Thursday, October 8, 2015


Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe pamoja na Tundu Lissu.
Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe pamoja na Tundu Lissu.
Tume ya Taifa ya uchaguzi nchini (NEC) imewataka wananchi kutosimama katika vituo vya kupigia kura mara baada ya kupiga kura oktoba 25 kufuatia viongozi wa Chama cha Demokrasia  na Maendeleo kuwataka Wananchi kukaa umbali wa mita 100 umbali unaokubalika kisheria baada ya kupiga kura ili wazilinde kura zao.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva alipokuwa akifungua mkutano wa tume na waratibu wa uchaguzi wa mikoa, wasimamizi wa uchaguzi na makamanda wa polisi nchini amesema kwamba haina haja ya wanachama kulinda kura kwa kuwa mawakala wa vyama vya siasa watakuwepo katika vituo vya kupigia kura ili kulinda maslahi ya chama pamoja na wagombea wao.
Jaji Lubuva amesema kuwa wajibu wa mawakala ni kuangalia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa na Tume zinazingatiwa katika mchakato mzima wa kupiga kura, kuhesabu kura na kutangaza matokeo na pia kulinda maslahi ya chama au wagombea wao.
“Changamoto zilizojitokeza katika chaguzi zilizopita ni pamoja na kuwapo na makundi ya vijana wanaohisiwa kuwa ni wafuasi wa vyama vya siasa kuwatisha wapiga kura hasa wakinamama ili wasiende kupiga kura”
<a href='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/ck.php?n=a08724c9&cb=Math.random()' target='_blank'><img src='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/avw.php?zoneid=19&source=https%3A%2F%2Fmpakasi.com&cb=Math.random()&n=a08724c9' border='0' alt='' /></a>
Mbali na hayo Jaji Lubuva amesema lengo la kushirikisha Jeshi la polisi kwenye uchaguzi mkuu ni kutambua na kuhakikisha kuwepo kwa hali ya usalama na amani wakati wa uchaguzi kwani uchaguzi huru na wa haki ni lazima uendeshwe katika hali ya utulivu na amani.
Naye Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Ernest Mangu amesema kuwa jukumu la jeshi la polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zao, kuimarisha ulinzi katika vipindi vyote na haswa kipindi hiki cha uchaguzi, kulinda vifaa vya uchaguzi na kusimamia usalama katika vituo vya kupigia kura.




Yale yake unaweza kusema hivyo baada ya mchezaji wa timu ya taifa ya mchezo wa raga ya Afrika Kusini kumng’ata mwenzake.


Kupitia picha iliyopigwa na Kevin Quigley, inaonyesha mchezaji wa Afrika Kusini ‘Springboks’, Frans Malherbe akididimiza meno yake kwneye bega la Matt Trouville wa timu ya taifa ya Marekani wakati wakiwania mpira.

Usisahau, siku chache zilizopita kumekuwa na gumzo la beki wa Mbeya City, Juma Nyosso kumtomasa makalio nahodha wa Azam FC, John Bocco. Tayari Nyosso amekumbana na adhabu ya kufungiwa miaka miwili na faini ya Sh milioni 2.

Hata hivyo, kitu kizuri zaidi, Trouville ambaye aling’atwa amewaeleza waamuzi kwamba hakumbuki kuhusiana na tukio hilo kwa kuwa alikuwa amevaa kifaa maalum cha kulinda mabega ambacho huvaliwa an wachezaji wa mchezo huo.

Bado haijajulikana kama Malherbe atakumbana na adhabu, au suala la muhusika yaani aliyeumwa kusema hakumbuki, linaweza kumuokoa.

