Wednesday, December 31, 2014


Na Bertha Lumala, Dar es Salaam
Vinara wa msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Mtibwa Sugar FC wamewaahidi wapenzi wa soka visiwani Zanzibar kufurahia makali yao ya msimu huu watakaposhiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi mwakani.


Mtibwa Sugar FC, mabingwa wa Tanzania Bara 1999 na 2000, ni miongoni mwa timu nne za VPL zilizoalikwa na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) kushiriki michuano hiyo itakayoanza Januari 1-13 mwakani.
Msemaji wa Mtibwa Sugar FC, Thobias Kifaru, amesema kikosi chao bado kiko Manungu, Turiani, km 100 kutoka mjini Morogoro na muda wowote leo Jumatano kitaanza safari kuelekea Zenj.

"Tumefanya vizuri katika Ligi Kuu ya Vodacom. Wazanzibar watarajie utamu kutoka kwetu. Tunahamishia makali yetu ya Bara huko Zanzibar," amesema Kifaru.
Mbali na timu nne zaa Tanzania Bara. Mtibwa, AzamFC, Yanga SC na Simba SC, timu nyingine nane zimealikwa kushiriki michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya tisa tangu ianzishwe kuenzi Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar yaliyofanyika Januari 12, 1964.


Timu hizo ni pamoja na mabingwa watetezi KCC FC ya Uganda, mabingwa wa Zanzibar KMKM, Mafunzo FC, Shaba FC ya Pemba, Police Zanzibar, Mtende Rangers, JKU FC na Ulinzi FC ya Kenya huku mabingwa mara 19 wa Ligi Kuu ya Sudan, El Merrikh wakiomba pia kushiriki.

MOTO WA BURUDANI KUWAKA COCO BEACH MWAKA MPYA


Wapenzi wa burudani ya muziki wa kizazi kipya watapata burudani ya fungua mwaka kutoka kwa magwiji wa muziki wa kizazi kipya ambao wanatamba nchini katika tamasha la wazi la maisha murua na Vodacom katika ufukwe wa Coco beach jijini Dar es Salaam.Baadhi ya magwiji hao ni Profesa J,Temba,Chege,Roma Mkatoliki na wengineo wengi.
Tamasha hili litakalokutanisha magwiji wa bongo fleva ambalo limeanza kuwa gumzo la jiji kutokana na kuwa na burudani za aina mbalimbali kwa ajili ya kukonga nyoyo za wapenzi wa burudani limeandaliwa na Vodacom Tanzania.


MSIMAMO ULIVYO:
PosLogo &TeamPWDLGDPts
1ChelseaChelsea1914412746
2Manchester CityManchester City1913422443
3Manchester UnitedManchester United1910631436
4SouthamptonSouthampton1910361733
5ArsenalArsenal199641133
6West Ham UnitedWest Ham United19946731
7Tottenham HotspurTottenham Hotspur19946031
8LiverpoolLiverpool19847128
9Swansea CitySwansea City19847128
10Newcastle UnitedNewcastle United19757-626
11Stoke CityStoke City19748-225
12EvertonEverton19568-221
13Aston VillaAston Villa19568-1121
14SunderlandSunderland193115-1120
15Queens Park RangersQueens Park Rangers195311-1318
16West Bromwich AlbionWest Bromwich Albion194510-1017
17Hull CityHull City19379-816
18Crystal PalaceCrystal Palace19379-1016
19BurnleyBurnley19379-1516
20Leicester CityLeicester City193412-1413

Monday, December 29, 2014


Mshambuliaji wa Chelsea na Spain Fernando Torres atajiunga moja kwa moja na AC Milan hapo Januari 5.
Torres, mwenye Miaka 30, alijiunga na AC Milan ya Italy kwa Mkopo tangu Mwezi Agosti lakini sasa Mkataba utabadilishwa na kujiunga kwa kudumu na Klabu hiyo ya Serie A.

Torres alijiunga na Chelsea kutoka Liverpool Januari 2011 katika Uhamisho ulioweka Rekodi ya Uingereza wakati huo wa Dau la Pauni Milioni 50.

Akiwa na Chelsea, Torres alifanikiwa kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI, EUROPA LIGI na FA CUP.
Kwenye Taarifa yao, Chelsea wamemshukuru Torres kwa utumishi wake kwao wa Miaka Minne na kumtakia kila la kheri katika maisha yake ya baadae.

 Ac Milan yajipanga kumchukua moja kwa moja

Torres alishaichezea Atletico Madrid dhidi ya  Barcelona kipindi cha nyuma mwaka  2006.
Lakini, habari za ndani zinadai Torres hatakaa AC Milan bali atapelekwa kwa Mkopo huko Spain kwenye Klabu yake ya zamani Atletico Madrid katika Dili ya kumbadili yeye na Straika wa Atletico Madrid Alessio Cerci ambae atatua AC Milan.
Dili hiyo itamfanya Torres aende Atletico kwa Mkopo wa Miezi 18 na Cerci, ambae ni Winga wa zamani wa Torino, atue AC Milan kwa Mkopo wa Miezi 6.
Tangu atue AC Milan, Torres amefunga Bao 1 tu kwenye Ligi Serie A katika Mechi 10 na hivi sasa ametupwa nje ya Kikosi cha Kwanza wakati Cerci nae hana namba huko Atletico.
Hivi sasa Ligi ya Serie A imesimama kwa mapumziko ya Krismasi na Mwaka mpya na itarejea hapo Januari 5.

