Saturday, April 26, 2014

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete usiku wa kuamkia leo ametunuku nishani na Tuzo kwa viongozi mbalimbali wa kitaifa na watumishi wa umma wapatao 86 waliotoa mchango wao katika kuulinda na kuudumisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliodumu kwa miaka Hamsini 50.
Mama Maria Nyerere akipokea nishani ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano(Order) kwa niaba ya Marehemu Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Mama Maria Nyerere Nishani ya Kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungnao Daraja nne.

Mama Fatma Karume akipokea Nishani ya Kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano(Order) kwa niaba ya Marehemu Abeid Aman Karume Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa kwanza wa Baraza la Mapinduzi.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Mama Fatma Karume nishani ya kumbukumbu ya Miaka 50 ya Muungano Daraja Nne wakati wa hafla ya kutunuku nishani na tuzo za miaka 50 Muungano zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano ikulu jijini Dar es Salaam jana usiku.

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Rais mstaafu wa Awamu ya tatu Mh.Benjamin William Mkapa Nishani ya Kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano(Order) wakati wa sherehe ya kutunuku nishani na tuzo iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano ikulu jijini Dar es Salaam jana usiku.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtunuku Nishani ya Kumbukumbu ya miaka 50 ya Muungano Daraja la Kwanza Waziri Mkuu mstaafu ambaye pia alikuwa Mwenyekiti Tume ya kurekebisha Katiba  Mhe. JajiJoseph Sinde Warioba wakati wa Sherehe hizo zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano ikulu jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia jana Picha zote na Freddy Maro

 Waziri Mkuu na Mgeni Rasmi wa Mkesha wa Muungano Mizengo Pinda akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam kuongoza mamia ya wananchi waliohudhuria kwenye mkesha huo.Kushoto kwake ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Abdulrahman Kinana na kulia kwake ni Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Iddi 
 Wageni waaliwa ikiwemo Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika za Kimataifa.
 Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Mwansoko (katikati) akiwa na Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Joyce Fisoo (wa pili kushoto) na watumishi wengine wa Wizara hiyo.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad akiwasili kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja kujumuika katika Mkesha wa Muungano.Kulia kwake ni mwenyeji wake 
Kikindi cha Taifa cha Taarabu kikitumbuiza wananchi waliohudhuria kwenye mkesha na wimbo Maalum unaojulikana kama Muungano Wetu.  
 Kikundi cha Burudani kutoka Tanga kikuburudisha hadhira 
 Mzee Yusuf na Kundi lake la Jahaz Morden Taarabu.


 Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda, akiwaaga baadhi ya wageni waalikwa na kuondoka baada ya kuongoza Mkesha wa Muungano.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Seif Iddi, akitoa salamu zake kwa wananchi.
 Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda, akitoa neno kwa wananchi.
 Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda, akijiandaa kubofya kitufe cha kuashiria kuzaliwa upya kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 Maandishi Maalumu yakihamasishana kuashiria kutimia kwa Miaka 50 ya Muungano.
 Fashfash na fataki zikamiminika kwenye anga ya viwanja vya Mnazi Mmoja. 
 Profesa Mwansoko akizungumza na Televisheni One.
 Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda, akiwaaga baadhi ya wageni waalikwa na kuondoka baada ya kuongoza Mkesha wa Muungano.



Balozi mpya wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress akikaribishwa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Afisa Ubalozi Suleiman Saleh siku ya Alhamisi April 24, 2014 alipotembelea Ubalozi huo na kujitambulisha kwa Mhe. Balozi Liberata Mulamula (hayupo pichani)
Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha Balozi mpya wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Mark Childress kwa Maafisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani Balozi huyo alipotembelea Ubalozi huo siku ya Alhamisi April 24, 2014 jijini Washington, DC.
Mhe. Mark Childress akipokea zawadi toka kwa Balozi Liberata Mulamula.



Vijana wakiwa kwenye matembezi ya Uzalendo yalioratibiwa na Umoja wa Vijana wa CCM katika kuadhimisha miaka 50 ya Muungano ambapo vijana hao walianzia matembezi kutoka ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Temeke mpaka kwenye viwanja vya sabasaba na kulakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam Ndugu Ramadhani Madabida muda mchache kabla ya kupokea matembezi ya Uzalendo yaliofanywa na vijana mbali mbali .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa ameshikilia picha ya  Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage huku Rais wa Mapinduzi ya Zanzibar  Dk.Ali Mohamed Shein akiwa ameshikilia picha ya  Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Abeid Amani Karume baada ya kuzipokea kutoka kwa vijana waliofanya matembezi ya Uzalendo.


hqdefault_744f4.jpg
photo_f8ce8.jpg
Kocha wa zamani wa timu ya Barcelona Tito Vilanova amefariki dunia usiku huu akiwa hospitarini alipokuwa amerazwa akisumbuliwa na maradhi ya saratani ya koo.(AWADH IBRAHIM)


