Friday, October 2, 2015

Kuchagua chuo sometimes inakuwa kazi ngumu sana kwasababu unajikuta na maswali mengi sana baadhi yakiwa; je campus unayoitaka ina mazingira mazuri ya kusomea, usafiri wa kufika chuoni unapatikana, huduma za maduka je zipo? lakini swali kubwa kuliko lote ni, je maisha ya mwanafunzi wa kawaida chuoni hapo yakoje!?
IGIG
Sasa kwa mujibu wa mtandao wa Time wa Marekani, wanafunzi waliomaliza High School yani A-level sasa hivi wameamua kutumia Instagram kuchagua vyuo vya kujiunga navyo! Yes Instagram mtu wangu, kwanini?
IGIG7
Kutokana na majibu ya utafiti uliyofanyika, wanafunzi wengi wamelalamika kuwa wanapata shida kujua vitu vidogo vidogo kuhusu vyuo wanavyofikiria kujiunga navyo, haswa kujua hali halisi ya maisha ya wanafunzi wa kawaida vyuoni… Wengine wamesema vipeperushi’ vinavyotolewa na vyuo vingi havijibu maswali ya hali halisi ya maisha vyuoni na ndio maana wengi wameamua kutumia Instagram ili waweze kuchunguza wenyewe maisha ya kawaida ya kila siku vyuoni yakoje, kujua kama vyuo hivyo vitawafaa!
IGIG3
Utafiti uliofanyika umesema kuwa social network ya Instagram siku hizi ina nafasi kubwa sana ya kumshawishi mwanafunzi kujiunga au kutojiunga na chuo husika kutokana na picha zinazopostiwa kwenye account za wanafunzi wa vyuo mbalimbali, zikionyesha mazingira halisi ya campus hizo pamoja na uhalisia wa maisha ya kila siku kitu ambacho hakipatikani kwenye vipeperushi vya matangazo au kwenye websites za vyuo vingi.
IGIG4
>>> “mimi binafsi nilichunguza account nyingi za watu kwenye Instagram ili kuona tu maisha ya kawaida ya wanafunzi yakoje… ni kama kufanya tour ya chuo husika bila wewe kwenda chuoni hapo na kutembelea kila sehemu yani ofisini, madarasa, viwanja vya michezo na hata kupata picha ya maisha ya kila siku … vyote navifanya kwenye Instagram sasa hivi! <<< Morgan Levy mwanafunzi.
IGIG5
>>> “kuna chuo kimoja nilikifuatilia lakini nikagundua kuwa wanafunzi wengi wa pale wanapenda sana starehe na party nyingi kitu ambacho sikukifurahia sana…” <<< Morgan Levy.
Hii imekaa poa sana mtu wangu kwasababu ni rahisi na wala haina gharama yoyote ile, au wewe unaonaje? Kitu hiki kitawafaa wanafunzi wetu wa Tanzania!?
Kocha wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson amemwambia nahodha wa Timu hiyo Wayne Rooney kuwa hatasita kumuacha kwenye kikosi hicho endapo ataendelea kucheza chini ya kiwango.
Kauli hii ya Kocha Hodgson inakuja baada ya mchezaji huyo ambaye pia ni nahodha wa Manchester United kuonesha kiwango duni ambapo ameshindwa kufunga bao lolote katika mechi kadhaa mpaka sasahivi .
Rooney kwenye msimu huu amefunga jumla ya mabao manne kwenye mechi 10, sita zikiwa mechi za ligi ambako amefunga bao moja na nne za ligi ya mabingwa akiwa amefunga mabao matatu.
Kocha Roy Hodgson amesema kuwa hatasita kumuweka benchi Rooney endapo hataonyesha kiwango.
Kocha Roy Hodgson.
Katika mchezo wa juzi kwenye ligi ya mabingwa, Rooney alikosa bao la wazi baada ya kupaisha juu mpira uliopigwa na mshambuliaji Anthony Martial akiwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga.
Hata hivyo Rooney atakuwa na nafasi ya kucheza kwenye mechi zinazofuata za England ambapo ataweza kuizidi rekodi ya gwiji Bobby Charlton kama mfungaji bora wa miaka yote wa timu ya taifa ya England.



Feneberhce ya Uturuki imejitutumua ikiwa ugenini Glasgow na kufanikiwa kupata sare ya mabao 2-2 katika michuano ya Kombe la Europa.

Ikiongozwa na Robin van Persie, Feneberhce ililazimika kusawazisha ikitoka chini kwa mabao 2-0 hadi kuwa 2-2.

Shuja alikuwa ni Fernandao ambaye alifunga mabao yote mawili ya kusawazisha katika dakika za 43 na 48.





TAIFA STARS
Tanzania imepanda nafasi nne katika viwango vya ubora vya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) lakini bado hali yake ni mbaya kwa jumla katika takwimu hizo zilizotolewa jana Alhamisi.


Takwimu hizo zinaonyesha kuwa Tanzania inashika nafasi ya 136 ikiwa ndiyo nchi ya chini kwa ubora kati ya zile zilizopo Afrika Mashariki katika chati hiyo.

Argentina imeendelea kubaki namba moja ikifuatiwa na Ujerumani ambayo imepanda kwa nafasi moja ikiishusha Ubelgiji iliyoshika nafasi ya tatu. Ureno imesogea mpaka nafasi ya nne wakati kwa nchi za Afrika inayoongoza ni Algeria ikiwa nafasi ya 19.

Viwango vya Fifa
1. Argentina
2. Ujerumani
3. Ubelgiji
4. Ureno
5. Colombia
6. Hispania
7. Brazil
8. Wales
9. Chile
10. England
93. Rwanda
75. Uganda
113. Burundi
131. Kenya
136. Tanzania

waliotembelea blog