1 kutoka Red Star Belgrade.
Inatarajiwa baada ya kukamilika kwa Uhamisho wake kwenda Liverpool, Kinda huyo atarudi kuichezea kwa Mkopo Red Star hadi mwishoni mwa Msimu na kujiunga na Liverpool kwa ajili ya Msimu ujao.
Liverpool imelazimika kufanya uamuzi wa kumnunua Grujic hivi sasa kwa sababu alikuwa akiwindwa pia na Klabu za Russia, CSKA Moscow na Zenit St Petersburg, ambazo zilitoa Dau kubwa, ikiaminika kuwa ni zaidi ya Pauni Milioni 7.

Lakini Kijana huyo aliamua mwenyewe kujiunga na Liverpool baada ya Msaidizi wa Klopp, Zeljko Buvac, ambae anatoka Serbia, kuingiliwa kati na kuleta ushawishi mkubwa kumchota Kijana huyo anaechezea Timu ya Taifa ya Serbia ya U-21.



Kamati ya maadili ya FIFA imependekeza katibu mkuu wa shirikisho hilo linalosimamia soka duniani Jerome Valcke asimamishwe kujihusisha na mchezo wa soka kwa miaka tisa.
Katibu huyo anadaiwa kutumia vibaya pesa ikiwemo uuzaji wa tiketi za kombe la duniani lililopita pamoja na kukiuka sheria za Shirikisho hilo.
Awali kamati ya nidhamu alimsimamisha katibu huyo kwa siku 90 kutojihusisha na mchezo wa soka ambapo adhabu yake imemalizika leo lakini ameongezewa adhabu kwa siku nyingine 45 wakati uchunguzi ukiendelea.
Jerome ataungana na viongozi wengine Sepp Blatter aliyekuwa Rais wa FIFA pamoja na makamu wake Michel Platini ambao wote wamesimamishwa tangu mwezi uliopita kwa miaka nane baada ya uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha kukamilika.

Mshambuliaji wa klabu ya Manchester united Wyne Rooney ametangazwa kuwa mchezaji bora kwa mwaka 2015 kwa mara nyingine.
Hii inakuwa mara ya pili staa huyo wa England kuchaguliwa mchezaji bora na mashabiki wa ligi kuu baada ya mwaka 2014 kushinda pia mwaka 2008 na  2009.
Pia kipa wa Stoke City Jack Butland amechaguliwa kuwa kipa bora kwa timu ya vijana chini ya miaka 21.
Rooney amefanikiwa kuibuka na shindi huo kwa mara nyingi baada ya kufunga jumla ya mabao 51 na kuvunja rekodi ya Bobby Charlton aliyefunga magoli 49.
Unataka kutumiwa MSG za habari zote kubwa kutoka kwa Millard Ayo? ukiwa na line ya tiGO andika ‘AYO’ tuma kwenda 15510, msg utayotumiwa jibu OK ili uanze kupokea matukio yote kwa sms, pia ungana na Millard Ayo kwenye Twitter, FB, Instagram na YouTUBE wa kubonyezahapa>>>INSTAGRAM TWITTER FB YOUTUBE.

Kocha wa klabu ya FC Bayern Munich ya Ujerumani Pep Guardiola December 29 aliingia kwenye headlines baada ya kutua Kenya kwa ajili ya mapumziko ya sikukuu ya Christimas na mwaka mpya, ujio wake Kenya uliwashangaza wengi kutokana na kuja kimya kimya. Ninazo pichaz za Pep Guardiola akitalii Kenya wakati ambao vilabu vya Chelsea na Man United vikitajwa kwa kiasi kikubwa kumuhitaji kocha huyo kwa ajili ya msimu ujao.
CXyZFP-WYAAvYTJ
Lakini Man City wanatajwa kuingia nae mkataba wa awali. Pep Guardiola ambaye aliwahi kuifundisha klabu ya FC Barcelona na sasa FC Bayern Munich ya Ujerumani amethibitisha kuwa hatoendelea kuifundisha Bayern Munich baada ya msimu kumalizika, hivyo wengi wanasubiria ataenda kuifundisha klabu gani baada ya FC Bayern Munich?
1919039_621862621288508_8491208548875364896_n
CXuOrMiWYAArySp
CXuOumqWMAASXK9

waliotembelea blog