Torres pia alishaichezea Liverpool kabla ya kwenda Chelsea kwa  £50million mwezi  January 2011

Saturday, December 27, 2014


Chini ya Uongozi wa Mtunzi na Mwimbaji Mahiri na mtunzi bora wa mwaka wa Kili Music Awards Christian Bella ilipotumbuiza mamia ya wapenzi wao katika ukumbi wa Raha Bukoba wa Lina's Night  Club akiwa sambamba na  Safu yake ya  ushambuliaji ya Malaika Band. 
BENDI ya muziki wa Dansi ya Malaika chini ya Christian Bella ‘Obama’ usiku huu ilitoa Burudani kali ya kukata na shoka kwenye ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba ikiwa ni kumalizia sikukuu za X-mass siku ya Boxing Day" na kuwapagawisha mashabiki kwa shoo kali na ya nguvu.
Onyesho hilo lililoanza saa mbili usiku ambapo Malaika Bendi walikuwa wakiwapa ladha mashabiki kwa kupiga kopi mbalimbali ya nyimbo za Kikongo zinazobamba.
Ilipofika saa nne na nusu ukumbi ulilipuka kwa shangwe baada ya kiongozi wa bendi hiyo Christian Bella kupanda jukwaani kwa wimbo wake wa Yako Wapi Mapenzi ambao ulisababisha mashabiki kuinuka katika viti vyao na wale ambao walikuwa wakinyemelewa na usingizi kuamka.
Bella alizidi kuwapagawisha mashabiki kwa kupiga nyimbo kali mfululizo ambazo zinatamba katika redio na vyombo mbalimbali vya habari ukiwemo Nani Kama Mama, Yako wapi Mapenzi, Msaliti, Usilie na nyingine kibao.
Mfalme wa masauti, Christian Bella ‘Obama’ akifanya yake usiku huu siku ya sikukuu Boxing Day kwenye Ukumbi wa Lina's Night Club, Bukoba uliopo Bukoba mjini.
Madansa wa Malaika Music bendi wakifanya yao.
Christian Bella Christian Bella 'Obama' achengua mashabiki kwa kutoa Burudani kwa kuimba wimbo wa Nani kama Mama ambao uliamsha Shamra Shamra katika Ukumbi wa Lina's Night Club usiku huu wa Boxing Day' katika kumalizia sikukuu za x-mass na kusonga kuoona mwaka Mpya 2015.
Wanenguaji wa Malaika Band wakiwajibika kwenye ukumbi wa Lina's Night Club usiku huu wa
Boxing Day Ijumaa.


Chini ya Uongozi wa Mtunzi na Mwimbaji Mahiri na mtunzi bora wa mwaka wa Kili Music Awards Christian Bella ilipotumbuiza mamia ya wapenzi wao katika ukumbi wa Raha Bukoba wa Lina's Night  Club akiwa sambamba na  Safu yake ya  ushambuliaji ya Malaika Band. 
BENDI ya muziki wa Dansi ya Malaika chini ya Christian Bella ‘Obama’ usiku huu ilitoa Burudani kali ya kukata na shoka kwenye ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba ikiwa ni kumalizia sikukuu za X-mass siku ya Boxing Day" na kuwapagawisha mashabiki kwa shoo kali na ya nguvu.
Onyesho hilo lililoanza saa mbili usiku ambapo Malaika Bendi walikuwa wakiwapa ladha mashabiki kwa kupiga kopi mbalimbali ya nyimbo za Kikongo zinazobamba.
Ilipofika saa nne na nusu ukumbi ulilipuka kwa shangwe baada ya kiongozi wa bendi hiyo Christian Bella kupanda jukwaani kwa wimbo wake wa Yako Wapi Mapenzi ambao ulisababisha mashabiki kuinuka katika viti vyao na wale ambao walikuwa wakinyemelewa na usingizi kuamka.
Bella alizidi kuwapagawisha mashabiki kwa kupiga nyimbo kali mfululizo ambazo zinatamba katika redio na vyombo mbalimbali vya habari ukiwemo Nani Kama Mama, Yako wapi Mapenzi, Msaliti, Usilie na nyingine kibao.
Mfalme wa masauti, Christian Bella ‘Obama’ akifanya yake usiku huu siku ya sikukuu Boxing Day kwenye Ukumbi wa Lina's Night Club, Bukoba uliopo Bukoba mjini.
Madansa wa Malaika Music bendi wakifanya yao.
Christian Bella Christian Bella 'Obama' achengua mashabiki kwa kutoa Burudani kwa kuimba wimbo wa Nani kama Mama ambao uliamsha Shamra Shamra katika Ukumbi wa Lina's Night Club usiku huu wa Boxing Day' katika kumalizia sikukuu za x-mass na kusonga kuoona mwaka Mpya 2015.
Wanenguaji wa Malaika Band wakiwajibika kwenye ukumbi wa Lina's Night Club usiku huu wa
Boxing Day Ijumaa.

Dada nao hawakuwa nyuma



Jamal na Mkewe nao walikuwepo ukumbin Lina's Night Club kushuhudia Bendi hiyo LiveJamal kalumuna akiwa meza kuu

Mtu wa Watu Ben Mulokozi


Nyomi ya Mashabiki walijitokeza kwa wingi katika Ukumbi huo wa Burudani Lina's Night Club.










Wadau wa Muziki wa Dansi...Bendi..

Wafanyakazi wa shirika la Cosad nao walitokelezea kwa namna yao siku ya Boxing Day na hapa walipata picha na Bella
Vinywaji vilitembea ukumbini hapo
Wadau
usipime!


Mwandaaji wa Shoo Mc Jerry akitokelezea na Mkali wa Masauti Bella



waliotembelea blog