 Mshindi wa jumla wa shindano la Serengeti Masta Said Kanolo (katikati) akifurahi na wadau wa bia ya Serengeti Premium Lager, wakati wa shindano la mwisho la Serengeti Masta kwa wateja wa kanda ya ziwa lililofanyika katika baa ya Shooters iliyopo barabara ya Airport jijini Mwanza. Kampeni hiyo ya Serengeti Masta imedumu katika kanda hiyo kwa takriban muda wa miezi (2) sasa ikiwakutanisha wateja na meneja wa bia hiyo katika kujifunza kwa undani kuhusiana na bia hiyo ambapo zawadi mbalimabli zilipatikana.
Wadau wa bia ya Serengeti Premium lager wakigonga cheers, ndani ya baa ya Shooters iliyopo barabara ya Airport jijini Mwanza wakati wa shindano la mwisho la kumtafuta Serengeti Masta wa jumla kwa mikoa ya kanda ya ziwa katika baa hiyo. Kampeni ya “Serengeti Masta” imedumu katika kanda hiyo kwa takriban miezi miwili na imezunguka baa kwa baa kusaka washindi mbalimbali wanaotambua ladha halisi ya bia hiyo lakini pia imetoa elimu kwa wateja wake kuhusiana na chapa hiyo namba moja kutoka SBL.  
 Mshindi wa jumla washindanola Serengeti Masta kwa wakazi wa kanda ya ziwa Said Kanolo (kushoto) akipokea fedha taslim Tsh. 100,000/= kutoka kwa Afisa mauzo wa Kampuni ya bia ya Serengeti Joan Semguruma, (kulia) wakati wa shindano la mwisho kwa kanda ya ziwa la bia hiyo lililofanyika katika baa ya Shooters iliyopo Barabara ya Airport jijini Mwanza. Ushindi wa jumla wa Bw. Kanolo kwa wateja wa kanda ya ziwa umekuja baada ya kuwashinda wateja wengi walioshiriki katika kutambua ladha halisi ya bia hiyo na kuielezea kwa undani ambapo mwanzo wa Kampeni alishinda Tsh. 50,000/= pamoja na zawadi nyingine kutoka bia ya Serengeti Premium Lager katika baa ya Cross parkjijini Mwanza nakufanikiwakutingafainali. Kampeni hii imezunguka katika baa mbalimbali za kanda ya ziwa ikiwaburudisha wateja wa bia hiyo na kuwafundisha wahudumu wa baa mbalimbali juu ya utoaji huduma kwa wateja.


Mwanamziki wa Uingereza,Arjun Coomeraswamy akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani)juu ya ujio na kukutana na watu mbalimbali katika Ukumbi wa Viva Tower jijini Dar es Salaam na  Jumamosi atafanya shoo Zanzibar katika ukumbi wa Kendwa Rocks Beach Resort iliyofanyika leo katika ukumbi wa New Afrika jijini Dar es Salaam.
Mkuu Kitengo  wa kinywaji cha John Worker na Masoko na uboreshaji,Stanley Samtu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  juu ya udhamini wa mwanamziki huyo iliyofanyika leo katika ukumbi wa New Afrika jijini Dar es Salaam,Kulia ni Mwanamziki wa Uingereza,Arjun Coomeraswamy ,kushoto ni Mwanamziki,Lina Sanga .
 Mwanamziki,Lina Sanga akizungumza leo jijini Dar es Salaam.


Masaa machache baada ya Rais wa FIFA Sepp Blatter kusimamishwa kuliongoza shirikisho hilo, kiongozi wa shirikisho la soka Afrika Issa Hayatou kutoka Cameroon amepewa jukumu la kuongoza shirikisho hilo kwa muda.
Hayatou atachukua nafasi hiyo kufuatia kusimamishwa kazi kwa Rais wa FIFA Sepp Blatter kwa muda wa siku 90 na Kamati ya Maadili ya shirikisho hilo.
Hayatou, ambaye aliongoza CAF tangu mwaka 1988, pia alikuwa makamu wa rais katika kamati ya utendaji ya Fifa aliyehudumu muda mrefu zaidi.
Blatter amesimamishwa kwa muda wa siku 90 kufuatia kashfa mpya ambayo imeibuka hivi karibuni ndani ya shirikisho hilo ikihusisha malipo ya fedha ambazo ziliandikishwa kwa akaunti ya rais wa shirikisho la vyama vya soka barani Ulaya Michel Platinni
Rais mpya wa FIFA atapatikana Februari 26, 2016.


