Sunday, June 22, 2014


Xabi Alonso, Kiungo wa Real Madrid, ametangaza kustaafu kuichezea Nchi yake Spain.
Alonso, Miaka 32, amekuwa mmoja wa kiini cha mafaniko ya Spain iliyotwaa EURO 2008 na EURO 2012 pamoja na Kombe la Dunia huko Afrika Kusini Mwaka 2010.
Juzi Alonso aliichezea Spain Mechi yake ya 112 ilipofungwa 2-0 na Chile kwenye Mechi Kundi B na kutupwa nje ya Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.

Kwenye Mechi hiyo, Alonso alibadilishwa wakati wa Mapumziko baada kupwaya na kupokonywa Mpira uliozaa Bao la Kwanza la Chile.
Lakini Alonso ndie Mchezaji pekee aliewafungia Spain Bao pekee kwenye Mashindano haya huko Brazil alipofunga kwa Penati kwenye Mechi ya Kwanza ya Kundi B waliponyukwa Bao 5-1 na Netherlands.

Mara baada ya Spain kutupwa nje ya Fainali ya Kombe la Dunia, Alonso alisema: “Vitu vinabadilika. Zama zinaisha kwa kufungwa…na hiki kilikuwa kipigo kichungu. Hatukutegemea lakini ndio mchezo. Hivi vitu vinatokea. Hatukutegemea lakini ni lazima tuyakabili majonzi yetu vile vile kama tunavyofurahia, kama Wanaume.”

Aliongeza: “Tumecheza dhidi ya Timu zilizojitayarisha vyema na sasa tunarudi nyumbani. Inauma lakini huu ndio mpira. Kama nilivyosema, tulijua namna ya kushinda, sasa inabidi tujue namna ya kushindwa!”

Mbali ya Alonso kutangaza kustaafu pia kuna wasiwasi kuwa Kiungo Xavi na Kipa Iker Casillas, ambao wote wamecheza ovyo huko Brazil, wanaweza kufuata nyayo zake.
Zipo habari kuwa Kocha wa Spain, Vicente del Bosque, hasa kwa vile Shirikisho la Soccer la Spain, RFEF, linaunga mkono aendelee na kazi yake.


KUHUSU REKODI YA XABI ALONSO
BORN: Tolosa, Spain, November 25, 1981

1999-2000: Real Sociedad B (39 apps, 2 gls)
1999-2004: Real Sociedad (114 apps, 9 gls)
2000-2001: Eibar (loan) (14 apps, 0 gls)
2004-2009: Liverpool (143 apps, 15 gls)
2009-NOW: Real Madrid (158 apps, 4 gls)



2003-NOW: Spain (112 caps, 16 gls)
CLUB HONOURS:

LIVERPOOL - FA Cup (2006), FA Community Shield (2006), Champions League (2005), UEFA Super Cup (2005)
REAL MADRID - La Liga (2012), Copa del Rey (2011, 2014), Supercopa de Espana (2012), Champions League (2014)
SPAIN - World Cup (2010), European Championship (2008, 2012)

WORLD CUP 2014: NIGERIA 1 vs BOSNIA-HERZEGOVINA 0, PETER ODEMWINGIE AWAPATIA USHINDI NIGERIA..

1-0, Peter Odemwingie kushoto akishangilia bao lake lililotosha kuwapatia alama 3 muhimu na kuwawezesha kuwa na jumala ya pointi 4 na wako nafasi ya pili kwenye kundi lao na mtanange ujao kwa Nigeria ni jumatano tarehe 25 saa moja kamili.Peter Odemwingie dakika ya 29 aliifungia bao timu yake baada ya kazi nzuri ya Emenike kwa kuwakacha mabeki wa Bosnia na kumpa pasi Odemwingie na kufunga bao huku wachezaji wa Bosnia wakishindwa kuamini bao hilo.
Mchezaji wa Bosnia midfielder Izet Hajrovic akipitwa na mchezaji wa Nigeria difenda Juwon Oshaniwa na kwenda eneo la hatari la kipa na kugawa pasi kwa Peter Odemwingie

waliotembelea blog