Thursday, October 9, 2014


Mshambuliaji wa kimataifa wa Arsenal, Mezut Ozil, ameondoka leo kutoka katika kambi aliyokuwa na timu yake ya taifa ya Ujerumani huko mjini Frankfurt na kuelekea mjini Munich kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi wa maumivu ya goti yanamsumbua kwa sasa ambayo ameyapata wakati akifanya mazoezi na timu yake hiyo ya taifa ikiwa ni maandali ya kuelekea katika mashinda ya kuwania kufuzu kushiriki michuano ya mataifa ya Ulaya 2016.
Ozil alikuwa ni sehemu ya kikosi cha Ujerumani, mabingwa wa kombe la dunia msimu uliopita, ambao walikuwa wanajiandaa kukipiga dhidi ya Poland na baadaye Jamuhuri ya Iland kuwani tiketi za kushiriki fainali za mataifa ya Ulaya ya 2016, lakini ndoto zake za kuendelea kuwa sehemu ya kikosi hicho zinaonekena kufifia kwa sababu ya majeraha hayo ambayo mpaka sasa haijawekwa bayana kwamba itamuweka nje ya dimba kwa muda gani.
Hili pia linaweza kumpa Arsene Wenger presha, kwa kuwa Ozil ni mmoja kati ya wachezaji anao wategemea sana kikosini hapo kwa sasa baada ya kuwa na idadi kubwa ya majeruhi mapema sana msimu huu. Wachezaji wengine ambao ni majeruhi katika klabu ya Arsenal mbali na Mesut Ozil ni; Olivia Giroud, Mathieu Debuchy Aron Ramsey, Mikel Arteta pamoja naye Theo Walcott ingawaje baahi yao wanaweza kurudi uwanjani muda mfupi.

MAKUNDI:
KUNDI A:
Netherlands, Czech Republic, Turkey, Latvia, Iceland, Kazakhstan.
KUNDI B: Bosnia-Hercegovina, Belgium, Israel, Wales, Cyprus, Andorra.
KUNDI C: Spain, Ukraine, Slovakia, Belarus, FYR Macedonia, Luxembourg.
KUNDI D: Germany, Republic of Ireland, Poland, Scotland, Georgia, Gibraltar.
KUNDI E: England, Switzerland, Slovenia, Estonia, Lithuania, San Marino.
KUNDI F: Greece, Hungary, Romania, Finland, Northern Ireland, Faroe Islands.
KUNDI G: Russia, Sweden, Austria, Montenegro, Moldova, Liechtenstein.
KUNDI H: Italy, Croatia, Norway, Bulgaria, Azerbaijan, Malta.
KUNDI I: Portugal, Denmark, Serbia, Armenia, Albania.


Timu mbili za juu toka kila Kundi pamoja na Timu moja Bora iliyoshika Nafasi ya 3 kwenye Makundi zitatinga Fainali na Timu 8 zilizobaki ambazo zitamaliza Nafasi ya Tatu zitapangiwa Mechi maalum za Mchujo ili kupata Timu 4 za mwisho kuingia Fainali.
Mechi za Makundi zilianza Septemba 2014 na zitaendelea hadi Oktoba 2015.

EURO 2016
RATIBA:

Alhamisi Oktoba 9
21:45 Slovenia vs Switzerland KUNDI E
21:45 Moldova vs Austria KUNDI G
21:45 Belarus vs Ukraine KUNDI C
21:45 Sweden vs Russia KUNDI G
21:45 Lithuania vs Estonia KUNDI E
21:45 Macedonia vs Luxembourg KUNDI C
21:45 Liechtenstein vs Montenegro KUNDI G
2145 England vs San Marino KUNDI E
2145 Slovakia vs Spain KUNDI C