Lionel Messi na Neymar, watakuwa nje wakati Nchi zao Argentina na Brazil zikianza Mechi zao za kwanza za Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini kusaka nafasi za kucheza Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Russia hapo Alhamisi.
Messi ataikosa Messi ya Argentina na Ecuador kwa vile ni majeruhi wakati Neymar ataikosa Mechi ya Nchi yake Brazil ikicheza Ugenini na Chile zikiwa ni Mechi za kwanza ambazo zitachezwa Alhamisi.
Mbli ya kwamba Mechi hizi ni muhimu kwenye Kundi hili lenye Nchi 10 ambazo 4 za juu ndizo hufuzu moja kwa moja kwenda Finali za Kombe la Dunia, Brazil na Argentina zina deni kwa Washabiki wao baada ya kufanya vibaya kwenye Copa America.
Copa America, Mashindano ya Mataifa ya Nchi za Marekani ya Kusini, yalifanyika Mwezi Juni na Julai Nchini Chile ambapo Wenyeji hao walibeba Kombe baada ya kuwabwaga kwa Mikwaju ya Penati Argentina.

Kwenye Mashindano hayo, Brazil walitolewa kwa Mikwaju ya Penati kwenye Robo Fainali na Paraguay na kabla ya hapo walipata pigo baada ya Kepteni wao Neymar kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu na kisha kufungiwa Mechi 4.
Licha ya Brazil kumkosa Neymar kwenye Mechi yao na Chile, Nchi hiyo inarekodi nzuri dhidi ya Mabingwa hao wa Copa America.
Katika Mechi za Mchujo za Kombe la Dunia, Brazil wamefungwa mara moja tu na Chile, 3-0 kwenye Mechi za kuelekea Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2002, na tangu wakati huo wamecheza Mechi 14 na Brazil wameshinda 12 na Sare 2.
Katika Mechi yao ya mwisho kukutana, Kirafiki Mwezi Machi Jijini London, Brazil iliifunga Chile 1-0.

KOMBE LA DUNIA 2018
Marekani ya Kusini-Mechi za Mchujo
Alhamisi Oktoba 8

22:00 Bolivia v Uruguay
23:30 Colombia v Peru
Ijumaa Oktoba 9

00:01 Venezuela v Paraguay
02:30 Chile v Brazil
03:00 Argentina v Ecuador
Jumatano Oktoba 14
00:01 Ecuador v Bolivia
02:00 Uruguay v Colombia
04:00 Brazil v Venezuela
04:00 Paraguay v Argentina
05:15 Peru v Chile

TIMU ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo imetakata baada ya kuifunga Malawi `The Flames’ kwa mabao 2-0 katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam. Mabao ya Taifa Stars yalifungwa na wachezaji wa Tanzania wanaocheza soka la kulipwa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu.

Mabao yote ya Taifa Stars yalifungwa katika kipindi cha kwanza huku Samatta akiwa wa kwanza kuwainua wapenzi wa soka nchini kwa bao lake katika dakika ya 18 akipokea pasi safi kutoka kwa Ulimwengu. Ulimwengu alifunga la pili katika dakika ya 20, baada ya kipa wa Malawi, Simplex Nthala kutema mkwaju wa krosi wa Haji Mwinyi na Ulimwengu akauwahi mpira huo na kuusukumia kimiani na kuihakikishia Taifa Stars ushindi.

Mechi ilikuwa ni ngumu kwa kila upande, Malawi ndiyo waliopeleka mashambulizi mengi zaidi ya Taifa Stars hasa kataika dakika 15 za mwanzo. Lakini kuanzia dakika 20 hadi 35, Stars walionekana kuutawala mpira zaidi lakini Malawi hawakuwa wamelala, kwani nao walifanya mashambulizi ya kushtukiza.

