Saturday, July 2, 2016



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kulia) akifungua Kikao cha Uongozi cha Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (wa tatu toka kushoto) akiongea na Viongozi wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakati wa Kikao cha Uongozi kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kulia) akimweleza jambo Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya CPA Kanda ya Afrika, Mhe. Lindiwe Maseko (Mb) (kushoto) kutoka Afrika Kusini wakati wa Kikao Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakati wa Kikao cha Uongozi cha Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.

Baadhi ya Wajumbe na Sekretarieti ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakifuatilia agenda za kikao kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya CPA Kanda ya Afrika, Mhe. Lindiwe Maseko (Mb) wakati wa Kikao cha Uongozi cha Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.
Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya CPA Kanda ya Afrika, Mhe. Lindiwe Maseko (Mb) (aliyekaa mbele) akiongea Viongozi wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakati wa Kikao cha Uongozi kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.

Sekretarieti ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakifuatilia agenda za kikao kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya CPA Kanda ya Afrika, Mhe. Lindiwe Maseko (Mb) wakati wa Kikao cha Uongozi cha Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.

Baadhi ya Wajumbe walioshiriki katika Kikao cha Kikao cha Uongozi cha Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakifuatilia agenda ya kikao hico kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.

Wajiumbe wa Kikao cha Uongozi wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Afrika wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (wa tatu kulia waliokaa mbele) mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam, 02 July, 2016.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, ajira, vijana na wenye ulemavu), Jenista Mhagama, (kulia), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), kwenye maonyesho ya 40 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, Julai 2, 2016. Kulia ni Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Fulgence Sebera.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, (katikati), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), kwenye maonyesho ya 40 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, Julai 2, 2016. Kulia ni Afisa Uhusiano wa WCF, Zaria Mmanga, na kushoto ni Mhasibu wa Mfuko huo, Grace Tarimo

NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, ameutaka Mfuko wa Fidia Kwa Wafanyakazi, (WCF), kujiweka tayari kulipa mafao ya Fidia kwa Wafanyakazi kama ambavyo Sheria ilivyoelekeza.Waziri Mhagama aliyasema hayo leo Julai 2, 2016 wakati alipokuwa kwenye ziara ya kutembelea Mifuko ya Hifadhi ya Jamii inayoshiriki kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iko chini ya Ofisi yake.

“Najua mnatakiwa kuanza kulipa fidia mwezi huu wa Julai, vipi mko tayari na kama bado basi mjiweke tayari kufanya hivyo.” Alisema Waziri.

Akimjibu Waziri Mhagama ambaye alifuatana na maafisa wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, (SSRA), wakiongozwa na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Mamlaka hiyo, Sarah Kibonde Msika, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa WCF, Fulgence Sebera alimwambia Waziri kuwa Mfuko umejiandaa kikamilifu kutoa fidia kwa wafanyakazi ambapo elimu ilitolewa kwa wadau wengi wakiwemo madaktari kote nchini watakaowafanyia tathmini wafanyakazi waliopata madhara mahala pa kazi.

Sebera pia alitoa wito kwa wadau kutembelea banda la WCF ili kujipatia maelezo ya kina ,kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko huo ikiwemo Fidia kwa Wafanyaakzi ambayo inaanza kutolea Julai mosi mwaka huu wa 2016.Banda la WCF liko kwenye ukumbi wa Sabasaba kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere.
Waziri akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakzi wa WCF, na maafisa wa SSRA.

Waziri akiagana na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano, Wizara ya Fedha na Mipango, Ben Mwaipaja, baada ya kutembelea Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwenye Jengo la Wizarabya Fedha, kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, Julai 2, 2016. Kushoto ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano cha SSRA, Sarah Kibonde Msika.

Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akimkaribisha kwa mazungumzo Ofisini kwake katika Jengo la SMZ Magogoni Jijiji Dar es salaam Balozi wa Jamuhuri ya Watu wa China Bwana Lu Youqing.
Balozi wa Jamuhuri ya Watu wa China Bwana Lu Youqing kati kati akielezea mikakati atakayoitekeleza katika kuratibu usimamizi wa miradi ya Zanzibar iliyopata ufadhili wa Nchi yake ya China.
Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akibadilishana mawazo na Balozi wa Jamuhuri ya Watu wa China Bwana Lu Youqing mara baada ya mazungumzo yao ya kuimarisha ushirikiano kati ya Zanzibar na China.Picha na – OMPR – ZNZ.

Balozi wa Jamuhuri ya Watu wa China Nchini Tanzania Bwana Lu Youqing ameahidi kufanya jitihada za makusudi katika kufuatilia taratibu za Mikataba ya makubaliano kwa upande wa Nchi yake ili kuona kwamba miradi yote ya Zanzibar iliyopata ufadhili wa Nchi hiyo inaanza, inaendelea na kukamilika kwa wakati uliopangwa.

Akizungumza na Makamu wa Pili wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipomtembelea Ofisini kwake katika Jengo la SMZ Magogoni Jijiji Dar es salaam Balozi Lu Youqing aliitaja baadhi ya miradi hiyo kuwa ni pamoja na ujenzi wa Bandari ya Mpiga Duri, ukamilishaji wa ujenzi wa eneo la maegesho ya Ndege kwenye uwanja wa ndege wa Zanzibar pamoja na Mradi wa Kisasa wa mawasiliano kwenye ofisi zote za SMZ { E government }.

waliotembelea blog