Ijumaa Oktoba 10
2145 Cyprus vs Israel KUNDI B
2145 Malta vs Norway KUNDI H
2145 Netherlands vs Kazakstan KUNDI A
2145 Latvia vs Iceland KUNDI A
2145 Turkey vs Czech Republic KUNDI A
2145 Bulgaria vs Croatia KUNDI H
2145 Belgium vs Andorra KUNDI B
2145 Wales vs Bosnia And Herzegovina KUNDI B
2145 Italy vs Azerbaijan KUNDI H


Jumamosi Oktoba 11
19:00 Romania vs Hungary KUNDI F
19:00 Scotland vs Georgia KUNDI D
19:00 Armenia vs Serbia KUNDI I
19:00 Ireland vs Gibraltar KUNDI D
2145 Poland vs Germany KUNDI D
2145 Northern Ireland vs Faroe Islands KUNDI F
2145 Finland vs Greece KUNDI F
2145 Albania vs Denmark KUNDI I

Jumapili Oktoba 12
1900 Austria vs Montenegro KUNDI G
1900 Estonia vs England KUNDI E
1900 Russia vs Moldova KUNDI G
1900 Ukraine vs Macedonia KUNDI C
2145 Luxembourg vs Spain KUNDI C
2145 Belarus vs Slovakia KUNDI C
2145 Sweden vs Liechtenstein KUNDI G
2145 Lithuania vs Slovenia KUNDI E


Jumatatu Oktoba 13

19:00 Kazakstan vs Czech Republic KUNDI A
21:45 Malta vs Italy KUNDI H
21:45 Norway vs Bulgaria KUNDI H
21:45 Bosnia And Herzegovina vs Belgium KUNDI B
21:45 Latvia vs Turkey KUNDI A
21:45 Iceland vs Netherlands KUNDI A
21:45 Croatia vs Azerbaijan KUNDI H
21:45 Andorra vs Israel KUNDI B
21:45 Wales vs Cyprus KUNDI B

Jumanne Oktoba 14
21:45 Denmark vs Portugal KUNDI I
21:45 Poland vs Scotland KUNDI D
21:45 San Marino vs Switzerland KUNDI E
21:45 Germany vs Ireland KUNDI D
21:45 Faroe Islands vs Hungary KUNDI F
21:45 Greece vs Northern Ireland KUNDI F
21:45 Finland vs Romania KUNDI F
21:45 Serbia vs Albania KUNDI I
21:45 Gibraltar vs Georgia KUNDI D


Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam leo,juu ya onyesho la Redd's Miss Tanzania 2014 linalotarajiwa kufanyika Oktoba 11,2014 katika Ukumbi wa Mlimani City,Jijini Dar.Katikati ni Meneja wa Kinywaji cha Redd's ambao ni Wadhamini Wakuu wa Mashindano hayo,Victoria Kimaro na kushoto ni Meneja Maria Stopes Tanzania,Anna Shanalingigwa.Picha zote na Othman Michuzi.

Meneja wa Kinywaji cha Redd's ambao ni Wadhamini Wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Victoria Kimaro (kushoto) akizungumzia zawadi watakayotoa kwa Washindi watakaopatikana kwenye Shindano hilo la Redd's Miss Tanzania 2014,ambapo mwaka huu mshindi wa kwanza katika kinyang'anyiro hicho atajinyakulia kitita cha sh. Mil. 18 taslim huku washindi wengine wakiendelea kuondoka na zawadi mbali mbali.Katikati ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga na kulia ni Meneja wa Hoteli ya JB Belmont,Gillian Macheche pamoja na Afisa Habari wa Miss Tanzania,Hidan Ricco.

Sehemu ya Wanahabari pamoja na Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014 wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Kampuni ya Rino International Agency ambao ni waratibu wakuu wa Mashindano ya Miss Tanzania,Hashim Lundenga alipokuwa akizungumza.




Sehemu ya Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014

Warembo watakaoshiriki kwenye kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania 2014 wakipata "SELFIE" mwanana kabisa.

waliotembelea blog