Ushindi wa Taifa Stars ni faraja kubwa kwao, ambayo mara mbili ilicheza na Malawi katika mechi za kimataifa za kirafiki, Mwanza na Mbeya kwa nyakati tofauti na kutoka sare ya kufunga 1-1, na ile ya suluhu.
Pia ni furaha iliyoje kwa kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa ambaye juzi tu aliingia mkataba wa mwaka mmoja na nusu wa kuwa kocha mkuu wa timu hiyo baada ya awali kuwa na mkataba wa miezi mitatu kama kocha wa muda.
Mkwasa alipewa mikoba ya kuifundisha Taifa Stars kwa muda baada ya kutimuliwa kwa kocha Mholanzi Mart Nooij baada ya timu hiyo kufanya vibaya katika michezo mingi ikiwemo ya kimashindano na kirafiki.
Mbali na Mkwasa, Hemed Morocco naye alilamba mkataba kama msaidizi wa Mkwasa kwa kipindi hicho cha mwaka mmoja na nusu.
Tangu Mkwasa aanze kuifundisha timu hiyo imeshapata sare mbili dhidi ya Uganda katika mashindano ya Kombe la Chan ya mabao ya 1-1 na dhidi ya Nigeria ya 0-0 katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon).

Samatta amekuwa msaada mkubwa kwa TP Mazembe baada ya hivi karibuni kuiwezesha timu hiyo kutinga fainali ya Ligi ya Mabigwa wa Afrika baada ya kufunga mabao mawili wakati wakishinda 3-0.
TP Mazembe katika mchezo wa awali ilifungwa mabao 2-1 na kuifanya kutinga fainali kwa ushindi wa jumla ya mabao 4-2, ambapo sasa itacheza na USM Alger ya Algeria. Fainali hiyo itapigwa kati ya Oktoba 30 na Novemba mosi wakati ule wa marudiano utafanyika kati ya Novemba 6 na 8.


STRAIKA Chipukizi wa Manchester United Anthony Martial ameteuliwa kuwa ndio Mchezaji Bora wa Mwezi Agosti/Septemba katika Ligi Kuu England na kuzoa Tuzo ya PFA ya Mashabiki.

PFA [Professional Footballers Association] ni Chama cha Kutetea Hakika Wachezaji wa Kulipwa wa Soka huko Uingereza.

Martial, mwenye Miaka 19, alijiunga na Man United katika Siku ya mwisho ya Dirisha la Uhamisho, hapo Septemba 1, kutoka AS Monaco ya France kwa Dau la Pauni Milioni 36.
Katika Mechi zake mbili za kwanza alifunga Bao 3 na kuwa Mchezaji Bora wa Mechi Man United walipoifunga Sunderland 3-0.
Ubora wa Martial ndio uliifanya Man United kutwaa uongozi wa Ligi Kuu England mwishoni mwa Septemba kitu ambacho walikuwa hawajafanya kwa Miaka Miwili.
Katika kinyang’anyiro cha Tuzo hii, Martial aliwabwaga Riyad Mahrez wa Leicester City na Mchezaji mpya wa West Ham Dimitri Payet.
Wachezaji wengine waliokuwemo kwenye Listi ya awali ya mchujo ni Bafetimbi Gomis (Swansea City), Odion Ighalo (Watford), Vincent Kompany (Manchester City), Graziano Pelle (Southampton), David Silva (Manchester City), Jamie Vardy (Leicester City), Callum Wilson (Bournemouth) na Ashley Williams (Swansea).Washindi wa Tuzo hii ya Mchezaji Bora wa PFA kwa Mashabiki hupatikana kila Mwezi kupitia Kura inayoendeshwa na www.skysports.com baada ya Wataalam kupendekeza Majina ya Wachezaji wanaogombea.
Jopo la Wataalam hao ni pamoja na Wachambuzi wa Soka wa Sky Sports Paul Merson, Ian Holloway na Peter Beagrie walijumuika na Mike Riley, Meneja Mkuu wa of the Professional Game Match Officials, [PGMO ni Kampuni inayosimamia Marefa wa Ligi] na Malcolm Clarke, Mwenyekiti wa Shirikisho la Mashabiki wa Soka, pamoja na Shabiki anaeshinda Tuzo ya kila Mwezi.

waliotembelea blog