0L7C0250 888b4

0L7C0297 5e5bb


Sherehe za kuhadhimisha miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyozaa nchi ya Tanzania zimefanyika leo mjini Dar es Salaam na kupambwa kwa maonyesho mbali mbali ya kijeshi pamoja na halaiki zilizoandaliwa na watoto.
Marais wanne wa nchi za Afrika Afrika Mashariki akiwemo Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa Kenya na Pierre Nkurunzinza wa Burundi ni miongoni mwa marais waliohudhuria sherehe hizo.
Wengine ni Rais Joyce Banda wa Malawi, Mfalme Mswati III wa Swaziland, mfalme Letsie III wa Lesoto Makamu wa Rais wa Nigeria Mohammed Sambo, Makamu wa Rais wa Zambia Guy Scott, Waziri Mkuu wa Rwanda Piere Habumurenyi, Waziri Mkuu wa Misri Ibrahim Mahlab na Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki.
Katika maadhimisho yao pia kulikuwa na maonyesho ya silaha mbali mbali za kivita zikiwemo ndege za kivita pamoja na za kiraia.
Hata hivyo kilichovutia  ni kikosi cha makomandoo wa jeshi la Tanzania ambao walionyesha umahiri wao kupambana na adui bila kutumia silaha na kuvunja vitu vigumu kwa kutumia kichwa  na mikono.
Onyesho jingine lililotia fora zaidi ni askari wa miamvuli ambao waliruka kutoka kwenye ndege umbali wa futi elfu arobaini  kutoka usawa wa bahari kwa kutumia miavuli na kutua katikati ya uwanja wa sherehe.


IMG-20140426-WA0034_af1cd.jpg
IMG-20140426-WA0035_686a4.jpg
Umati wa watu waliohudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea hivi sasa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, maonyesho haya yanajumuisha shughuli mbalimbali zikiwemo maonyesho. Maadhimisho haya yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoaka mataifa mbalimbali

Tuesday, April 22, 2014


UEFA CHAMPIONS LIGI, LEO Jumanne na Jumatano Usiku zitakuwa na Mechi zake za Kwanza za Nusu Fainali huko Jijini Madrid Nchini Spain.
LEO Jumanne, ndani ya Estadio Vicente Calderon, Vinara wa La Liga, Atletico Madrid, wataikaribisha Chelsea ya Engand.
Siku ya Pili yake, yaani Jumatano Usiku, huko Santiago Bernabaeu, Real Madrid watakuwa Wenyeji wa Mabingwa Watetezi wa UCL, Bayern Munich.



ATLETICO MADRID v CHELSEA:
Jose Mourinho ameshawahi kuifikisha Chelsea mara 2 Nusu Fainali ya UCL, Mwaka 2005 na 2007, na kutolewa na Liverpool.

Lakini safari hii wapo Uwanja wa Vicente Calderon ambao Atletico Madrid hawajafungwa hata Mechi moja ya La Liga Msimu huu na wanaongoza Ligi hiyo ya Spain wakiwa Pointi 4 mbele ya Barcelona.
Chelsea watatinga kwenye Mechi hii bila ya Fulbeki wao Branislav Ivanovic ambae amefungiwa na hili linaweza kumrudisha Kikosini Mkongwe Ashley Cole ambae amepoteza namba kwa Cesar Azpilicueta ambae atapelekwa Fulbeki ya Kulia na Cole kucheza kushoto.



Hatimaye kocha Manchester United David Moyes amefukuzwa kazi, miezi 10 baada ya kumrithi Sir Alex Ferguson.
United jana waligoma kuthibitisha kuhusu ripoti kwamba Moyes angefukuzwa mwishoni mwa msimu.
Moyes, 50, alichaguliwa na Sir Alex Ferguson kumrithi wakati kocha huyo mwenye 72, alipoamua kustaafu baada ya miaka 26 mwaka jana baada ya ligi kuisha.
Moyes aliondoka Everton na kusaini mkataba wa miaka sita na mabingwa ya Premier league.
Kwenye taarifa rasmi, klabu ilisema: “Tungependa kumshukuru kwa kazi nzuri aliyoifanya, uaminifu wake aliokuwa nao kwenye kazi yake”.
Ryan Giggs kwa pamoja na Nicky Butt watashika majukumu ya ukocha mpaka mwishoni mwa msimu.

Mashabiki wa United wakiwa wachache Uwanjani wakati wa malumbano ya hapa na pale kabla ya mtanange huku wakishinikiza baongo la  'Chosen One' kuondolewa uwanjani hapo..

Moyes akiwa amebeba kombe la Ngao ya Jamii (Community Shield) baada ya Man  United kuifunga Wigan bao 2-0 kwenye uwanja wa  Wembley mwezi wa Nane kipindi cha nyuma.

Saturday, April 19, 2014


Wakristo duniani kote wanajiandaa kusherehekea Sikukuu ya Pasaka. Ingawa si madhehebu yote ya Kikristo yanayosheherehea kwa uzito sawa, katika kalenda ya Kanisa Katoliki, Pasaka ni furaha ya kusherehekea kufufuka kwa Yesu.
Ijumaa Kuu
Ijumaa Kuu ni siku ambayo wakristo wanaadhimisha kufa, kuzikwa kwa Yesu, tukio lililotokea katika mji wa Yerusalemu siku ya Ijumaa.
Kulingana na Mtume Yohane, kesho yake, yaani baada ya Ijumaa, ilikuwa Sabato na ikafuatia na Pasaka yenyewe siku ya Jumapili. Ijumaa Kuu ni sehemu ya Juma Kuu linaloanza kwa adhimisho la Yesu kuingia mji huo wa Yerusalemu akishangiliwa kama mfalme wa Wayahudi. Ijumaa Kuu pia ni sehemu ya siku tatu kuu za Pasaka zinazoadhimisha mateso na kifo chake, kuzikwa kaburini, na hatimaye kufufuka.
Umuhimu wa Pasaka
Pasaka ni moja ya sikukuu kubwa sana kwa Wakristo. Pamoja na kuwa imeendelea kuchukuliwa kama tukio la kihistoria tu, bado dhana yake ya kuonyesha upendo wa Mungu kwa wanadamu haitapotea. Ni upendo wa kutoa moja ya nafsi za Mungu, iteswe, isulubiwe, ife na kisha ifufuke kudhihirisha utukufu wa Mungu na upendo wake kwa wanadamu.
Lakini kwa sisi wanadamu wa leo Pasaka ni nini?
Kuna umuhimu gani wa kuendelea kukumbuka Sikukuu ya Pasaka? Ni mafundisho gani tunayoyapata juu ya siku hii? Pasaka ni sikukuu ya kufufuka kwa Yesu Kristo na ni sikukuu muhimu kwa Wakristo, watu huenda kanisani na kusherekea sikukuu hii ya kidini.
Wakristo pote ulimwenguni husherekea Pasaka kwa furaha kubwa sana kwa sababu wanaiona ndio siku ambayo mwokozi wao huwa amefufuka. Watu wengi huvalia nguo mpya kwenda kanisani siku ya Pasaka.
Kuna alama nyingi zinazotambulisha siku ya Pasaka, moja ni msalaba ambao Wakristo, huuona kama alama ya ushindi wa Kristo dhidi ya kifo. Msalaba mara nyingi hutokea kama alama ya Pasaka. Watu katika sehemu nyingi ya ulimwengu huoka keki maalumu ziitwazo 'mikate ya moto ya msalaba'.
Mishumaa 
Taa, mishumaa na moto mkubwa wa sherehe inatoa ishara ya kusherekea kwa Pasaka katika baadhi ya nchi.
Wakatoliki katika baadhi ya nchi huzima taa zote katika makanisa yao siku ya Ijumaa kuu. Jioni ya siku inayotangulia Pasaka, hutengeneza moto mpya kuwashia mshumaa mkubwa wa Pasaka kuashiria siku na mambo mapya ndani ya ufufuo mpya wa Yesu.
Hutumia mshumaa huu kuwashia mishumaa mingine yote kanisani. Halafu huwasha mishumaa yao nyumbani ili itumike katika nyakati za sherehe maalumu.
Katika sehemu za Ulaya Kaskazini na Kati,watu huchoma moto mkubwa wa sherehe katika vilele vya milima. Halafu hujikusanya kuzunguka huo moto mkubwa na kuimba nyimbo na mashairi ya Pasaka.
Mwanzo wa Pasaka
Wakristo hufanya ibada ya siku 40; kipindi cha mfungo na sala hujulikana kama Kwaresma.Inakumbusha siku 40 za Kristo kufunga na kwenda jangwani.
Wiki ya mwisho ya Kwaresma iitwayo wiki takatifu hutukuza matukio ya wiki ya mwisho wa maisha ya Yesu Kristo kuwepo duniani, na inaanza katika Jumapili ya Matawi. Imetajwa hivyo kwa sababu ya matawi ambayo watu waliyatawanya kabla Yesu kristo hajaingia Yerusalemu kwa kushangiliwa
kwa shangwe kubwa.
Katika Alhamisi ya wiki ya mwisho ya Kwaresma kabla ya Ijumaa Kuu, Wakristo hukumbuka chakula cha mwisho cha Yesu Kristo cha jioni wakati walipoosha nyayo za miguu yao.
Waliiona Ijumaa Kuu ya kusulubiwa kwa Yesu kristo katika namna au njia ya huzuni na majonzi na kutumia Jumamosi takatifu katika fikra ya mambo yatakayotokea mbeleni katika Jumapili ya Pasaka. 

waliotembelea blog